Watanzania tunajitambua kweli?

Watanzania tunajitambua kweli?

GOTILANGU

Senior Member
Joined
Aug 23, 2013
Posts
182
Reaction score
46
Huwa hatuishi kulalamika kila siku tunaonewa , tunaonewa na chama tawala. Utasikia oooh CCM wezi, CCM mafisadi, CCM wao kwanza na tunalalamika kwelikweli ooh CCM wameharibu elimu yetu oooh CCM shaghalabaghala kila siku yaani haiwezi kupita siku hakuna malalamiko juu ya chama tawala chama alichokianzisha baba Wa taifa hili ambae twamuheshimu sana karibia watanzania wote.

TUNALALAMIKA TUNAHITAJI NINI?

Utasikia tunahitaji chama kingine hiki kimechoka kimeshindwa kutatua matatizo ya umma yaani ya wananchi na kimefanya maisha yamekuwa magumu sana. Ukiendelea kuuliza utaambiwa ni chama cha mafisadi kinatumia rasilimali kwa ajili ya wachache na wengi wamebaki na maisha magumu sana.
Utasikia chama hiki kina viongozi wengi wachumia tumbo, wafanyabiashara oooh utasikia chama sasa sio cha wafanyakazi na wakulima bali cha wafanyabiashara. Ukufika hapo usiendelee kuuliza utaambiwa mengi sana na watanzania hawa!
Kinachonifurahisha mimi na suala la zuri wanataka mabadiliko kupitia sanduku la kura na ukienda katika mitandao ya Simu hasa watsupp watu wameunda magroup ya majimbo wanaotoka na yakiwa na kauli mbiu kabisa wengine, KIBOVU HAKIPITI MWAKA HUU, WANANCHI KWANZA, TUNAHITAJI MABADILIKO ili mradi tu mambo yaende na yawe!

Pamoja na hari hiyo na kulalamika kote huko watanzania tumekuwa hatujui tunahitaji nini kutoka chama tawala na wala hatujui tufanye nini ili kupata tunachohitaji kutoka chama tawala.

KWANINI?

1: CHADEMA walikuja na kuwa chama cha matumaini sana tu na kutoa focus ya kuleta mabadiliko na watu walianza kuimba na kusema huu ni mpango Wa Mungu na CHADEMA kinakuja kukomboa Watanzania. Kilichotokea na kinachosikitisha sana ni pale Watanzania hawa badala ya kuungana kujua wanahitaji nini wafanyeje wamekuja na kauli ACT wazalendo chama kinachokuja kukomboa watanzania.
Hapa ndio msingi wa swali langu WATANZANIA TUNAJITAMBUA? tutaendelea kuimba hizi nyimbo mpka lini? Wengi hapa ni wasomi wanajua maana ya DIVIDE AND RULE na wengine ni maprofessor na walimu wazuri wamekubali dhana hii iendelee kutotufikisha tunapopahitaji.
Najiuliza tutaendelea kuwa katika kipindi cha mpito mpaka lini? Cha kusubiri kuondokana na huu tunaouhita uonevu, tunajua kama tunaonewa? Tumechagua njia sahihi ya sanduku la kura kipi kinachotugawa? kipi kinachotupofusha? Kwanini tumekubali kusalitiana na tunaanangaliana pasipo kuambiana ukweli? Kwanini kwa pamoja hatujaamua kuondokana na Yale tunayoyaona ni matatizo yanayoikwamisha nchi yetu.

Nasikitika sana kuona Mtanzania anaendelea kufikiria kipindi cha mpito tena wakati mwafaka umefika 2015 wakufanya maamuzi sahihi kwa Yale tunayo yalalamikia kama kweli yapo!
Kushindwa kuungana pamoja na kushindwa kujitambua kwetu ni kumaanisha hatusikii machungu ni kuendelea kusema kuwa ni sahihi chama tawala na serikali yake kilichofanya kuhusu Rasimu ya katiba, EPA, ESCROW, Buzwagi, Richmond, Elimu, madaraka yakupokezana, ajira na mengineyo.
Tusipofanya maamuzi ya kile tunacholalamikia wakati huu kwa upofu Wa kutoona ukweli kwa upofu Wa ushabiki Wa MTU mmoja au kwa manufaa ya MTU mmoja ni kutokujitambua.

