Fidel80
JF-Expert Member
- May 3, 2008
- 21,947
- 4,445
Lawama ya kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa Yanga kwenye hatua ya nusu fainali ya michuano ya Tusker, imemuangukia beki huyo ambaye anashutumiwa kuwa ni kawaida yake.
Habari za uhakika kutoka ndani ya Simba zimeeleza tayari kumekuwa na kikao kilichowakutanisha viongozi kuwajadili wachezaji kadhaa wenye mwelekeo wa kuiumiza Simba na Yondani ameonekana ana makosa mengi zaidi.
Mmoja wa viongozi walioingia katika mkutano huo uliofanyika siku mbili baada ya Simba kulala kwa Yanga. Amesema Yondani hatadumu katika klabu hiyo.
Sipendi kutajwa gazetini, lakini hili utaliona tu. Unajua imekuwa ni kawaida, kila unapofika mchezo wa Yanga kuna wachezaji ambao lazima wabembelezwe kuwa wawe makini wasitufungishe.
Lakini kama hiyo haitoshi hao hao ndiyo wamekuwa wakitufungisha, angalia Yondani mechi hii amefanya uzembe, mpira ulikuwa wake. Kaenda kucheza rafu makusudi halafu kajiangusha. Hata hakuamka badala yake alikuwa anamuangalia Ngassa anaenda kufunga huku akisingizia misuli.
Kama una kumbukumbu alifanya hivyo mechi nyingine dhidi ya Yanga kumauchia Baraza apige krosi. Sisi tunaelewa tatizo ni nini na hata kocha pia ameliona hilo, ile si hali ya kawaida, alisema kiongozi huyo akionyesha kukerwa na namna alivyofanya Yondani.
Dakika za mwisho kabisa za muda wa nyongeza wa dakika 30, Yondani alienda kurukia mpira uliokuwa unaonekana hauna madhara yoyote dhidi ya Ngassa.
Ajabu alitaka kumrukia Ngassa ambaye alimkwepa na kuchukua mpira kasi, wakati anaondoka, Yondani alianguka na kulala kabisa. Ngassa alitoa krosi safi kwa Shamte Ally aliyeimaliza Simba akafunga kirahisi
Tunawasubili Mapinduzi Cup sijui nako mtakuja na lawama gani.