Salam ndefu inaonyesha hulka nzuri katika mawasiliano ya wawili hao au kundi hilo. Huwezi ukawa too short kwa watu wako wa karibu, inabidi uongee ili kuweka bond kati yenu. Kuna msemo wa kizungu wansema "silence is a rerationship killer", Ukiwa mkimya mwenzio au mtu wako wa karibu anatafsiri labda anakukera kwa yeye kuongea au labda anaongea sana. sasa inafikia muda naye anajifunza kutoka kwako, mkikutana mna gumiana kama mabubu ,"mambo vipi?", "poa" kwisha mnakaa kimya.
Vijana kama marafiki au classmates, au school mate, mnapaswa kuchangamkiana na hiyo inaongeza/nogesha uhusiano miongoni mwenu au kati yenu. Hii inaanzia kwenye urafiki wa kawaida hadi kwenye ndoa na familia. Ukianza kuona wenzako wanaongea saaana, wakikaa kimya ,mtajikuta wote mnakuwa kimya halafu mnaanza ohoo home pana boa hakuna stori, kila mtu kanuna tuuu utadhani tumegombana.
Sisemi uongee saana ,hapana lakini salaam ndefu ni gesture nzuri kwa marafiki wenye mahusiano mazuri, inaonyesha kila mmoja ana mmiss mwenzie. Sasa ukimsalimia mwenzio "mambo vipi?", akajibu "poa" kasha wote mkakaa kimya ndio nini, unapo extend maongezi ni jamabo zuri kwamba mwenzio anaonyesha anao muda nawewe. sasa ukijidai una haraka wakati unaenda mjini kuzurura inakusaidia nini. Unataka uonekane wa maana wakati huna maana yoyote, ni upuuzi. Hata kwa mzazi, mdogo, kaka au dada, mke ,mume msalimie muongee kidogo mchekeshe mfurahiane sio muwe kama kondoo mtachukiana bure.
Kwa kifupi ongezeni nyama kwenye salamu, hata ukisalimia hadi paka wa jirani kwani kuna ubaya gani? mwenzi atacheka na kila akikuona au kukukumbuka ata cheka au kusmile hilo ndio jambo zuri. Acheni kujenga tamaduni mbaya, mara wasukuma mara sijui wagogo, kwani kuna asiyekuwa na kabila Tanzania hii? Tuwe vijana wachangamfu na kufurahishana kuanzia nyumbani hadi mtaani. trust me haya nayaandika hapa mnaweza kuya puuza ukiya practice utafurahi na kuwa mwenye furaha kila mahali.
Hutoogopa kukutana na watu, hutoogopa ku open conversation, hutoogopa kuonge na yeyote awe mkubwa au mdogo, maana kila mtu atakuwa amesha kufahamu hulka/aiba yako kwamba wewe ni mcheshi au mzungumzaji mzuri, na ni jambo zuri kuliko kuwa mkimya muda woote, hakuna mtu anataka kuwa na mtu mkimya muda wote. Muwe charming wote wavulana kwa wasichana, na hii huanzia kwenye salamu.