Huwa hatuishi kulalamika kila siku tunaonewa , tunaonewa na chama tawala. Utasikia oooh CCM wezi, CCM mafisadi, CCM wao kwanza na tunalalamika kwelikweli ooh CCM wameharibu elimu yetu oooh CCM shaghalabaghala kila siku yaani haiwezi kupita siku hakuna malalamiko juu ya chama tawala chama alichokianzisha baba Wa taifa hili ambae twamuheshimu sana karibia watanzania wote.
TUNALALAMIKA TUNAHITAJI NINI?
Utasikia tunahitaji chama kingine hiki kimechoka kimeshindwa kutatua matatizo ya umma yaani ya wananchi na kimefanya maisha yamekuwa magumu sana. Ukiendelea kuuliza utaambiwa ni chama cha mafisadi kinatumia rasilimali kwa ajili ya wachache na wengi wamebaki na maisha magumu sana.
Utasikia chama hiki kina viongozi wengi wachumia tumbo, wafanyabiashara oooh utasikia chama sasa sio cha wafanyakazi na wakulima bali cha wafanyabiashara. Ukufika hapo usiendelee kuuliza utaambiwa mengi sana na watanzania hawa!
Kinachonifurahisha mimi na suala la zuri wanataka mabadiliko kupitia sanduku la kura na ukienda katika mitandao ya Simu hasa watsupp watu wameunda magroup ya majimbo wanaotoka na yakiwa na kauli mbiu kabisa wengine, KIBOVU HAKIPITI MWAKA HUU, WANANCHI KWANZA, TUNAHITAJI MABADILIKO ili mradi tu mambo yaende na yawe!
Pamoja na hari hiyo na kulalamika kote huko watanzania tumekuwa hatujui tunahitaji nini kutoka chama tawala na wala hatujui tufanye nini ili kupata tunachohitaji kutoka chama tawala.
KWANINI?
1: CHADEMA walikuja na kuwa chama cha matumaini sana tu na kutoa focus ya kuleta mabadiliko na watu walianza kuimba na kusema huu ni mpango Wa Mungu na CHADEMA kinakuja kukomboa Watanzania. Kilichotokea na kinachosikitisha sana ni pale Watanzania hawa badala ya kuungana kujua wanahitaji nini wafanyeje wamekuja na kauli ACT wazalendo chama kinachokuja kukomboa watanzania.
Hapa ndio msingi wa swali langu WATANZANIA TUNAJITAMBUA? tutaendelea kuimba hizi nyimbo mpka lini? Wengi hapa ni wasomi wanajua maana ya DIVIDE AND RULE na wengine ni maprofessor na walimu wazuri wamekubali dhana hii iendelee kutotufikisha tunapopahitaji.
Najiuliza tutaendelea kuwa katika kipindi cha mpito mpaka lini? Cha kusubiri kuondokana na huu tunaouhita uonevu, tunajua kama tunaonewa? Tumechagua njia sahihi ya sanduku la kura kipi kinachotugawa? kipi kinachotupofusha? Kwanini tumekubali kusalitiana na tunaanangaliana pasipo kuambiana ukweli? Kwanini kwa pamoja hatujaamua kuondokana na Yale tunayoyaona ni matatizo yanayoikwamisha nchi yetu.
Nasikitika sana kuona Mtanzania anaendelea kufikiria kipindi cha mpito tena wakati mwafaka umefika 2015 wakufanya maamuzi sahihi kwa Yale tunayo yalalamikia kama kweli yapo!
Kushindwa kuungana pamoja na kushindwa kujitambua kwetu ni kumaanisha hatusikii machungu ni kuendelea kusema kuwa ni sahihi chama tawala na serikali yake kilichofanya kuhusu Rasimu ya katiba, EPA, ESCROW, Buzwagi, Richmond, Elimu, madaraka yakupokezana, ajira na mengineyo.
Tusipofanya maamuzi ya kile tunacholalamikia wakati huu kwa upofu Wa kutoona ukweli kwa upofu Wa ushabiki Wa MTU mmoja au kwa manufaa ya MTU mmoja ni kutokujitambua.
Kama tumeamua Watanzania tuachane na vyama vipya tuungane kupitia muungano Wa UKAWA na vyama visivyotaka muungano huu tuviache kabisa vifanye siasa yao pamoja na CCM sisi tuamue kutumia sanduku la kura kufuta kile tunachokilalamikia miaka yote. Hizi porojo Rushwa ndogo ndogo na kuwa kipofu kwa ukweli uliopo ni matusi makubwa sana.
