pmwasyoke
Platinum Member
- May 27, 2010
- 4,982
- 3,787
Naomba wastaafu na wastaafu watarajiwa tuutumie uzi huu kushauriana mambo kadhaa yahusuyo masilahi ya wazee kama:
(a) Jinsi ya kupitisha muda - maana masaa 24 kwa siku ni mengi. Tatizo hili ni hasa kwa wale ambao shughuli walizojiandalia kujikimu zinajiendesha bila kuhitaji muda wao mwingi;
(b) kwa wastaafu ambao kujikimu ni shida kutokana na maandalizi hafifu au kipato kidogo wakati wa ajira - mawazo kuhusu shughuli za kujipatia/kujiongezea kipato japo kidogo - kwa waajiriwa wajue kwamba kwa walio wengi mifuko ya hifadhi ya jamii hutoa kipato duni mno;
(c) Matibabu, bima za afya zihudumiazo wazee;
(d) Mbinu mbalimbali za kuongeza ubora wa maisha ya uzeeni;
(e) Kwa wasioifikia hatua hiyo, mbinu za kujiandaa ili kuongeza ubora wa maisha uzeeni;
(f) n.k.
Hili linatuhusu wote kwani hata ukiwa na umri wa miaka 30 au pungufu utafika huko.
Karibuni.
(a) Jinsi ya kupitisha muda - maana masaa 24 kwa siku ni mengi. Tatizo hili ni hasa kwa wale ambao shughuli walizojiandalia kujikimu zinajiendesha bila kuhitaji muda wao mwingi;
(b) kwa wastaafu ambao kujikimu ni shida kutokana na maandalizi hafifu au kipato kidogo wakati wa ajira - mawazo kuhusu shughuli za kujipatia/kujiongezea kipato japo kidogo - kwa waajiriwa wajue kwamba kwa walio wengi mifuko ya hifadhi ya jamii hutoa kipato duni mno;
(c) Matibabu, bima za afya zihudumiazo wazee;
(d) Mbinu mbalimbali za kuongeza ubora wa maisha ya uzeeni;
(e) Kwa wasioifikia hatua hiyo, mbinu za kujiandaa ili kuongeza ubora wa maisha uzeeni;
(f) n.k.
Hili linatuhusu wote kwani hata ukiwa na umri wa miaka 30 au pungufu utafika huko.
Karibuni.