Arthurtz
Senior Member
- Feb 10, 2017
- 151
- 121
Tanzania tumejaaliwa na vijana wengi sana ambao ndio chachu ya mendeleo na mabadiliko chanya kwa Taifa letu. Bila kusahau tuna Vyuo Vikuu na Taasisi 64 zinazotoa elimu juu (Kuanzia Certificate, Degree na hadi Masters). Dar es salaam tu kuna Vyuo Vikuu na Taasisi 22 za elimu ya juu hivyo tuna maelfu ya Vijana wenye ujuzi na taaluma za kutatua changamoto za jamii zetu kama wakiwa na ushirikiano na wakipewa nafasi.
Leo hii ningependa tujadili na kuchangua swala moja. Wewe kama Mwana JF, Mwananchi mzalendo, Mpenda maendeleo na Mlipa Kodi wa Taifa, Unadhani ni jambo gani vijana wetu wasomi wa Vyuo Vikuu kwa umoja wao wanatakiwa kuungana na kulifanya ili kuleta Mabadiliko chanya na Maendeleo kwa jamii yetu.
Tafadhali tunaomba uchangia fursa, idea, kero au wazo lolote ambalo ungependa wasomi wetu walifanyie kwa pamoja kwa manufaa ya jamii.
Angalizo, Tungependa lisihusishe Dini au Siasa.
Sent using Jamii Forums mobile app
Leo hii ningependa tujadili na kuchangua swala moja. Wewe kama Mwana JF, Mwananchi mzalendo, Mpenda maendeleo na Mlipa Kodi wa Taifa, Unadhani ni jambo gani vijana wetu wasomi wa Vyuo Vikuu kwa umoja wao wanatakiwa kuungana na kulifanya ili kuleta Mabadiliko chanya na Maendeleo kwa jamii yetu.
Tafadhali tunaomba uchangia fursa, idea, kero au wazo lolote ambalo ungependa wasomi wetu walifanyie kwa pamoja kwa manufaa ya jamii.
Angalizo, Tungependa lisihusishe Dini au Siasa.
Sent using Jamii Forums mobile app
