KARLO MWILAPWA
JF-Expert Member
- Apr 10, 2019
- 2,590
- 4,601
Tangu wazee wetu ndani ya CCM ambao wamewahi kuwa makatibu wakuu wa chama kwa nyakati tofauti, Mzee Makamba na Mzee Kinana kutoa waraka wao, nimejifunza jambo moja kubwa nalo ni Imani waliyonayo upinzani kwa CCM na upinzani unaamini CCM ni kubwa sana kuweza kutolewa na upinzani wa sasa.
Sitaki kuzungumzia waraka wala chochote kinachowahusu viongozi hao wastaafu kwa sababu ni suala la kichama na chama kina taratibu zake ambazo sisi wanachama hatuwezi kuziingilia. Mjadala wetu utaegemea ni jinsi gani wapinzani wanavyozungumzia waraka na CCM kwa ujumla.
Kwa siku chache hizi toka waraka umetolewa nimejifunza jambo moja kwa hakika kwa upinzani juu ya CCM, wapinzani wanaamini kwamba CCM ni chama kikubwa sana( maoni ya wapinzani wengi) na kutolewa kwa waraka ule wapinzani wanaona kama ni mgogoro ndani ya chama na wanataka kutumia huo wanaodhani na kufikiri ni mgogoro kama fursa ya kuinua vyama vyao ambavyo vingine bado ni vichanga na vingine vimekuwa ni dhaifu.
Upinzani unaamini kuwa kwa nguvu, uwezo na kukubalika kwa CCM sasa haitawezekana kwa CCM kuondoka madarakani ndani ya miaka 20 ijayo labda kwa miaka 100 au karne 2 zijazo na ukweli ndio huu. Wanaona watanufaika na migogoro ndani ya CCM kwa sababu CCM ilivyo sasa inatisha sana na uwezekano wa kushinda uchaguzi wa serikali za mitaa ni 95% na uchaguzi mkuu ni 90%.
Wapinzani wametupatia kanuni moja kubwa ambayo ni kutumia migogoro ya kisiasa ndani ya CCM kujinufaisha na kujitangaza kisiasa lakini hali hiyo ya kutumia migogoro kutokuwepo kipindi hiki cha Rais Magufuli ndio maana tunaona upinzani umekuwa dhaifu sana na ndio maana wanahakikisha tofauti ndogo ndani ya CCM wanaukuza ili uonekane ni mgogoro.
Nawahahakishia upinzani CCM ya rais Magufuli hakuna migogoro yeyote ya ninyi kuitumia kama fursa na kutoka na kukosekana kwa migogoro hiyo jiandaeni kwa anguko kubwa la kisiasa.
Mmelitendea vema taifa kwa kuwatahadharisha wananchi kwamba upinzani uliopo ni wa kunufaika na fursa za migogoro kutoka CCM na si wa sera.
Sitaki kuzungumzia waraka wala chochote kinachowahusu viongozi hao wastaafu kwa sababu ni suala la kichama na chama kina taratibu zake ambazo sisi wanachama hatuwezi kuziingilia. Mjadala wetu utaegemea ni jinsi gani wapinzani wanavyozungumzia waraka na CCM kwa ujumla.
Kwa siku chache hizi toka waraka umetolewa nimejifunza jambo moja kwa hakika kwa upinzani juu ya CCM, wapinzani wanaamini kwamba CCM ni chama kikubwa sana( maoni ya wapinzani wengi) na kutolewa kwa waraka ule wapinzani wanaona kama ni mgogoro ndani ya chama na wanataka kutumia huo wanaodhani na kufikiri ni mgogoro kama fursa ya kuinua vyama vyao ambavyo vingine bado ni vichanga na vingine vimekuwa ni dhaifu.
Upinzani unaamini kuwa kwa nguvu, uwezo na kukubalika kwa CCM sasa haitawezekana kwa CCM kuondoka madarakani ndani ya miaka 20 ijayo labda kwa miaka 100 au karne 2 zijazo na ukweli ndio huu. Wanaona watanufaika na migogoro ndani ya CCM kwa sababu CCM ilivyo sasa inatisha sana na uwezekano wa kushinda uchaguzi wa serikali za mitaa ni 95% na uchaguzi mkuu ni 90%.
Wapinzani wametupatia kanuni moja kubwa ambayo ni kutumia migogoro ya kisiasa ndani ya CCM kujinufaisha na kujitangaza kisiasa lakini hali hiyo ya kutumia migogoro kutokuwepo kipindi hiki cha Rais Magufuli ndio maana tunaona upinzani umekuwa dhaifu sana na ndio maana wanahakikisha tofauti ndogo ndani ya CCM wanaukuza ili uonekane ni mgogoro.
Nawahahakishia upinzani CCM ya rais Magufuli hakuna migogoro yeyote ya ninyi kuitumia kama fursa na kutoka na kukosekana kwa migogoro hiyo jiandaeni kwa anguko kubwa la kisiasa.
Mmelitendea vema taifa kwa kuwatahadharisha wananchi kwamba upinzani uliopo ni wa kunufaika na fursa za migogoro kutoka CCM na si wa sera.