Watafuta kazi fursa hii hapa

Watafuta kazi fursa hii hapa

mmteule

JF-Expert Member
Joined
Oct 3, 2011
Posts
6,035
Reaction score
15,071
kwa taarifa za uhakika ambazo hazina chenga, ukweli ni kwamba kuna uhaba mkubwa wa madereva Serikalini. wengi wao wamekosa sifa za kuingilia ktk utumishi wa UMMA yaani kuwa na cheti cha kidato cha nne. kwa ushahidi ni kwamba kila wanapoitwa Interview wengi wao wanakutwa hawana vyeti vya sekondari hivyo wanarudishwa bila hata kufanya interview......kutokana na hali hii magari mengi ya serikali yanaendeshwa na deiwaka au mengine kuendeshwa na watumishi wasio madereva.....tatizo ni kubwa kuliko.
wakati wenzetu kule Nigeria wenye PHd wakiomba nafasi kama hizi hapa kwetu tunaziacha.....its vert rare Mtanzania mwenye kadegree kake aombe nafasi ya udereva kozi anajiona booonge la msomi.....
my take...anza na kidogo kikubwa kitafuata. anzen kuchangamkia nafasi za udereva hazina ushindani jamaniii. hata mbuyu ulianza kama mchicha
 
Bro umeona mbali sana!! thats true kuliko kukaa home ukashindwa tofautishwa na wasio na elimu ni bora ukakamata steringi usongeshe life,,
 
hiyo ndo ajira ya kweli. mimi nawajua jamaa zangu wanaendesha magari ya serikali wapo njema sana, ila graduate wa leo wataleta shobo.
ni bora graduate uwe dereva wa serikali na degree yako ya ualimu kuliko kupiga kazi robo siku huko CWT.
Njooni mambo iko huku
 
Ahsante mkuu kwa hiyo kama mimi(form 4) sijafanikiwa kuendelea na masomo ya juu
Ila nina cheti cha form 4 vp naweza nikapata nafasi?



mkuu utapata tuu, kinachotakiwa wewe nenda vyuo vinavyotambulika serikali ukasomee/ukajifunze udereva upate leseni halali.....itapendeza zaidi ukasoma NIT AU VETA KOKOTE ili cheti chako kiwe Lulu zaidi ndugu yangu. ukipata hivyo utapata ajira kiulaiiini sana. achana na mawazo mfu....madereva wanapiga pesa sana.
 
Ahsante mkuu kwa hiyo kama mimi(form 4) sijafanikiwa kuendelea na masomo ya juu
Ila nina cheti cha form 4 vp naweza nikapata nafasi?



mkuu utapata tuu, kinachotakiwa wewe nenda vyuo vinavyotambulika serikali ukasomee/ukajifunze udereva upate leseni halali.....itapendeza zaidi ukasoma NIT AU VETA KOKOTE ili cheti chako kiwe Lulu zaidi ndugu yangu. ukipata hivyo utapata ajira kiulaiiini sana. achana na mawazo mfu....madereva wanapiga pesa sana.

Ebana! Wewe umenena serikalini kuna uhaba wa madereva na hii inasababishwa na vigezo vinavyotumiwa kwamba atleast form IV, awe pia amepitia mafunzo ya udereva kwenye vyuo vinavyotambulika na serikali na awe na class c.Majanga ni hapo kwenye form IV madereva wengi "kitaa" huwa ni chini ya form IV.Kama wewe hupendezwi na wazo hili waachie wenye shida hulazimishwi nenda kawe mjasiriamali,meneja n.k huwa ndiyo mgawanyiko waache wenye shida wakomae usiwakatishe tamaa.
 
Akili yako ni nzuri, ila naamini Magari ya Serikali ni Macheche kuliko idadi ya wafanyakazi hivyo kwa kusema kwako kuwa ni afadhali watu waombe udereva kuliko kazi zao za kitaaluma siamini kama umefikiria mbali. Na sio vizuri kuwakatisha watu tamaa ili waache kusomea taaluma zao na kuona afadhari udereva maana ndio unaajira za haraka. Je wewe ni Dereva na kama ni kweli ni graduate wa kozi gani?
 
Akili yako ni nzuri, ila naamini Magari ya Serikali ni Macheche kuliko idadi ya wafanyakazi hivyo kwa kusema kwako kuwa ni afadhali watu waombe udereva kuliko kazi zao za kitaaluma siamini kama umefikiria mbali. Na sio vizuri kuwakatisha watu tamaa ili waache kusomea taaluma zao na kuona afadhari udereva maana ndio unaajira za haraka. Je wewe ni Dereva na kama ni kweli ni graduate wa kozi gani?

Mkuu hapo Red Hujamuelewa mleta maada
Yeye kasema kwa waliograduate ila hawana ajira
Ni bora mda huo wakautumia kuomba nafasi ktk udereva huku wakiendelea kutafuta nafasi nzuri zaidi sawa na taaluma zao!
Pamoja mkuu!
 
Umeongea ukweli tupu wabongo tusichague kazi kama bado haujapata anza kidogo kidogo huku ukiangaika na nyingine ni rahisi sana kupata kazi ukiwa na kazi.....anza na kidogo!! Its a real talk...
 
Mada kama hizi zinafaa sana katika kuleta tija kwa wanajamvi. Ni vizuri kuanza na ajira hata kama ipo chini ya qualifications zako, baadae utapata ya qualifications zako
 
Mie tayari ni dereva mkuu katika shirika moja la kigeni na ni graduate...kiukweli niko safi..end of month navuta take home 1.5 hapo bado nikisafiri navuta 80 elfu per day na mazaga kibao...nshamaliza mjengo wangu pande za salasala, mkoko upo wife yeye anasukuma mzigo nae basi maisha swaafi...wenzangu walionicheka sasa hata kunisabahi wanaogopa!
 
Back
Top Bottom