h120
JF-Expert Member
- Jan 10, 2012
- 2,545
- 3,367
Habari zenu wana tech,
Najua kuna wapenzi wengi wa gaming, kuna wale wa pc, consoles na pia hata kwenye smartphones wengine huburudika pia.
Leo ntawagusa zaidi wale wa PC, lengo kuu likiwa ni kupeana miongozo katika uundaji wa Gaming pc, najua kuna wengi hawajui wapi ka kuanzia na wapi pa kuishia, ila tutaeleza kidogo kidogo ili kupata ufahamu, miongozo yote twafahamu ipo mtandaoni ila wengine huona uvivu au kuhisi vitu hivo kwa mazingira yetu ni ngumu kuvifanikisha, ila kila kitu kinawezekana.
Changamoto katika uundaji wa gaming pc ni fedha tu, hichi ndicho kikwazo kikuu, maana sote tunajua vitu vizuri vina gharama, ila kama mfuko upo vizuri wala hamna ugumu wowote.
Hivi karibuni nimefanya custom build moja na nitatumia hiyo kama reference katika kuelezana.
Kabla ya hii mashine ya sasa nilikuwa natumia Dell hii:
Dell Optiplex 790
intel core i5 3.1Ghz (Second generation)
8GB RAM
1TB HDD (storage)
64GB SSD (OS) brand samsung
Zotac Geforce GTX 560 1GB
Hii niliiuza nadhani hata wengine mtakua mliona mabandiko ya hii mashine humu JF, niliamua kuuza kwasababu nilitaka kufanya upgrade. Niliuza mashine peke yake na Graphics card peke yake, hivyo nilikuwa na fungu la kuanzia katika mashine mpya nitakayo ijenga.
Manunuzi baadhi ya vitu nimefanya Ebay na vingine hapa hapa nyumbani TZ, sinta zungumzia jinsi ya kufanya manunuzi ebay kwasababu tayari zipo thread zimechambua na kuelezea A to Z kwa newbies.
Kitu cha kwanza kabisa kutafuta ilikuwa ni processor, unaweza ukauliza kwanini processor, kwa upande wangu processor ilikuwa ni muhimu kuitafuta kwanza kwasababu, options za kupata motherboard itakayo support processor husika ilikuwa ni rahisi, kwa ufafanuzi zaidi ni kwamba ningepata motherboard kwanza ningesumbuka kupata processor ya hiyo motherboard, ila ningepata processor kwanza nisingesumbuka kupata motherboard ya hiyo processor.
Motherboard huendana na processor huwezi chukua processor aina fulani ukaiweka kwa motherboard fulani ikafanya kazi unless ziwe compatible, (Na compatibility hatuangalii ufanano wa pin za processor, pin zaweza fanana na zisiwe compatible, mafundi wetu bongo wengi huangalia ufanano ila si sahihi kufanya hivo unatakiwa kuangalia specs za processor au motherboard husika) Ipo thread Chief-Mkwawa amezichambua bila shaka.
Nilinunua processor kupitia humuhumu jamvini kwa nixp ni intel core i5 3.2Ghz Fourth generation, mnaweza kumcheki anauza uza parts za pc, cards n etc.
Baada ya kupata processor motherboard haikuwa shida sana kuipata, Hivyo niliagiza motherboard kupitia Ebay, Motherboard zipo aina nyingi na zenye specs tofauti tofauti chakuangalia kwanza ni compatibility halafu ndio urukie kwenye features na korokoro nyingine, kwa processor niliyokuwa nayo ya Haswell(Fourth generation) nilihitaji motheboard ya socket LGA 1150 (hii ina support 4th na 5th generation intel processors)
Model niliyochukua ni GIGABYTE Z97X-SLI LGA1150 i3/i5/i7 ATX
Gharama ni $105.62 + $26.39 shipping
Graphics card
Niliagiza MSI GTX 960 2gb, nilinunua 2 moja niliuza
Gharama $165 + $40 shipping (kwa moja)
Power supply
Hii niliagiza mwaka jana, OCZ ModXStream Pro 500 W 80+ efficiency
Gharama $60 (free shipping)
Case/Chasis
Hili ni jumba na kuhidhi motherboard na makorokoro yote, nilitafuta case itakayoendana na motherboard yangu, case zipo aina nyingi na zina ukubwa tofauti, chasis nzuri ni za hp kwasababu zina support ATX motherboard nyingi tofauti na za dell, nilinunua chasis ya HP XW 4300, nimefanya modification chache kwenye switch na motherboard backet ili motherboard yangu ikae vizuri.
Gharama 45,000 (Bei hii ni kubwa sana kwa PC case ila maeneo nilipo nilikuwa sina alternative option, bei za case ni 10,000-20,000 zisizidi hapo)
CPU heat sink
Arctic Cooling Freezer 7 Pro Rev 2 CPU Cooler
Hii ni cooler ya kupooza processor, nayo nimefanya kuagiza yenye ubora zaidi
Gharama $37 pamoja na shipping (Hii bado haijafika)
HDD, RAM,
Nilikuwa na reserve HDD ya 500GB na pia nimepata SSD ya 120GB kwa mdau wangu mmoja, pia kwa sasa RAM ninazo ya 4GB soon nitaongeza nataka niwe na 8GB yatosha.
Hapo ndipo nimefikia kwa sasa nangoja cooler ifike niwashe Mashine,
Total cost $493.25
****UPDATE****
CPU fan imefika
Karibuni kwa maswali na michango zaidi.
