Ilianza na Abdurahman Babu, alipoonekana hataki muungano pamoja na mambo mengine, akapoozwa kwa kupewa uwaziri Bara. Hata Makamu wa kwanza wa mjomba hakuwa anapenda muungano, akapoozwa, sasa hivi swaaafi pamoja na wengine wengi mnao wajua! Jusa siyo tu kama ni mbaguzi, lakini anajua wazi akisimamia kauli yake sio tu kama atopewa uwaziri bara, pengine kwenye serikali ya umoja huko Zanzibar..(kama bado). Kwahiyo washajua dili, aliyepo kwenye kijinafasi japo tu cha uwakilishi, akisema na kukaza kuwa hataki muungano, fukuza hao wabara warudi kwako, basi Tanzania bara watatetemeka na kutafuta jinsi ya kumpoza huyo mtu kwa cheo au fedha....!
Lazima tufahamu kuwa Jusa pamoja na ubaguzi wake hayupo pekee, anao wananchi nyuma yake ambao wangependa wamsikie hivyo, kama anavyoonwa shujaa kwa kutamka wabara watoswe ajira visiwani HADHARANI, kama alivyompinga Tibaijuka katika mipaka. Hata katika baraza la wawakilishi Jusa aliposema wabara waniwe, nusu walimwunga mkono, na walio mpinga walieleza wasiwasi wao kuwa wazenji waliopo Bara nao watatoswa, lakini siyo kwa ajili ya sababu kuwa WABARA WASINYIMWE FURSA ZA AJIRA KWAKUWA Ni WENZETU.
Seriakali ya Jamuhuri, upande wa Bara, inatumia gharama kubwa kwa kile kinachoitwa kuudumisha muungano, ambao upande wa pili (zanzibar) hawautaki. Na kama wananchi wangekuwa wanautaka, hakika wangewakemea kina JUSA. Wazenji wengi wapo peponi huku, wakituuzia vimeo vya electoniki, wana mashamba na majumba, maduka ya jumla na rejareja, vibanda vya urojo na maziwa, mawaziri, polisi n.k lakini hali ni tofauti kwa wabara walioko zenji.
Hivi, nterest ya Tanzania Bara juu ya huu Muungano ni nini? Nini Watanzania tunafaidika na huu Muungano? Au pengine, faida yake ni vyeo vinavyozaliwa katika ishu ya kero na jinsi ya kuitatua? Hivi ni kweli kuwa wao wanalipa bei ya chini ya unit moja ya umeme na maji ukilinganisha na bara? Hivi ni kweli pass mark zao hupandiswa ili kupewa ufaulu katika usahihishaji wa mitihani ili amfikie mtanzania bara? Wapo kwenye bunge letu, lao wabunge wetu wapo? Jusa anataka rais ajaye wa Tanzania (Mwinyi aliwahi) atoke Zanzibar (bado haina shida hata wakija mia), lakini hatujamsikia anataka lini rais wa Zanzbar ajaye atokee Bara? Hivi, walivyochoma vibanda vya biashara vya wa bara walioko Zenji, hawajui kuwa ndugu zao wana vibanda vya kuchaji simu mitaani kwetu D'salaam? Tayari walishaunda katiba yao ambayo haiitambui katiba iliyopo, tena bila kuhusisha upande mwingine wa muungano, lakini hii ya huku inayofanyiwa marekebisho wao wametoa wajumbe 15, je marekebisho ya katiba hii itahusisha na marekebisho ya katiba mpya ya zanzibar? Kwasababu ili twende sawa lazima katiba zitambuane.
KWA KIFUPI, KAMA KUNA FAIDA ZOZOTE KWA TANZANIA BARA JUU YA HUU MUUNGAO, TUELIMISHWE ILI TUUPENDE NA KUUENZI. KAMATI YA JAJI WARIOBA WATUELIMISHE KATIBA MPYA YA ZANZIBAR ITAOANA VIPI NA KATIBA HII MPYA TUNAYOITEGEMEA, HASA KAMA KUNA HAJA YA KUWA NA MUUNGANO. Tanzania tumejitolea sana kwa ukombozi na uhuru wa nchi nyingi za Africa, ikiwapo Zanzibar, matokeo yake raia wetu wananyanyaswa katika nchi hizo, sasa basi inatosha kufanywa MAZUZU, ni wakati sasa wa kujijenga wenyewe na kuacha unafiki wa kuita hawa wenzetu, huku tukitambua fika kabisa wao hawatutambui sisi kama wenzao. Haya na kwa manufaa ya wajukuu wa wajukuu zetu tusio wafahamu.
