major mwendwa, Huwa naangalia mawazo ya watanzania wengi kuhusu tatizo la ajira nikaja kugundua watanzania wengi ni fuata upepo na jambo hili co tu kwa watanzania ambao elimu yao ni ndogo hapana, mpk walioenda shule wengi wao majibu yao ni yale yale ya kimihemko na ya kusikiasikia, hata mtoa uzi nae ameenda kwny mkumbo ule ule, imefika kipindi elimu imeanza kuonekana c kitu eti kwasabu ya tatizo la ajira, vijana hawataki kusoma kwasabu ya kuharibiwa kisaikolojia na wapumbavu wachache wanaoongea maneno ya kusikia sikia, mkuu
major mwendwa umeongea vitu konki sn na huu ndio ukweli, tuache kupotosha elimu ibaki kuwa elimu cz hakuna taifa likaendelea pasipo kutia mkazo ktk elimu, hili tatizo la ukosefu wa ajira lisichanganywe na elimu kwakuwa tatizo la ajira ni changamoto hata kwa wasioenda shule, cha msingi ni kufanya midahalo yenye tija km taifa tujue tuna lisovu vp tatizo hili na co kujibu kwa hoja nyepesi nyepesi km hoja aliyoleta mtoa mada.
Sent using
Jamii Forums mobile app