Nashukuru, umenielewa vizuri. Sina maana kwamba mhimili unawalinda wezi, ninachojaribu kuzungumzia ni pale ambapo wizi wa wazi kabisa umetokea, wezi wanafahamika lakini aliyepaswa kuwachukulia hatua kali kabisa ili iwe fundisho kwa wengine, naye amekaa kimya.
Kwa mfano, wewe ni mlinzi halafu wezi wanakuja kuiba mali unazozilinda, wanafanikiwa kuondoka na hizo mali, wakati huo wezi wamekuja na Mapanga lakini wewe kama mlinzi una AK-47. Mwishowe unaanza kulalamika eti umeibiwa. Mbaya zaidi ni kwamba, wezi wanafahamika, uwezo wa kuwachukulia hatua kali unao, lakini huchukui hatua.
Je, katika hali ya kawaida, wewe kama mlinzi sisi tutakutafsiri vipi?