Hapa Bunda shamrashamra tu asilimia zaidi ya 90 ya watu niliozungumza nao wanasema sasa ni wakati wa mabadiliko, sasa ni Chadema. Akimnadi mgombea wa udiwani Bw Julius Wasira juzi, kada wa Chadema Lilian Wasira alisema hakuna wa kuizuia Chadema katika uchaguzi huu au chaguzi zijazo. Alisema hakuna kitu CCM imeshindwa kufanya kwa miaka 53 itaweza kufanya kwa miaka michache ijayo. Ni Chadema pekee inaweza kuleta ukombozi, alisema. Nae mgombea alisema wampe fursa ya kuongoza na atawawakilisha vema katika kulinda mapato ya halmashauri.