Kibanga Msese
Lazima tufahamu kuwa Jusa pamoja na ubaguzi wake hayupo pekee, anao wananchi nyuma yake ambao wangependa wamsikie hivyo, kama anavyoonwa shujaa kwa kutamka wabara watoswe ajira visiwani HADHARANI, kama alivyompinga Tibaijuka katika mipaka. Hata katika baraza la wawakilishi Jusa aliposema wabara waniwe, nusu walimwunga mkono, na walio mpinga walieleza wasiwasi wao kuwa wazenji waliopo Bara nao watatoswa, lakini siyo kwa ajili ya sababu kuwa WABARA WASINYIMWE FURSA ZA AJIRA KWAKUWA Ni WENZETU.
Seriakali ya Jamuhuri, upande wa Bara, inatumia gharama kubwa kwa kile kinachoitwa kuudumisha muungano, ambao upande wa pili (zanzibar) hawautaki. Na kama wananchi wangekuwa wanautaka, hakika wangewakemea kina JUSA. Wazenji wengi wapo peponi huku, wakituuzia vimeo vya electoniki, wana mashamba na majumba, maduka ya jumla na rejareja, vibanda vya urojo na maziwa, mawaziri, polisi n.k lakini hali ni tofauti kwa wabara walioko zenji.
Hivi, nterest ya Tanzania Bara juu ya huu Muungano ni nini? Nini Watanzania tunafaidika na huu Muungano? Au pengine, faida yake ni vyeo vinavyozaliwa katika ishu ya kero na jinsi ya kuitatua? Hivi ni kweli kuwa wao wanalipa bei ya chini ya unit moja ya umeme na maji ukilinganisha na bara? Hivi ni kweli pass mark zao hupandiswa ili kupewa ufaulu katika usahihishaji wa mitihani ili amfikie mtanzania bara? Wapo kwenye bunge letu, lao wabunge wetu wapo? Jusa anataka rais ajaye wa Tanzania (Mwinyi aliwahi) atoke Zanzibar (bado haina shida hata wakija mia), lakini hatujamsikia anataka lini rais wa Zanzbar ajaye atokee Bara? Hivi, walivyochoma vibanda vya biashara vya wa bara walioko Zenji, hawajui kuwa ndugu zao wana vibanda vya kuchaji simu mitaani kwetu D'salaam? Tayari walishaunda katiba yao ambayo haiitambui katiba iliyopo, tena bila kuhusisha upande mwingine wa muungano, lakini hii ya huku inayofanyiwa marekebisho wao wametoa wajumbe 15, je marekebisho ya katiba hii itahusisha na marekebisho ya katiba mpya ya zanzibar? Kwasababu ili twende sawa lazima katiba zitambuane.
KWA KIFUPI, KAMA KUNA FAIDA ZOZOTE KWA TANZANIA BARA JUU YA HUU MUUNGAO, TUELIMISHWE ILI TUUPENDE NA KUUENZI. KAMATI YA JAJI WARIOBA WATUELIMISHE KATIBA MPYA YA ZANZIBAR ITAOANA VIPI NA KATIBA HII MPYA TUNAYOITEGEMEA, HASA KAMA KUNA HAJA YA KUWA NA MUUNGANO. Tanzania tumejitolea sana kwa ukombozi na uhuru wa nchi nyingi za Africa, ikiwapo Zanzibar, matokeo yake raia wetu wananyanyaswa katika nchi hizo, sasa basi inatosha kufanywa MAZUZU, ni wakati sasa wa kujijenga wenyewe na kuacha unafiki wa kuita hawa wenzetu, huku tukitambua fika kabisa wao hawatutambui sisi kama wenzao. Haya na kwa manufaa ya wajukuu wa wajukuu zetu tusio wafahamu.
Kibanga Msese