Operesheni ya kutokomeza majangili inavyotuangamiza, inavyotutesa. Hawa ni wakaazi wa Wilaya ya Singida waliochomewa nyumba kwa utekelezaji wa operesheni hiyo maeneo ya Mgori. Kwanini watu wanaitwa wavamizi wa maeneo waliyokaa tangu utoto wao miaka mingi? Tumekosea wapi kwanini serikali inatutesa? Hivi tukiangalia kati ya hawa kuna mtu hatari kwa wanyama hata digidigi? Kwanini wanaonufaika na Tembo ndio wanaoandaa mateso kwa wasio na mateso?.... Watetezi wa haki za binadamu, watetezi wa akina mama, watetezi wa watoto fikeni saidieni suala hili. Serikali ndio imewatendea hivi wakimbilie wapi?. Tuhamie wapi?