Imeandikwa na Na Joseph Lugendo;
Tarehe: 28th November 2009
TANZANIA imeweka rekodi ya aina yake barani Afrika kwa kuibuka nchi pekee yenye wananchi wenye mapenzi makubwa kwa taifa lao kuliko jambo au mfumo wowote wa kitamaduni, kiuchumi au kijamii unaowagawa katika makundi mbalimbali na matabaka.
Rekodi hiyo ambayo ni moja ya kigezo cha nchi iliyo na ulinzi imara, imepatikana baada ya wananchi wa nchi za Afrika, wakiwemo Watanzania, kufanyiwa mahojiano maalumu kuhusu jambo la fahari wanalodhani ni muhimu kujitambulisha nalo kati ya mambo kadha wa kadha yanayotumika kumtambulisha mwanadamu.
Vigezo vingine vinavyoifanya nchi kuwa na ulinzi imara na madhubuti licha ya uzalendo wa wananchi wake kulipenda taifa lao ni teknolojia ya vita, ushirikiano mzuri na nchi marafiki zikiwemo nchi jirani, wingi wa wanajeshi, bajeti inayotumika kwa ajili ya ulinzi na usalama na idadi ya watu.
Katika mahojiano hayo yaliyohusisha wananchi kati ya 1,200 na 2,400 katika kila nchi kati ya nchi 16 zilizochaguliwa kufanya utafiti kuhusu ujenzi wa taifa katika nchi za Afrika, wananchi waliulizwa maswali ili kubaini iwapo wanajisikia fahari zaidi kutambulishwa kwa jina la taifa lao kwa mfano Mtanzania, au kwa jina la kitu kingine haswa kabila.
Kwa mujibu wa maoni ya utafiti huo uliofanywa na taasisi ya kimataifa ya utafiti ya Afro Barometer yenye makao makuu nchini Ghana na kuongozwa na Amanda Lea Robinson wa Chuo Kikuu cha Stanford, Marekani ulionesha kuwa waliojisikia fahari kutambuliwa kwa mataifa yao zaidi ya kitu kingine ilikuwa asilimia 42 ya wahojiwa wote wanaofikia 22,765.
Tanzania ni ya pekee, ambapo asilimia 88 wanaelezea kulipenda zaidi taifa lao, hata wale ambao kabila lao lilikuwepo katika orodha asilimia 87 walisema wanajisikia fahari kutambulishwa kwa taifa lao, alieleza msomi huyo katika utafiti wake huo.
Robinson ambaye ni mwanafunzi wa Shahada ya Uzamivu (PhD) katika Idara ya Sayansi ya Siasa ya Stanford University anasema katika utafiti huo uliotolewa Septemba mwaka huu kwamba wakati wastani wa wanaopenda mataifa yao katika nchi hizo ni asilimia 42 ya wahojiwa, kwa Tanzania wanaolipenda taifa lao ni asilimia 88 ya wahojiwa wote.
Alifafanua kuwa mapenzi hayo kwa taifa yanaweka mazingira mazuri ya kukua kwa demokrasia kwa kuwa mtu hatazuiwa haki yake ya kuchaguliwa kwa kigezo cha kuwepo katika kikundi fulani ambayo pia itachangia kukua kwa uchumi na maendeleo ya watu.
Hii nimeipenda zaidi. Jamani kumbe sisi ni wazalendo kiasi hiki sasa kwanini tunaendelea kuwa maskini? uzalendo huu ungesaidia sana kuliweka taifa katika maendeleo ya kiuchumi na kiutamaduni. Mbona wazalendo sisi ni mafisadi, au wanaohusika na ufisadi si WATANZANIA?
Je asilimia 88 ya watu waliohojiwa hawa hawamo katika wimbi la ufisadi kuanzia ofisi za wevyeviti wa vijiji, kata,tarafa etc? je hakukuwa na hawa manesi wanaotuzalisha baada ya kuwapa 5000 kinyume cha hapo unazaa mwenyewe yeye anakunywa chai yake akisoma gazeti?
Je hawa hawajahusika na kashfa za kugawa mashamba ya wanakijiji wenzao kwa wageni? Je hawa 88 wamo pia wahanga wa mabomu mbagala? je wamachinga na wa vibaka pia wamo? bila kusahau trafiki na madereva wa daladala! je wamo viongozi waandamizi wa serikali, je wamo wahadhiri wa vyuo ambao baadhi yao hupenda kutoa digrii za ch..i? wawakilishi watu je?
Kama hawa wote na wengine walikuwepo katika sample hii Je wali respond uongo tu kwenye mahojiano au ndio dhamira zao za kweli?