WATANZANIA TUJITAMBUE TUTAENDELEA KUWA KATIKA KIPINDI CHA MPITO MPAKA LINI?
TUNALALAMIKA TUNAHITAJI NINI?
Utasikia tunahitaji chama kingine hiki kimechoka kimeshindwa kutatua matatizo ya umma yaani ya wananchi na kimefanya maisha yamekuwa magumu sana. Ukiendelea kuuliza utaambiwa ni chama cha mafisadi kinatumia rasilimali kwa ajili ya wachache na wengi wamebaki na maisha magumu sana.
Utasikia chama hiki kina viongozi wengi wachumia tumbo, wafanyabiashara oooh utasikia chama sasa sio cha wafanyakazi na wakulima bali cha wafanyabiashara. Ukufika hapo usiendelee kuuliza utaambiwa mengi sana na watanzania hawa!
Kinachonifurahisha mimi na suala la zuri wanataka mabadiliko kupitia sanduku la kura na ukienda katika mitandao ya Simu hasa watsupp watu wameunda magroup ya majimbo wanaotoka na yakiwa na kauli mbiu kabisa wengine, KIBOVU HAKIPITI MWAKA HUU, WANANCHI KWANZA, TUNAHITAJI MABADILIKO ili mradi tu mambo yaende na yawe!
Pamoja na hari hiyo na kulalamika kote huko watanzania tumekuwa hatujui tunahitaji nini kutoka chama tawala na wala hatujui tufanye nini ili kupata tunachohitaji kutoka chama tawala.
KWANINI?
1: CHADEMA walikuja na kuwa chama cha matumaini sana tu na kutoa focus ya kuleta mabadiliko na watu walianza kuimba na kusema huu ni mpango Wa Mungu na CHADEMA kinakuja kukomboa Watanzania. Kilichotokea na kinachosikitisha sana ni pale Watanzania hawa badala ya kuungana kujua wanahitaji nini wafanyeje wamekuja na kauli ACT wazalendo chama kinachokuja kukomboa watanzania.
Hapa ndio msingi wa swali langu WATANZANIA TUNAJITAMBUA? tutaendelea kuimba hizi nyimbo mpka lini? Wengi hapa ni wasomi wanajua maana ya DIVIDE AND RULE na wengine ni maprofessor na walimu wazuri wamekubali dhana hii iendelee kutotufikisha tunapopahitaji.
Najiuliza tutaendelea kuwa katika kipindi cha mpito mpaka lini? Cha kusubiri kuondokana na huu tunaouhita uonevu, tunajua kama tunaonewa? Tumechagua njia sahihi ya sanduku la kura kipi kinachotugawa? kipi kinachotupofusha? Kwanini tumekubali kusalitiana na tunaanangaliana pasipo kuambiana ukweli? Kwanini kwa pamoja hatujaamua kuondokana na Yale tunayoyaona ni matatizo yanayoikwamisha nchi yetu.
Nasikitika sana kuona Mtanzania anaendelea kufikiria kipindi cha mpito tena wakati mwafaka umefika 2015 wakufanya maamuzi sahihi kwa Yale tunayo yalalamikia kama kweli yapo!
Kushindwa kuungana pamoja na kushindwa kujitambua kwetu ni kumaanisha hatusikii machungu ni kuendelea kusema kuwa ni sahihi chama tawala na serikali yake kilichofanya kuhusu Rasimu ya katiba, EPA, ESCROW, Buzwagi, Richmond, Elimu, madaraka yakupokezana, ajira na mengineyo.
Tusipofanya maamuzi ya kile tunacholalamikia wakati huu kwa upofu Wa kutoona ukweli kwa upofu Wa ushabiki Wa MTU mmoja au kwa manufaa ya MTU mmoja ni kutokujitambua.
Kama tumeamua Watanzania tuachane na vyama vipya tuungane kupitia muungano Wa UKAWA na vyama visivyotaka muungano huu tuviache kabisa vifanye siasa yao pamoja na CCM sisi tuamue kutumia sanduku la kura kufuta kile tunachokilalamikia miaka yote. Hizi porojo Rushwa ndogo ndogo na kuwa kipofu kwa ukweli uliopo ni matusi makubwa sana.
WATANZANIA TUJITAMBUE TUTAENDELEA KUWA KATIKA KIPINDI CHA MPITO MPAKA LINI?