Watafuta ajira tuache kujimwambafai

Watafuta ajira tuache kujimwambafai

donocean

Member
Joined
Jan 10, 2019
Posts
72
Reaction score
46
Habarini wana wa jukwaa hili,

Tatizo la ajira ni kubwa mno hapa nchini kwa sasa, ambapo watu wengi wamekuwa wakitamani kufanya kazi serikalini wakiamini ndiyo kwenye unafuu na mapumziko ya kutisha.

Lakini kwa mtazamo wangu, siyo mkubwa sana ukilinganisha na nchi za wenzetu kama Marekani na nchi nyingine zilizoendelea ambapo mtu kupata ajira angalau serikalini inakubidi uwe na kipaji cha ajabu sana.

Wasomi wengi wa Tanzania wamekuwa wakichagua sana kazi. Kwa mfano, kwenye nchi za wenzetu unakuta mtu anafanya kazi za ndani huku ana Master's au hata kufanya kazi bar huku ana degree nzuri tu.

Mtu unaitwa ukafanye kazi ya kutafuta wateja au customer care, au call center lakini unakataa kwa kigezo cha elimu uliyo nayo.

Kampuni nyingi za kizungu ukipeleka CV watakuambia una experience? Na experience wanazotaka kuziona ni kama umewahi kuuza hata duka la mtu au kama umewahi kufanya kazi bar wanataka ionekane kwenye CV.

Kwa hiyo Watanzania tuache kuchagua kazi kwa kigezo cha elimu. Kama una shahada unaweza kufanya hata kazi ya kuuza duka, kuhudumia mgahawa, kukaa counter na nyingine nyingi tu zinazofanana na hizo.

Mim pia ni mhanga wa ajira ila sichagui kazi yoyote itakayokuja mbele yangu poa tu, na nina Shahada ya Kwanza ya Uchumi na Maendeleo ya Jamii.

Tusichague kazi hata kama una PHD, unless soko liwe upande wako.
 
Mawazo kama haya nayasikia hata kwa viongozi kadhaa na baadhi wenye ajira, sasa watu wanasoma Chuo ili iweje kama hawawezi kuja kutumika katika nafasi ambazo wana ujuzi nazo? mawazo kama haya yanapelekea kukatisha tamaa ambao wapo ngazi za chini za kielimu.

Ni sahihi kabisa kama mtu atatafuta ajira isiyo ya taaluma yake kama tu itakuwa ajira ya ziada kwa ajili ya kuongeza kipato, huko kwa wenzetu hizo ajira unazozisema wanazifanya watu wenye elimu za kawaida tu na kama ajira za ziada. Mtafuta ajira anayo haki ya kuchagua kazi kwasababu sio kila kazi ana ujuzi nayo, na anayo sababu ya kutafuta kazi ya ujuzi wake ili awe na tija zaidi kwa mwajiri wake.

Tofauti na hapo hizi stori za kazi yeyote tunakubali kama taifa tumeshindwa kukuna vichwa jinsi ya kuwatafutia watu wetu ajira kulingana na taaluma zao ili wawe na tija kwa taifa, Swali la kujiuliza kwanini mtu Asome uhasibu, udaktari, Uhandisi, Uanasheria halafu badala ya kuutumia ujuzi wake awe muuza chipsi? Kwa nini Chipsi zisiuzwe na waliosomea Nutrition na mambo ya Chakula? Moja ya jawabu Taifa letu hatuheshimu Ujuzi ndo maana kuna vitu tunavichukulia poa tukiamini havihitaji Elimu lakini si kweli, Wenzetu Salon zinasomewa kabisa, upishi ndio usiseme
 
major mwendwa, Fact, huwez somea ubwana shamba eti ukauze lambalamba hiyo elimu ya ubwana shamba itakuwa imo kweli ? Mwenyewe ni mhanga wa ajira lkn mpaka najilaumu Kwa nn nisingeishia tu form four maana leo naona niliomaliza nao form four wanamaendeleo kupita mm na wengine wananidharau nakuniambia ulisoma nn sasa ona unaanza mwanzo sisi tulishakupta sana
 
