econonist
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 22,138
- 32,715
Kwakweli nilishangaa ACT walipomchagua Mh Mpina kuwa mgombea wao wa Urais JMT. Nilishangaa Sana kwamba Jana yake kabla hajateuliwa kuwa mgombea urais, Kiongozi wa chama Mama Dorothy Semu alikuwa akimpiga picha za usajili wa kadi ya uanachama live kabisa kqenye TV.
Nikajiuliza swali, inakuaje Mpina atoke CCM Leo kesho yake apewe ugombea urais wa chama? Kwamba ACT hakuna mtu mwenye sifa za kugombea urais zaidi ya Mpina?. Hilo lilinishangaza Sana. Yani ACT wakarudia kosa la 2020 la kumpa ugombea urais mgeni kutoka CCM.
Ushauri wangu ni kwamba vyama vya upinzani viachane na kasumba ya kubeba wagombea urais kutoka CCM ni aibu Sana. Tena mgombea urais anatoka CCM Leo kesho anapewa ugombea urais. Ni kujidharilisha na kujishuaha mbele ya CCM kwamba ndani ya vyama vya upinzani havina watu sahihi mpaka wakope watu kutoka CCM . Nadhani maneno ya Esther Bulaya mliyasikia kwa umakini.
Nikajiuliza swali, inakuaje Mpina atoke CCM Leo kesho yake apewe ugombea urais wa chama? Kwamba ACT hakuna mtu mwenye sifa za kugombea urais zaidi ya Mpina?. Hilo lilinishangaza Sana. Yani ACT wakarudia kosa la 2020 la kumpa ugombea urais mgeni kutoka CCM.
Ushauri wangu ni kwamba vyama vya upinzani viachane na kasumba ya kubeba wagombea urais kutoka CCM ni aibu Sana. Tena mgombea urais anatoka CCM Leo kesho anapewa ugombea urais. Ni kujidharilisha na kujishuaha mbele ya CCM kwamba ndani ya vyama vya upinzani havina watu sahihi mpaka wakope watu kutoka CCM . Nadhani maneno ya Esther Bulaya mliyasikia kwa umakini.