Wapendwa.

Mwammbelo

JF-Expert Member
Jun 9, 2013
349
159
Wapendwa.
Kuna hii issue nmeona *Danford Kitwana* ameshare nahali fulani japo ni kwa wanansdoa lakini nadhani hata wengine humu bachelors/singles linatuhusu..

In short madhara ya *ndoa za mbali*..


Tafadhali soma hadi mwisho kuiponya ndoa yako... C&P

BARUA YA DHARULA KWA WANANDOA WOTE
(Nakala kwa mnaotarajia kuingia ndoani)

Ndugu wanandoa,
Nawasalimu salamu za mwisho wa mwezi!

Mahusiano ya wanandoa wanaoishi sehemu tofauti kwa kigezo cha kazi au masomo ni hatari Sana kwa ustawi wa ndoa yako,ni sawa na mtu anayelima shamba Iringa yeye anaishi dar ,yeye anapiga simu tu na kutegemea kuvuna mavuno kedekede.

Mme unaishi Mwanza mke anaishi mtwara halafu mnasema mmeoana.Ninakupa tahadhari kwa nguvu ya Roho Mtakatifu aliyeko ndani yangu. Eva alikuja kulubuniwa na nyoka baada ya kuona kuwa Adamu ameondoka,nina uhakika kama Eva angekuwa na mme wake nyoka asingethubutu kumsogelea Eva na kumdanganya.

Kuna mambo mengine mkiwa mnaishi pamoja mke na mme shetani hawezi kuthubutu kuyaleta ila ile kutengana shetani anapata hapo mwanya wa kuja kuwajaribu.Nimeshuhudia ndoa nyingi ambazo zimepigwa kwa jinsi hii.Ninawaonya binti zangu BHM na wale mlio kwenye ndoa tayari kuepuka jambo hili kwa garama yoyote.Msije kusema sikuwambia.

ELOI! ELOI!

Maneno hayo hapo juu isipokuwa kichwa cha habari na salamu, vimeandikwa na dada na mshirika wangu wa kiagano, Winnie Nzobakenga. Mimi nina pointi zifuatazo kama nyongeza:-

1). Kinachosababisha kufika hali hii sio serikali kukataa kuhamisha watumishi, bali ni wafanyakazi wenyewe kukataa kuhamisha akili. Shida ya kwanza kwa wengi ni kuamini kwamba ajira ni kila kitu. Shida ya pili ni vipaumbele. Ukiona unaacha mke Dar unaenda kufanya kazi Mtwara, na mke nae akawa mwajiriwa na miongoni mwenu hakuna alietayari kuacha kazi kumfuata mwingine, mjue kwamba wote wawili hakuna ambae ameweka ndoa kama kipaumbele cha kwanza!

2). Nioneshe mtu aliewahi kuthamini ajira kuliko ndoa halafu ndoa ikabaki salama kwa muda mrefu. Mnaweza kusema ohooo, tunaaminiana, mara ohooo, mke wangu/mume wangu hawezi kunisaliti, sikatai! Enhee, akishakuwa hajakusaliti what is next? Nyie ni watu wazima bana, naomba niwaeleze kwamba kuna mambo ambayo maombi yanaweza kuhamisha, lakini kuna mambo yapo mwilini huwa hayahami kwa maombi ng'oooo. Ukiamua kubisha shauri yako mwenyewe! Wewe umekomaa na ajira yako huko Mwanza mume umemuacha Dar, halafu unategemea maombi ya kwa Nabii Malisa, eti Mungu amlinde mumeo kule Dar? Subiri uvune mabua, ndio utaelewa!

3). Halafu aliewaambia kwamba mmoja akiacha ajira kumfuata mwingine, eti mtakufa na njaa nani? Shida yenu ni kwamba tukiwaelekeza ujasiriamali mnaona as if hauwahusu, ndio maana ajira mnazitetemekea kiasi cha ku-risk ndoa zenu. Aliekudanganya kwamba ukiwaachia liajira lao wanalokulipa "vilaki nane", ukamfuata mke/mme na kupiga ujasiriamali, utakosa kuzalisha zaidi ya laki nane, ni nani huyo? Unajua ninawamaindi kwa sababu, nilishawaelezaga kwamba kwenye ajira mnalipwa asilimia chini ya kumi ya mnachozalisha, sasa kinawashinda nini kuzitoa sadaka ajira ili mkaokoe ndoa? Nakuona tu unavyonibinulia midomo, na kunifyonya, lakini huu ndio ukweli.

