Ibrahim K. Chiki
JF-Expert Member
- Apr 5, 2011
- 594
- 163
Wadau, kiukweli inauma kuona tunaigawa tz yetu kichama. mimi ni mpinzani na nawakulabali sana chadema kwa sababu zangu binafsi na si tu kishabiki. kwa mfano, ilani na mikakati ya chadema inalenga kumkomboa mwananchi wa kawaida, ukilinganisha na ilani na mikakati ya ccm, inauma kuona wabunge wetu bungeni wakiendekeza uchama ndani ya bunge? wakipigia kura na kupitisha hoja ambazo kiukweli hazimlengi mtanzania wa kawaida..? hii inadhihirisha kwamba hata tukisema tupambambane kuleta mabadiliko kwa kuchagua rais kutoka upinzani itakua bado ni bure, la msingi hapa ni kupambambana na kuongeza idadi ya wabunge wa upinzani bungeni hata kufikia 70%, hapo tutaweza. Kaaa chini tafakari kwa umakini. nawakilisha.