Kama tumeamua Watanzania tuachane na vyama vipya tuungane kupitia muungano Wa UKAWA na vyama visivyotaka muungano huu tuviache kabisa vifanye siasa yao pamoja na CCM sisi tuamue kutumia sanduku la kura kufuta kile tunachokilalamikia miaka yote. Hizi porojo Rushwa ndogo ndogo na kuwa kipofu kwa ukweli uliopo ni matusi makubwa sana.

WATANZANIA TUJITAMBUE TUTAENDELEA KUWA KATIKA KIPINDI CHA MPITO MPAKA LINI?
 
Ndugu,
Unaonekana kwa namna fulani una machungu na nchi hii kama walivyo watanzania wengi,ni vizuri
Mtazamo wako unaonekana kuwalaumu/kutulaumu wananchi zaidi bila kuwagusa viongozi wa vyama vya upinzani ambao kwa kiasi kikubwa ni washika dau wakubwa.
Quote: "Kwanini tumekubali kusalitiana na tunaanangaliana pasipo kuambiana ukweli?"
Tumekuwa tukipiga makelele kuhusu mabaya wanayofanya CCM lakini ndani ya vyama vya upinzani kumekuwa na yaleyale ambayo tunaipigia kelele CCM huu ni unafki,eg rushwa,ufujaji/matumizi mabaya ya fedha,uroho wa madaraka
NDUGU KAMA UNATAKA TUIONDOE CCM basi kweli tuambiane ukweli bila kuoneana aibu kwa kila anayekosea
Nachukulia Mfano wa Chadema: Nakuuliza swali moja nijibu Honestly nitajua kwamba lawama unazotoa kwa watanzania zinastahiki au hazina msingi
QN: Inakuwaje Uongozi wa Chadema unaruhusu ubadilishaji wa katiba usio wa kihalali ili tu Kumruhusu mtu mmoja aendelee kutawala? huu sio uroho wa madaraka tunaowapigia kelele CCM? Kwani hakuna watu wengine ndani ya Chama wenye uwezo wa kuongoza chama? Au unataka kuniambia unasubiri watakaokuwa Courageous enough kuchallenge hilo uje uwaite wasaliti? au umuite mroho wa madaraka?
Mpaka tutakapoweza kuwa na ushujaa wa kuambiana ukweli katika nyuso zetu katika maswala kama hayo ndipo CCM itakapotoka madarakani.
 
Naona mtoa mada umekula kimya? imeingia eeh? Bitter Truth.

Ndo siasa za bongo kila mtu anataka madaraka angalia aliyeingia ACT within days na kuwa kiongozi Mkuu wa chama as if hapakuwa na mwingine yeyote anayeweza kuwa yote hayo ni kutaka madaraka!! Hivi vyama havina tija kwa taifa hata kimoja....
 
ila zito atakuja kutwa na laana mbaya sana...ameuza watanzania vibaya mno
 
Ukombozi utakuja pale vijana watakapokombolewa kifikra.waondokane na fikra za kuvutwa huku na huku.leo cdm kesho act.
 
measkron said:
Ndo siasa za bongo kila mtu anataka madaraka angalia aliyeingia ACT within days na kuwa kiongozi Mkuu wa chama as if hapakuwa na mwingine yeyote anayeweza kuwa yote hayo ni kutaka madaraka!! Hivi vyama havina tija kwa taifa hata kimoja....
Ninyi mlimtaka Zitto baada ya kumfukuza akafanye nini?Apewe cheo gani?Kwa muda gani ili mridhike?
 
Ndo siasa za bongo kila mtu anataka madaraka angalia aliyeingia ACT within days na kuwa kiongozi Mkuu wa chama as if hapakuwa na mwingine yeyote anayeweza kuwa yote hayo ni kutaka madaraka!! Hivi vyama havina tija kwa taifa hata kimoja....
Wengine wapo ila yeye ndo ameonekana anafaa kwa sasa,cha muhimu tu Katiba haijakanyagwa.Kitu ambacho ni kinyume kwa vyama vingine eg Chadema.
 
Back
Top Bottom