Najua kuna wapenzi wengi wa gaming, kuna wale wa pc, consoles na pia hata kwenye smartphones wengine huburudika pia.
Leo ntawagusa zaidi wale wa PC, lengo kuu likiwa ni kupeana miongozo katika uundaji wa Gaming pc, najua kuna wengi hawajui wapi ka kuanzia na wapi pa kuishia, ila tutaeleza kidogo kidogo ili kupata ufahamu, miongozo yote twafahamu ipo mtandaoni ila wengine huona uvivu au kuhisi vitu hivo kwa mazingira yetu ni ngumu kuvifanikisha, ila kila kitu kinawezekana.
Changamoto katika uundaji wa gaming pc ni fedha tu, hichi ndicho kikwazo kikuu, maana sote tunajua vitu vizuri vina gharama, ila kama mfuko upo vizuri wala hamna ugumu wowote.
Hivi karibuni nimefanya custom build moja na nitatumia hiyo kama reference katika kuelezana.
Kabla ya hii mashine ya sasa nilikuwa natumia Dell hii:
Dell Optiplex 790
intel core i5 3.1Ghz (Second generation)
8GB RAM
1TB HDD (storage)
64GB SSD (OS) brand samsung
Zotac Geforce GTX 560 1GB
Hii niliiuza nadhani hata wengine mtakua mliona mabandiko ya hii mashine humu JF, niliamua kuuza kwasababu nilitaka kufanya upgrade. Niliuza mashine peke yake na Graphics card peke yake, hivyo nilikuwa na fungu la kuanzia katika mashine mpya nitakayo ijenga.
Manunuzi baadhi ya vitu nimefanya Ebay na vingine hapa hapa nyumbani TZ, sinta zungumzia jinsi ya kufanya manunuzi ebay kwasababu tayari zipo thread zimechambua na kuelezea A to Z kwa newbies.
Kitu cha kwanza kabisa kutafuta ilikuwa ni processor, unaweza ukauliza kwanini processor, kwa upande wangu processor ilikuwa ni muhimu kuitafuta kwanza kwasababu, options za kupata motherboard itakayo support processor husika ilikuwa ni rahisi, kwa ufafanuzi zaidi ni kwamba ningepata motherboard kwanza ningesumbuka kupata processor ya hiyo motherboard, ila ningepata processor kwanza nisingesumbuka kupata motherboard ya hiyo processor.
Motherboard huendana na processor huwezi chukua processor aina fulani ukaiweka kwa motherboard fulani ikafanya kazi unless ziwe compatible, (Na compatibility hatuangalii ufanano wa pin za processor, pin zaweza fanana na zisiwe compatible, mafundi wetu bongo wengi huangalia ufanano ila si sahihi kufanya hivo unatakiwa kuangalia specs za processor au motherboard husika) Ipo thread Chief-Mkwawa amezichambua bila shaka.
Nilinunua processor kupitia humuhumu jamvini kwa nixp ni intel core i5 3.2Ghz Fourth generation, mnaweza kumcheki anauza uza parts za pc, cards n etc.
Baada ya kupata processor motherboard haikuwa shida sana kuipata, Hivyo niliagiza motherboard kupitia Ebay, Motherboard zipo aina nyingi na zenye specs tofauti tofauti chakuangalia kwanza ni compatibility halafu ndio urukie kwenye features na korokoro nyingine, kwa processor niliyokuwa nayo ya Haswell(Fourth generation) nilihitaji motheboard ya socket LGA 1150 (hii ina support 4th na 5th generation intel processors)
Model niliyochukua ni GIGABYTE Z97X-SLI LGA1150 i3/i5/i7 ATX
Gharama ni $105.62 + $26.39 shipping
Graphics card
Niliagiza MSI GTX 960 2gb, nilinunua 2 moja niliuza
Gharama $165 + $40 shipping (kwa moja)
Power supply
Hii niliagiza mwaka jana, OCZ ModXStream Pro 500 W 80+ efficiency
Gharama $60 (free shipping)
Case/Chasis
Hili ni jumba na kuhidhi motherboard na makorokoro yote, nilitafuta case itakayoendana na motherboard yangu, case zipo aina nyingi na zina ukubwa tofauti, chasis nzuri ni za hp kwasababu zina support ATX motherboard nyingi tofauti na za dell, nilinunua chasis ya HP XW 4300, nimefanya modification chache kwenye switch na motherboard backet ili motherboard yangu ikae vizuri.
Gharama 45,000 (Bei hii ni kubwa sana kwa PC case ila maeneo nilipo nilikuwa sina alternative option, bei za case ni 10,000-20,000 zisizidi hapo)
CPU heat sink
Arctic Cooling Freezer 7 Pro Rev 2 CPU Cooler
Hii ni cooler ya kupooza processor, nayo nimefanya kuagiza yenye ubora zaidi
Gharama $37 pamoja na shipping (Hii bado haijafika)
HDD, RAM,
Nilikuwa na reserve HDD ya 500GB na pia nimepata SSD ya 120GB kwa mdau wangu mmoja, pia kwa sasa RAM ninazo ya 4GB soon nitaongeza nataka niwe na 8GB yatosha.
Hapo ndipo nimefikia kwa sasa nangoja cooler ifike niwashe Mashine,
Total cost $493.25
****UPDATE****
CPU fan imefika
Karibuni kwa maswali na michango zaidi.