PreGE2025 Wasira: Tutapendekeza wagombea wanaokubalika na wananchi

PreGE2025 Wasira: Tutapendekeza wagombea wanaokubalika na wananchi

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

DuaZaMama

JF-Expert Member
Joined
Jun 2, 2025
Posts
1,882
Reaction score
4,129
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Stephen Wasira, amesema wagombea wakiwamo wabunge wanaomaliza muda wao watakaochukua fomu Julai 2, 2025 na kuzirudisha, baada ya vikao vya chama hicho, watatazamwa na kupendekezwa wagombea wanaokubalika na wananchi

Amesema baada ya Rais Samia Suluhu Hassan, kuvunja bunge Juni 27, mwaka huu, kazi iliyobaki kwa chama hicho, itakuwa ni kuendesha taratibu za kupata wagombea na kusisitiza haitakata mtu bali itateua.

Wasira ameyasema hayo leo, alipokuwa akizungumza katika mkutano wa hadhara na wananchi wa wilaya ya Sengerema, mkoani Mwanza, wakati akihitimisha ziara yake katika mkoa huo.

Amesema wagombee ni wengi lakini watachuja na wala hawatakata mtu bali watateuwa: "Kukata ni kwa hasira, ukiteua unatazama uwezo kwa wakati. Kwa hiyo CCM hatukati mtu, ila tunateua wagombea wachache kati ya wanachama wengi.

"Maana tunawanachama wengi, hivyo watakaobaki watasubiri uchaguzi ujao maana vijana wako wengi," amesema Wasira.
1750851992239.png
 
kwani wewe na mama Abdul mnakubalika na wananchi au polisi ? tuache kutumia neno nakubalika vibaya haiwezekani hata vitu vya msingi sisi tunafanya maigizo kama mnazingatia wanao kubalika wekeni tume huru.
 
Am 80 yrs am requesting the employment opportunity at your institution...✍️✍️
 
Back
Top Bottom