S.Liondo
JF-Expert Member
- Apr 20, 2011
- 3,408
- 1,713
Wakuu ninaomba msaada wa maelekezo, ninatamani sana kuanza biashara ya madini, hii ikimaanisha kuyanunua na kuyauza hata nje ya nchi ikibidi. Ninajua kibali ni kitu cha muhimu sana katika biashara kama hii na hasa ukizingatia serikali tuliyonayo kwa sasa. Ninaomba nijulishwe ni mamlaka ipi au taasisi ipi inayohusika na kutoa kibali cha aina hii? Na pia ni nini watakachohitaji niwe nacho ili nijue kama nimejiandaa vema au la.