Watanzania msaada wenu, nasumbuliwa na kifua

Watanzania msaada wenu, nasumbuliwa na kifua

faru joni

JF-Expert Member
Joined
Dec 21, 2016
Posts
478
Reaction score
734
Ndugu wana jamiiforum, naombeni msaada wenu, nasumbuliwa sana na kifua.

Dalili ninazoziskia mpaka muda huu ni hizi hapa:
1. Kwanza nianze kusema sikohoi kabisa, nikimeza mate naskia mkwamo wa kitu kooni, ila nikimeza chakula naskia kawaida (kwenye kumeza chakula sisikii maumivu yeyote)

2. Kwenye upande wa kulia wa kifua (upande wa juu) kuna muda naskia maumivu ambayo yanashuka kwa chini kuna muda naskia normal (sisikii maumivu)

3. Sina mafua wala maumivu ya kichwa.

4. Hii hali ilinianza tangu mwezi wa 3 mwishoni (2020) nilienda hospita nikapewa dawa, dozi ya siku 10 nikatumia, baada ya siku 8 kumaliza dozi hali ikarudi upya ya kusikia mkwamo ninapomeza mate.

Maombni yangu kwenu:
Nimeskia kuna mchanyiko wa asali + limao na tangawizi je inaweza nisaidia? Kama mchanyiko uwo unaweza nisaidia je nauandaaje au naongezea na nini kingine?

Kama kuna njia nyingine ya kitabibu ya kuponyesha hii hali yangu naombeni mnisaidie ndugu zangu

Natanguliza shukrani na matarajio mazuri kwenye ili kutoka kwenu.

Mungu awabariki sana.
 
Si uende ukafanye endoscope ya koo I see, pengine uko na madonda kooni,
Je unavuta fag?
 
Nenda kamwone Daktari akupime akupe matibabu yanayostahili.
 
kunywa CIPRO

ukimaliza doz kaa sku mbil kunywa tena erthythromycin

kumbuka kula chakula kabla ya dawa na kunywa maji mengi kuokoa mzunguko wako wa damu! COVID inaua
thank me later
 
Pole sana mkuu na imani utapata ufumbuzi ngoja wajuzi waje.
 
kunywa habat souda au blackseed.inauzwa kwenye maduka ya dawa za asili
 
Mkuu pole sana Wakati wa Asubuhi kabla ya kula kitu tumia njia hii hapa. Chukuwa kipande cha Tangawizi isafishe kwa maji na usiimenye hiyo tangawizi iponde ponde iwe laini kisha weka katika sufuria kisha tia maji katika glasi moja na nusu kisha weka jikoni ipate kuchemka kwa dakika 10 moto wa kawaida.

Kisha weka katika kikombe dawa yote pamoja na Tangawizi kisha kamulia limao na kisha tia kijiko1 cha Asali Safi ya nyuki koroga vizuri kisha kunywa iwe ya moto na wakati wa mchana tengeneza tena dawa kama ulivo tengeneza asubuhi na unywe na kisha usiku tengeneza tena dawa mpya. tumia siku 3 au siku 5 au siku 7 utapona.
 
Back
Top Bottom