Waraka Wa Jaji Warioba kwa Wassira

frema120

JF-Expert Member
Joined
Jan 1, 2012
Posts
5,098
Reaction score
1,341
Jana nilipata kusikia kuwa jaji warioba kaandika waraka mzito kwa mh. wassira juu ya anachokifanya sasa kupotosha rasmi ya katiba na mambo mengi juu ya ubaya wa wasira na misimamo yake sasa.

Na kikubwa kuelezea alivyomfanya kukimbia/kufukuzwa CCM na kuelekea NCCR. pls mwenye nao hatuweke hapa tusome.



Chanzo: Mwananchi
 
huo waraka akiandika Warioba nitaona uzee umemfika kiwango cha juu sasa na ni utoto.
 
Nilikuwa najiuliza kwanini Makamba na Wassira ni watu wa karibu? Sasa nimepata jibu, hawa wote wako tayari kukupakazia lolote ailimuradi ana survive ktk siasa maslahi....JK akamtosa Makqmba kwa shinikizo la wenye CCM ila huyu amemganda kama ruba.....lakini ni suala la wasaa tu naye ataondoka naye ktk siasa za nchi hii, nashangaa Bulaya leo kuitwa msagaji eti kwa sababu anatishia ustawi wa Wasssira pale Bunda! Makamba , Wasira, Makinda waliwatumia Kombani na Mkulo huku Aziz Aboud aki finance operesheni tokomeza Ngasongwa 2007...2008...2010. Nikikumbuka hawa watu walivyomfanyia visa Alhaj Ngasongwa siamini mpaka leo kama kweli hii ndio Tanzania! Dhambi kubwa ni influence yake ktk kumminya Aboud Morogoro 2000 na 2005 pale alipowabeba wazawa Mazola na Dkt Mzeru.....ktk ubunge, Polyster na vitu kama hivyo. Wasira alimuhofia sana Ngasongwa huku akimuita anajifanya Msomi sana huyu jamaa. Wassira ni janga ambalo limeachwa litamalaki kwa miaka 10 ya JK. Kuna mtu alihoji kwanini Jakaya anayumbishwa na watu wawili wa Mara? kila mmoja ana mapungufu yake but Wassira is the worst thing happened to Jakaya na hana pa kujitenga naye.
 
Waziri Mkuu Mstaafu,Jaji Joseph Sinde Warioba ameandika waraka kumjibu Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Stephen Wasira kwa akauli yake kuwa ndiye aliyemkimbiza CCM kwenda upinzani mwaka 1995. Jaji Warioba amemtaka Wasira ajifunze kusema ukweli kwakuwa mambo anayoyasema yanaweza kumrudia baadaye.

Kimsingi,waraka wa Jaji Warioba unamuasa Wasira kuacha kutumia Jaji Warioba kama mtaji wake katika kutetea msimamo wake juu ya Rasimu ya Katiba mpya."Yeye anafikiria kugombea urais.Ni vizuri basi akajifunza kusema ukweli (ambayo ni ahadi mojawapo ya wanaCCM)"inasema sehemu ya waraka huo.

Chanzo: Mwananchi
 
Weka waraka hapa. Habari isiyo na nyama inakuwa ni mifupa.
 
Siku zote Msemakweli ni ADUI wa ccm!Warioba kawa adui no 1 wa ccm
 

Umeendika nn sasa Mkuu mbona watu mnaendeshwa na chuki??? Kwanza mi ni CDM ila sitaki siasa zenu za majitaka
 
Jamani waraka upo na Mwananchi wamejikongoja kuuweka hadharani.....huu ndio msimu wa kuufahamu ukweli. Nyerere ndie aliyemkimbiza Wasira na si Warioba kama kumbukumbu zetu ziko sawa....1995, ni sawa na Slaa alivyokimbizwa na Mwinyi 1995 pale alipomtaka Qorro ....fact hizi si za kubezwa, Slaa alipinga NEC akagomewa ikabidi atumie haki yake nje ya CCM na akasimamia haki hiyo. Wassira hakufanya hivyo na kibaya zaidi alitumia rushwa ktk kupata ushindi wake....akabainika mahakamani pia. Sasa kuendelea kutudanganya eti alionewa ilihali alikosea mwenyewe, asiyesikia la mkuu huvunjika mguu, kama wengi hamuamini huu waraka utamuumiza Wassira mbele ya safari. Akubali tu amepewa second chance kimagumashi imetosha....kung'ang'ania tena 2015 ni kusaka unhealthy downfall. Ukiiba bila kuonwa...bila kuhisiwa...basi shukuru kuwa umekula na vipofu imetosha. Funika kombe.....
siyo kutukana watu
 
Warioba hana ukweli wowote ni MTU anaependa popularity

Ni umaarufu upi autake zaidi alionao? Tunaweka wazi matendo mabaya ya watu wanaotaka tuamini ni wapenda amani na Tanzania ilihali ni watu wafitini, wasio wakweli na ni hatari sana kwa nchi yetu....Huyu ndie mshauri wa Rais tutegemee nini ? JK amefanya uislamu wake kwa kuwanusuru watu kama hawa ili wazeeke kwa heshima japo kidogo lakini wanamuangusha...hilo si tatizo lake kama ni deni la fadhira 1995 campaign amezilipa huyu Mkuu hana deni, deni liko kwao kina Wassira kuonyesha uaminifu kiutendaji uliotukuka kwa umma na siyo fitina na ulafi wa madaaraka na mali anaouonyesha! Kwanini tusimkemee yeye na ninyi wachumia tumbo wake? Muogopeni Mungu kwa kutenda haki na kuwa wakweli.
 
Ni kweli watu wanajifanya wapambe na kutukana watu hapa mtandaoni! siyo wote tuko imara ktk lugha kengeufu kama hizo.
 
Huyu Mzee Warioba anazeeka vibaya anapenda kutumia MIC kama mswaki wa kusukutua meno, mtu akipiga chafya tu akataja jina lake tayari ameisha wakusanya Wandishi wa Habari.

Arudi Nyamuswa akapumzike, awaombe radhi waikizu kwani amekuwa Makamu wa Rais na Waziri Mkuu kwa muda mrefu lakini hata kisima hakuchimba.
 
huo waraka akiandika Warioba nitaona uzee umemfika kiwango cha juu sasa na ni utoto.

kwa akili yako ya lumumba unaweza kujilinganisha ki elimu au ufahamu zaidi ya jaji warioba?
 
Wasira hajatueleza kuhusu ile BILIONI 1 aliyompatia mwanae.AJIBU KWANZA ILO.

wasira hafai mahakama kuu iliyoketi musoma ilimkuta na hatia ya kutoa rushwa. Hafaiiiii

Anayekutumia amekuharibu ubongo wako, sasa unawaza kama yeye, pole.
Kamwambie Wassira hana kashfa hata moja, hayo yote mnajitahidi kutunga kumchafua Rais wa Watanzania mtarajiwa.
 

Huyu wasira ametufanyia nini hapa bunda?maji tunaenda zaidi ya km 3,wacha kucheza ngoma husiyo ijua sisi ndio tunaojua ubaya wa hao watu wawili.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…