broken ages
JF-Expert Member
- Mar 23, 2012
- 235
- 84
Nionavyo tunapaswa ama kuangalia upya sheria inayolinda maliasili zetu kama misitu na tunapaswa kuweka uzalendo sana ktk hili.kuna ukweli kwamba serikali ya Kenya imepiga maruku uvunaji wa aina yeyote ya miti katika nchi yake ama ndani ya aridhi yake lakini maruku hayo hayaandamani na uzuiaji wa matumizi ya mbao ama bidhaa za miti, na inavyosadikika ni kwamba kwa sasa Kenya inatgemea zaidi mazao ya miti ama mbao zaidi kuiport kutoka TANZANIA.je serikali ya Tanzania haioni hatari ktk hili? Kuna sababu gani ya kuweka usalama wa taifa kwenye mipaka iwapo bidhaa ama rasilimali za taifa kama hizi zinaweza kuwa zinapita tu na wala hao usalama wa taifa wasione ama wasichukue hatua ya kuishauri serikali kuzuia hili?ama Tanzania tuna misitu mingi zaidi kiasi kwamba hata ikivunwa na kusafirishwa nje haitakuwa na athari kwa nchi?ama kweli tunakuwa wavivu wa kutambua na hata vipofu wa kuona haya yote yanapotendeka? Maswali haya yote na mengi mengineyo nimekuwa najiuliza bila kupata jibu la kutuliza akili yangu mwanajf naomba tubadilishane mawazo ktk hili.