Warioba Anataka Nini Hasa?


serikali tatu
 
Warioba alikuwa Mwenyekiti wa Tume na hivyo msemaji. Hata hivyo, maoni yaliyotolewa hayakuwa ya kwake peke yake. Hivyo siyo busara hata kidogo kumshambulia yeye kama mtu binafsi.
Busara ni kujadili hoja na kufanya marekebisho panapostahili. Tunapoteza muda mwingi na rasirimali kujadili mtu badala ya hoja
 
Samahan Mtoa mada sio Kijana!!
pls edit ur commmt
Asante kwa kunijulisha kuwa mtoa mada siyo kijana. Ila ukimlinganisha na Mzee warioba kiumri yeye ni kijana mdogo sana na yeye na wenye umri kama wake au umri mdgo zaidi watakuwa ni watovu wa nidhamu kama wataendelea kumtupia maneno ya kashfa mzee wetu huyu kwa kisingizio cha kumuenzi Baba wa Taifa..
 
- Sijakuelewa mkuu sana eti tatizo lipo wapi na hayo maneno ya English? hebu fafanua kidogo?

Le Mutuz System


rekebisha sarufi mkuu hivi tunatumia comparison bila neno than? " A BIGGER PICTURE BEHIND ALL THESE!!" pia epuka direct translation from Kiswahili to English,vinginevyo tumia tu Kiswahili tutakuelewa vizuri tu mkuu (mwaha) valamse:smile-big:
 

https://www.jamiiforums.com/katiba-...e-azungumza-kuhusu-tanganyika-na-nyerere.html
 
Hiyo yako ndiyo sera ya ccm tumezoea kuisikia, maelezo hafifu kweli lakini wanayaenzi sana. Hujawa mwanaccm hai mpaka utamke neon baya juu ya Warioba. Mzee wa watu kafanya kazi yake na sasa katunukiwa na tuzo ya muungano, huyo nJK anawafanyia usanii ccm lakini ao hawaoni wala kusikia, amemkubali Warioba ile mbaya na hata serikali tatu anazitaka lakini kwa uwa kazisoma bongo za wccm upororo sana anawaambia maneno wanayotaka kuyasikia lakini pembeni anasema ukweli wake kwamba wananchi wataamua, yeye akiwa mmojawao.

Leteni hiyo katiba ya ccm mtajiju, ombwe la nini?
 
Hoja ipi au swali lipi la warioba linatafuta majibu mbona maswali yake yote yanamajibu ya kiasili na mengine yote yamejibiwa bungeni unakurupuka bila hata kujua unaongea nini.
kumbe wewe hujatulia, unahitaji kupepewa
 
Subirini nirudi ngoja nkatipike siasa ya bongo kichefchef hamna jipya
 
Hoja ipi au swali lipi la warioba linatafuta majibu mbona maswali yake yote yanamajibu ya kiasili na mengine yote yamejibiwa bungeni unakurupuka bila hata kujua unaongea nini.

acha umbwiga weyee mama... usikurupuke tu kama umefumaniwa.. chukua hiyo rasimu ya rais kikwete afu isome vizuri ndo utajua kwanini imependekeza serikali tatu. utambue kuwa hiyo rasimu si ya warioba ni ya mzee wa kaya. jaji warioba yeye ni mtumishi tu alitumwa na mzee wa kaya afanye kazi na kazi ndo hiyo aliyoipitisha mzee wa kaya ili wabunge.. SORRY.. wajumbe waijadili yaliyomo na kuipitisha.
 
Tofautisha uwelewa wa mzee wako na mzee warioba then utapata jibu lakn jilinganishe ww na hampery polepole... utaona tofauti ya ujana wako..
 
Ndiyo maana hata serikali ilimshinda wakati akiwa waziri mkuu mpaka akajiudhuru wadhifa wake ni miongoni mwa watu wa hovyo kabisa wanaopenda kulazimisha mambo hata kama hayana maana yapite.

Mkuu sasa ndio amekuwa mtu hovyo? Nadhani rais na chama chenu cha CCM mlimteua kuwa mwenyekiti wa tume kwa kumuona ana uwezo na weledi wa kuifanya kazi ya kukusanya maoni ya wananchi nadhani shida imeanzia pale alipotimiza uadilifu wa kazi yake kwa kutokariri ngonjera za chama na kusimamia matakwa ya wananchi ndio maana mafisadi mnalia mlitarajia awe mr. yes mzee imekula kwenu.
 
Nafikiri huna hata redio chumban kwako na unachofanya kwa sasa ni kutafuta cha kuongea! Kama unaipenda nchi basi ongea interahamwe waache upuuzi na kama kweli wewe una data basi mjibu warioba(Father of Tanganyika) maswali yote aliyouliza interahamwe na wafuasi wao kama wewe
 
Bwana Malecela, hivi wewe ulitaka iweje baada ya Tume ya Warioba kuwasilisha ripoti yake?Ulifikiri kwa akili zenu za ki-CCM baada ya kuivunjilia mbali Tume hiyo mlitaka Jaji Warioba awe BUBU!!?? Kwamba asijibu wala kuongea chochote kwa vile Tume haipo???Yaani mlitaka Jaji Warioba na kwa heshima aliyo nayo na kazi nzuri alofanya akae kimya tu kisa Serikali ya CCM mmeamua kuvunja Tume???Mkakati wenu umebuma!

Mzee wa watu, Jaji Joseph Sinde Warioba wala hataki maneno. Anachotaka ni RASIMU No.-2 aliyoiwasilisha kwa Marais wote wawili wa Tanganyika na Zanzibar na ndani ya BMK ndiyo ijadiliwe. Kwamba maoni ya Wananchi yaliyomo kwenye Rasimu No.2 ya Katiba mpya yajadiliwe kwa kina kama yalivo na kufanyiwa maboresho pale tu panapo onekana pana mapungufu.

Lakini pia Mzee wa Watu Jaji Warioba anataka ajibiwe yale maswali yake 7 aliyowauliza Viongozi wa CCM na Wapambe wao.Hamuwezi kumzuia Jaji Warioba asizungumze na media ili kufafanua yale ambayo CCM wanajaribu kuyapindisha na kuyapotosha kwa manufaa yao. Yeye kama Mwenyekiti wa Tume iliyosimamia mchakato huu, hawezi kukaa kimya anapoona anatukanwa matusi ya nguoni na kukashifiwa tena na Wana-CCM wenyewe! Hakuna mtu anaweza kukubaliana au kuvumilia upuuzi huu unaofanywa na Serikali ya CCM! Never.
 

Huyu Bwana katoa post nzuri sana tena yenye hoja zenye mashiko, Wewe kwa sababu ya upofu wako na uwezo wako mdogo wa kuchambua hoja critically ndiyo maana umeishia kubeza tu. Hujahenga hoja yoyote kuonesha kuwa amepwaya wapi badala yake unamuongelea Mzee Malecela kaba kwamba kuna ubishi juu ya wazee hawa waili Waryoba na Malecela. Kama Elimu zebu ni ndogo kwa sababu ya kuogopa umande na kuoenda viporo vya wali nyumbani enzi ya utotoni, badi waacheni waliobobea ktk hoja.
 
Siyo wewe peke yako Ndugu yangu. Hata Mimi namshangaa Ana lengo gani huyu. Akae pembeni. Anabowa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…