Pia hata hizo ajira za kuuza bar na duka, angalau basi kungekua kuna makubaliano yanayotekelezeka, siyo mtu unafanyishwa kazi kama punda, halafu hata malipo yenyewe kuyapata bado uzungushwe tena. Hizo nchi za watu unazosema watu wanaheshimu jasho la mtu, utafanya kazi na kulipwa kulingana na makubaliano, hii kwa Bongo bado sana.
 
Fact, huwez somea ubwana shamba eti ukauze lambalamba hiyo elimu ya ubwana shamba itakuwa imo kweli ? Mwenyewe ni mhanga wa ajira lkn mpaka najilaumu Kwa nn nisingeishia tu form four maana leo naona niliomaliza nao form four wanamaendeleo kupita mm na wengine wananidharau nakuniambia ulisoma nn sasa ona unaanza mwanzo sisi tulishakupta sana
Wahenga walisema, "kusoma sio kazi, kazi kupata kazi".
 
Tatizo unatoa mifano ya ardhi na mbingu ni vitu tofauti. Huku nchi za mtu mweusi kuna kazi hazina maadili na unafanya kazi masaa mengi, full time job na malipo kiduchu.
Na degree yako mtu ukashikwe makalio bar huko si bora ukae njaa. Mshahara wa elfu 70 au 60.

Ngoja kwanza ustaarab uuingie watu wanaweza fanya hizo kazi la sivyo bado sana.
 
major mwendwa, Huwa naangalia mawazo ya watanzania wengi kuhusu tatizo la ajira nikaja kugundua watanzania wengi ni fuata upepo na jambo hili co tu kwa watanzania ambao elimu yao ni ndogo hapana, mpk walioenda shule wengi wao majibu yao ni yale yale ya kimihemko na ya kusikiasikia, hata mtoa uzi nae ameenda kwny mkumbo ule ule, imefika kipindi elimu imeanza kuonekana c kitu eti kwasabu ya tatizo la ajira, vijana hawataki kusoma kwasabu ya kuharibiwa kisaikolojia na wapumbavu wachache wanaoongea maneno ya kusikia sikia, mkuu major mwendwa umeongea vitu konki sn na huu ndio ukweli, tuache kupotosha elimu ibaki kuwa elimu cz hakuna taifa likaendelea pasipo kutia mkazo ktk elimu, hili tatizo la ukosefu wa ajira lisichanganywe na elimu kwakuwa tatizo la ajira ni changamoto hata kwa wasioenda shule, cha msingi ni kufanya midahalo yenye tija km taifa tujue tuna lisovu vp tatizo hili na co kujibu kwa hoja nyepesi nyepesi km hoja aliyoleta mtoa mada.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwanza mda mwingine wanatafuta kazi kupitia hata kwa marafiki lakini kinachotushinda hata kuwaunganisha na hizo kazi ni tabia zao za kiundashi wa sms.

(Oya bro nifanyie manuva ya kijobu ili nami nitusue kama vipi) anaekwandikia sms ya hivyo ni dogo saizi ya mwanao na ana degree kweli kwa sms hiyo mie nikujibu
 
  • Thanks
Reactions: THT
Mawazo kama haya nayasikia hata kwa viongozi kadhaa na baadhi wenye ajira, sasa watu wanasoma Chuo ili iweje kama hawawezi kuja kutumika katika nafasi ambazo wana ujuzi nazo? mawazo kama haya yanapelekea kukatisha tamaa ambao wapo ngazi za chini za kielimu.

