Watalii kushukia KIA ni tatizo

Watalii kushukia KIA ni tatizo

Rexwinton

Member
Joined
Mar 26, 2021
Posts
74
Reaction score
137
Toka mama arudi kutoka Royal Tour nasikia watalii wameongezeka sana cha ajabu wote wanashukia KIA na sio Dar ama Dodoma.

Sasa kwanini nasema wasishukie huko. Sababu ya kwanza ni unapunguza matumizi ta mtalii. Mtalii anatakiwa kushukia mbali na sehemu ya utalii ili aanze kutumia hela zake mapema kabla ya kufika eneo husika hii itasaidia kuongeza kipato.

Mfano akishukia Dar baadae atalazimika kupanda ndege nyingine mpaka KIA au eneo husika hii inaingiza faida.

Kuna wengine watapumzika kabla ya kuendelea na safari atatafuta hoteli yenye hadhi atalala atakula na kunywa atafanya starehe kabla ya kuendelea na safari yake hii itamfanya aanze kutumia pesa zake kabla ya kufika eneo husika la utalii hii inaongeza pato la kigeni nchini.

Pili inapunguza exposure kwa mtalii. Inapunguza uhitaji wa mtalii kutembelea maeneo mengine ambayo sio Arusha wala Moshi mfano mtalii anapoenda Ngorongoro anakosa hamu ya kutembelea sehemu nyingie za nchi mfano hifadhi ambazo zipo Kusini na Magharibi kama Ruaha na Gombe ambazo pengine asingeanzia Arusha angezitalii pia

Sababu ni nyingi ila za msingi ni kama hizo nilizoongea TUTAFAKARI.
 
Uzi wakijinga kabisa mwaka huu 2022. Hivi unajua hao watalii wame save mda gani mpaka kufunga safari kuja Tanzania?

Unafikiri wanakuwa hawajafanya 'research' mapema wakati wanapanga kutalii? Je unafikiri kampuni zinazowaleta nazo zitapata reviews positive ikiwa mtalii atajua alikuwa na uwezekanao wa kushukia KIA lakini ameshushwa JKNIA?

Usifikiri wazungu wanatumia hela hovyo hovyo tu. Mpaka anakuja TZ alisha budget kila cent atakayotumia na anahakikisha gharama zinaendana na uwezo wake na huduma anayopata.


Wewe uje umuongezee gharama za kipuuzi puuzi tu kama hiyo kampuni yako haijafa kibudu au nchi kukimbiwa na watalii.
 
Si kweli watalii kushukia KIA ni miaka mingi kabla hata swahili tour haijaanza ,kama mpandaji wa pipa kama KLM utaona robo tatu ya watalii wanaokwea KLM wote hushukia na kupandia KIA.
 
Toka mama arudi kutoka royal tour nasikia watalii wameongezeka sana cha ajabu wote wanashukia KIA na sio dar ama dodoma.
Sasa kwanini nasema wasishukie huko. Sababu ya kwanza ni unapunguza matumizi ta mtalii. Mtalii anatakiwa kushukia mbali na sehemu ya utalii ili aanze kutumia hela zake mapema kabla ya kufika eneo husika hii itasaidia kuongeza kipato. Mfano akishukia dar baadae atalazimika kupanda ndege nyingine mpaka KIA au eneo husika hii inaingiza faida. Kuna wengine watapumzika kabla ya kuendelea na safari atatafuta hoteli yenye hadhi atalala atakula na kunywa atafanya starehe kabla ya kuendelea na safari yake hii itamfanya aanze kutumia pesa zake kabla ya kufika eneo husika la utalii hii inaongeza pato la kigeni nchini.
Pili inapunguza exposure kwa mtalii. Inapunguza uhitaji wa mtalii kutembelea maeneo mengine amabayo sio arusha wala moshi mfano mtalii anapoenda ngorongoro anakosa hamu ya kutembelea sehemu nyingie za nchi mfano hifadhi amabazo zipo kusini na magharibi kama ruaha na gombe ambazo pengine asingeanzia arusha angezitalii pia
Sababu ni nyingi ila za msingi ni kama hizo nilizoongea TUTAFAKARI.

Dodoma kuna international airport? Na Dar es salaam kuna serengeti na Kilimanjaroro?
 
We unafikiri Watalii (Wazungu) ni Wandengereko Wenzako?.

Hao wanafanya hesabu tangu huko walipo, hivyo ukiwapa rout zako wasizozielewa wanaachana na wewe...huwezi kuwaambia wakashukie kilomita 1000 away kutoka sehemu wanayoikusudia...sasa kama umewaambia una uwezo wa kuwaleta Ngorongoro, Serengeti, Kilimanjaro na Tarangire wewe jichanganye kesho ukirudi usikie wote wamekuhepa wapo Kenya.
 