Kama ni dhamira za kweli jamani kwanini sisi ni maskini sasa? wazalendo wenzangu nisaidieni maana nafahamu kuwa hata kuwa JF tumesukumwa na uzalendo wetu pia
Tarehe: 28th November 2009
TANZANIA imeweka rekodi ya aina yake barani Afrika kwa kuibuka nchi pekee yenye wananchi wenye mapenzi makubwa kwa taifa lao kuliko jambo au mfumo wowote wa kitamaduni, kiuchumi au kijamii unaowagawa katika makundi mbalimbali na matabaka.
Rekodi hiyo ambayo ni moja ya kigezo cha nchi iliyo na ulinzi imara, imepatikana baada ya wananchi wa nchi za Afrika, wakiwemo Watanzania, kufanyiwa mahojiano maalumu kuhusu jambo la fahari wanalodhani ni muhimu kujitambulisha nalo kati ya mambo kadha wa kadha yanayotumika kumtambulisha mwanadamu.
Vigezo vingine vinavyoifanya nchi kuwa na ulinzi imara na madhubuti licha ya uzalendo wa wananchi wake kulipenda taifa lao ni teknolojia ya vita, ushirikiano mzuri na nchi marafiki zikiwemo nchi jirani, wingi wa wanajeshi, bajeti inayotumika kwa ajili ya ulinzi na usalama na idadi ya watu.
Katika mahojiano hayo yaliyohusisha wananchi kati ya 1,200 na 2,400 katika kila nchi kati ya nchi 16 zilizochaguliwa kufanya utafiti kuhusu ujenzi wa taifa katika nchi za Afrika, wananchi waliulizwa maswali ili kubaini iwapo wanajisikia fahari zaidi kutambulishwa kwa jina la taifa lao kwa mfano Mtanzania, au kwa jina la kitu kingine haswa kabila.
Kwa mujibu wa maoni ya utafiti huo uliofanywa na taasisi ya kimataifa ya utafiti ya Afro Barometer yenye makao makuu nchini Ghana na kuongozwa na Amanda Lea Robinson wa Chuo Kikuu cha Stanford, Marekani ulionesha kuwa waliojisikia fahari kutambuliwa kwa mataifa yao zaidi ya kitu kingine ilikuwa asilimia 42 ya wahojiwa wote wanaofikia 22,765.
Tanzania ni ya pekee, ambapo asilimia 88 wanaelezea kulipenda zaidi taifa lao, hata wale ambao kabila lao lilikuwepo katika orodha asilimia 87 walisema wanajisikia fahari kutambulishwa kwa taifa lao, alieleza msomi huyo katika utafiti wake huo.
Robinson ambaye ni mwanafunzi wa Shahada ya Uzamivu (PhD) katika Idara ya Sayansi ya Siasa ya Stanford University anasema katika utafiti huo uliotolewa Septemba mwaka huu kwamba wakati wastani wa wanaopenda mataifa yao katika nchi hizo ni asilimia 42 ya wahojiwa, kwa Tanzania wanaolipenda taifa lao ni asilimia 88 ya wahojiwa wote.
Alifafanua kuwa mapenzi hayo kwa taifa yanaweka mazingira mazuri ya kukua kwa demokrasia kwa kuwa mtu hatazuiwa haki yake ya kuchaguliwa kwa kigezo cha kuwepo katika kikundi fulani ambayo pia itachangia kukua kwa uchumi na maendeleo ya watu.
Hii nimeipenda zaidi. Jamani kumbe sisi ni wazalendo kiasi hiki sasa kwanini tunaendelea kuwa maskini? uzalendo huu ungesaidia sana kuliweka taifa katika maendeleo ya kiuchumi na kiutamaduni. Mbona wazalendo sisi ni mafisadi, au wanaohusika na ufisadi si WATANZANIA?
Je asilimia 88 ya watu waliohojiwa hawa hawamo katika wimbi la ufisadi kuanzia ofisi za wevyeviti wa vijiji, kata,tarafa etc? je hakukuwa na hawa manesi wanaotuzalisha baada ya kuwapa 5000 kinyume cha hapo unazaa mwenyewe yeye anakunywa chai yake akisoma gazeti?
Je hawa hawajahusika na kashfa za kugawa mashamba ya wanakijiji wenzao kwa wageni? Je hawa 88 wamo pia wahanga wa mabomu mbagala? je wamachinga na wa vibaka pia wamo? bila kusahau trafiki na madereva wa daladala! je wamo viongozi waandamizi wa serikali, je wamo wahadhiri wa vyuo ambao baadhi yao hupenda kutoa digrii za ch..i? wawakilishi watu je?
Kama hawa wote na wengine walikuwepo katika sample hii Je wali respond uongo tu kwenye mahojiano au ndio dhamira zao za kweli?
Kama ni dhamira za kweli jamani kwanini sisi ni maskini sasa? wazalendo wenzangu nisaidieni maana nafahamu kuwa hata kuwa JF tumesukumwa na uzalendo wetu pia