Ni sahihi kabisa kama mtu atatafuta ajira isiyo ya taaluma yake kama tu itakuwa ajira ya ziada kwa ajili ya kuongeza kipato, huko kwa wenzetu hizo ajira unazozisema wanazifanya watu wenye elimu za kawaida tu na kama ajira za ziada. Mtafuta ajira anayo haki ya kuchagua kazi kwasababu sio kila kazi ana ujuzi nayo, na anayo sababu ya kutafuta kazi ya ujuzi wake ili awe na tija zaidi kwa mwajiri wake.

Tofauti na hapo hizi stori za kazi yeyote tunakubali kama taifa tumeshindwa kukuna vichwa jinsi ya kuwatafutia watu wetu ajira kulingana na taaluma zao ili wawe na tija kwa taifa, Swali la kujiuliza kwanini mtu Asome uhasibu, udaktari, Uhandisi, Uanasheria halafu badala ya kuutumia ujuzi wake awe muuza chipsi? Kwa nini Chipsi zisiuzwe na waliosomea Nutrition na mambo ya Chakula? Moja ya jawabu Taifa letu hatuheshimu Ujuzi ndo maana kuna vitu tunavichukulia poa tukiamini havihitaji Elimu lakini si kweli, Wenzetu Salon zinasomewa kabisa, upishi ndio usiseme
Umechangia vyema ,sijajua kama JF kuna watu wenye akili kubwa kama ww!

Wengi hawachagui ajira ila wanataka ajira inayoendana na field yake,kama umeomea uhasibu unaweza uza duka sio mbaya,kama una mechanical au engineer raha yake ni kuona Mashine zipo karibu pale zinaongeza kitu kidogo na kuweza Ku activate ile sehemu ya ubogo inayohusika na ubunife.
Nutrition akiuza misosi poa sana.
 
major mwendwa, Fact, huwez somea ubwana shamba eti ukauze lambalamba hiyo elimu ya ubwana shamba itakuwa imo kweli ? Mwenyewe ni mhanga wa ajira lkn mpaka najilaumu Kwa nn nisingeishia tu form four maana leo naona niliomaliza nao form four wanamaendeleo kupita mm na wengine wananidharau nakuniambia ulisoma nn sasa ona unaanza mwanzo sisi tulishakupta sana
Mkuu nikuhakikishie haupo wewe pekee katika kundi hili ni wengi, hii hali inatokea sababu wenye dhamana ya kufanya maamuzi ya uelekeo wa Taifa letu wengi hawaguswi na haya ambayo wengi yanawaumiza, tunazungumzia viongozi ambao wao wanapokea mishahara ya kutosha, wanapeana marupurupu na pensheni zilizonona, Watoto wao wanasoma shule nzuri na vyuo bora kabisa wanawahakikishia nafasi za ajira kwenye mashirika ya umma au makampuni makubwa ambayo wana ushawishi, Mwenye shibe hamjui mwenye njaa, lakini laiti hili swala lingekuwa linatukumba wote hakika hali isingekuwa hivi. Nikupe mfano tuna uhitaji mkubwa sana wa Madaktari, Wahandisi, Walimu, Manesi, Wanasheria, Wahasibu kila aina ya wataalamu serikali ina mapungufu, Serikali haitaki kuajiri sababu haina mishahara ya kuwalipa, Mwalimu Mmoja Mshahara wake ni kuanzia laki 7, Mhandisi laki 9, Daktari 1.4m Lakini Tuna wabunge Zaidi ya 350, Mbunge Mmoja Mshahara na Marupupu yake anapokea takribani 11m, Hivi tungeshusha hayo marupupu hata mpaka 5m Tungeajiri wataalamu wangapi? Mbunge anakiinua Mgongo cha zaidi ya milioni 350 kwa kufanya kazi ya kuwakilisha wananchi kwa Miaka 5 tu, Mwalimu aliyedumu katika utumishi kwa zaidi ya Miaka 35 hawezi kufikisha Pensheni ya Milion 200,
Hapo ndipo ilipo shida sijaongelea changamoto ya mfumo wetu wa Elimu
 
Back
Top Bottom