Sasa kwanini nasema wasishukie huko. Sababu ya kwanza ni unapunguza matumizi ta mtalii. Mtalii anatakiwa kushukia mbali na sehemu ya utalii ili aanze kutumia hela zake mapema kabla ya kufika eneo husika hii itasaidia kuongeza kipato. Mfano akishukia dar baadae atalazimika kupanda ndege nyingine mpaka KIA au eneo husika hii inaingiza faida.
Ndiyo mentality inayowakaanga waTanzania hivi sasa, miji yote wanapeleka stand za mabasi mbali kwa lengo la kuzifanya daladala, bajaj na bodaboda za wanasiasa na matajiri zifanye biashara bila kukumbuka kuwa wanawaongezea mzigo wa matumizi wananchi ambao kimsingi kipato chao ni duni na gharama za maisha zimewaelemea sana.
 
Utampangia ajee mtu sehem ya kushukia...we unafikiri mtalii anapo kuja tz hajui kuna sehem ina itwa dar..!? Wengi wanajua
Na wengi wanao shukia KIA wanakuja kwa specific purpose kupanda mlima Kilimanjaro au kwenda ngorongoro na n.k sio kufanya starehe au wewe unajua utalii ni starehe...!?
Mbona maeneo y starehe ya na juikana Zanzibar, visiwa vya cap Verde italy na Greece mkuuu tz hakuna seheme ya streeh tuna mfano wa sehem za streeh
 
Toka mama arudi kutoka royal tour nasikia watalii wameongezeka sana cha ajabu wote wanashukia KIA na sio dar ama dodoma.
Sasa kwanini nasema wasishukie huko. Sababu ya kwanza ni unapunguza matumizi ta mtalii. Mtalii anatakiwa kushukia mbali na sehemu ya utalii ili aanze kutumia hela zake mapema kabla ya kufika eneo husika hii itasaidia kuongeza kipato. Mfano akishukia dar baadae atalazimika kupanda ndege nyingine mpaka KIA au eneo husika hii inaingiza faida. Kuna wengine watapumzika kabla ya kuendelea na safari atatafuta hoteli yenye hadhi atalala atakula na kunywa atafanya starehe kabla ya kuendelea na safari yake hii itamfanya aanze kutumia pesa zake kabla ya kufika eneo husika la utalii hii inaongeza pato la kigeni nchini.
Pili inapunguza exposure kwa mtalii. Inapunguza uhitaji wa mtalii kutembelea maeneo mengine amabayo sio arusha wala moshi mfano mtalii anapoenda ngorongoro anakosa hamu ya kutembelea sehemu nyingie za nchi mfano hifadhi amabazo zipo kusini na magharibi kama ruaha na gombe ambazo pengine asingeanzia arusha angezitalii pia
Sababu ni nyingi ila za msingi ni kama hizo nilizoongea TUTAFAKARI.
Mtu anapotoka kwao anajua anapokwenda, na hapangiwi na mtu! Sema ufahamu wako kwa mambo ya kimataifa, usafiri na utalii, ni mdogo!
Unaposafiri unaangalia kwa mawakala mbalimbali, wanakupa options mbalimbali za usafiri! Kwa mfano, mtu anatoka USA, anaweza kuwa na ruti ya kupitia England, Qatar kisha Dar, kwa kutumia Qatar Air Ways, au Holland kisha KIA kwa KLM! Turkish Airways nao wana njia zao, Ethiopian au Kenya Air Ways! Wewe msafiri unaangalia gharama, layovers na kadhalika! Katika hayo yote, Samia na Royal Tour hawahusiki! Pia haiwezekani kumlazimisha mtu aende Dom au Dar, wakati yeye anataka kwenda Arusha!
 
Hahaha unafikiri mtalii na kama mbuzi tu unakokota wee unatkiwa kushukia Dar, Dom au Chato, hapana

Watalii wapo very specific na wanachotaka na huwezi mpangia, na akikosa anachotaka atachukua options nyingine!!

Mfano anataka kuona Wildebeest Migration na budget yake ni kiasi fulani kwa siku tatu au nne, akiona hiyo budget kwa tanzania haiwezekani ataenda kenya!!

Kwa hiyo lazima kuhakikisha Tanzania as destination inakuwa as much cheaper ili kuvutia watalii wengi iwezekanavyo!!
 
Back
Top Bottom