4). Haya basi! Tuseme ninyi ni wa kisasa, so, ishu ya ndoa ya bluetooth haiwasumbui, je, hayo malezi ya watoto inakuwaje? Mke Kigoma, mume Arusha, watoto wako boarding Tabora! What a wastage of parentalhood! Shida yenu mlio wengi mnadhani ni sifa kupeleka watoto wa chekechea boarding in the name of kutingwa ama in the name of ajira. Laiti mngekielewa ambacho Mtume Paulo alimweleza Timotheo kuhusu watoto (2Tim 3:15), msingekubali mtindo huu, ama mtindo wa baba kusubiri miezi sita ama mwaka ndio akawaone watoto kwa mkewe, maana watoto wanalelewa na mama Songea baba akiwa kazini Dodoma!

5). Hadi hapa najua nimeshawakorofisha watu, maana ndoa za masafa siku hizi imekuwa ndio fasheni, kwamba mke na mume wakikutana ni spesho kwa ajili ya ujauzito na from there huyu kule mwingine huko. Hivi aliewaeleza kwamba ndoa ni just ijulikane umeoa ama umeolewa ni nani? Kwani haijaandikwa kwamba mmeoana ili muishi pamoja?

Hata hizo hela mnazotafuta (if ni nyingi kihivo) mnawezaje kuzipangia matumizi na maendeleo ya familia? Au ndio mnategemea bando la halichachi na jazwa ujazwe na WhatsApp kujadiliana kuhusu familia? Hivi mnajua kwamba kuna nguvu kubwa kupanga mambo ya ndoa na familia mkiwa mnatazamana kwa macho na mwenzi wako? Mkoje, nyieeee? Kwani maparoko, mapasta na mashehe hawawaelezi haya?

Wakinga huwa wanasema vyungu viwili huwa vinamaliza kuni haraka. Mume uko Tanga una bajeti ya nyumba, mke yuko Geita nae ana bajeti ya nyumba, hee, kwa mishahara hii ya chini ya milioni mbili, lini mtafanya maendeleo ya maana?. Ni ujinga mkubwa wa kiwango cha utoroshaji wa makinikia, wanandoa kuishi mbalimbali na ku-risk ndoa eti kwa mishahara ambayo inaishia kwenye matumizi!

By the way, who told you kwamba hata muajiriwe ajira tatu-tatu eti ndio mtakuwa na financial freedom? Wengine wananiuliza, "Je, kwa waliopo masomoni inakuwaje?". Haaa! Haaa! Mie leo naongelea mnaofanya kazi, mengine msinipangie!

6). Mmeambiwa kwamba kisiwepo cha kuwatenganisha isipokuwa kifo. Hamuoni kwamba ajira zimeshakuwa vifo? Mnapata wapi ujasiri wa kuishi na kifo mkingali hai? Nyie mnaujasiri sana. Yaani kifo kinazunguka zunguka, mpo tu mwaka wa kwanza, mwaka wa pili, mwaka wa tatu mnakitazama tu???!!!?? Kweli? Mbona mna hatari namna hiyo!

7). Pointi hii yaweza kuwa ngumu zaidi. Unajua wanaume huwa wanasisimka kwa kuona(kutazama), right? The fact is, asipokua anakiona anachokipenda mara kwa mara (yaani mke wake) ataanza kuona mibadala, hata kama ni "mlokole masalia". Mwanamke anasisimuliwa kwa kusikia (with physical expression). Ndio maana hata mke ukimuangalia usoni na kumwambia, "Nakupenda", anasisimka zaidi kuliko ukimpigia simu na kumwambia, "Nakupenda".

Mpo? Mwanamke anaihesabu "care" kwa kupima ukaribu, (yaani muda unaokua nae physically). Wanawake ni kama watoto, sio kiakili bali kwa hitaji lao la kuwa cared to the maximum. Mwanamke yeyote unaweza kumpata kiurahisi ikiwa kuna factor mbili:- mosi, ikiwa mumewe amezembea kum-care. Pili, ikiwa muwindaji utatumia sayansi ya ku-care. (Mliooa shikeni pointi hapa mnafanya uzembe halafu nyani wanakula mahindi yenu).

So, mwanamke alieolewa anapokuwa mbali na mumewe, huwa anakuwa na gepu fulani, hata kama awe anajikaza. Kuna two things hapa:- gepu hilo likiwepo ndio anaweza kuendelea kujikaza lakini ikizidi sana atakuwa anaumia na itamuathiri. Akiwa anavumilia ashukuriwe Mola. Pili ni kwamba anaweza kutafuta mbadala.

Wanaume ukiona ametafuta mbadala automatically huwa ni kwa ajili ya ngono lakini wanawake huwa wanatamani just care, baasi. The question comes, wanaume wangapi wanaweza kuwa karibu na wake za watu kwa extend ya ku-care that much halafu wawaache pasipo kuwakula? Ndio ile unakuta mke wa mtu ameshaliwa halafu anasema, "Wewe kaka Abdul nilikuwa nakuchukulia kama kaka yangu lakini umenifanya tumefanya hivi, basi iwe siri yetu".

8). Baadhi ya wanawake mlioolewa katika ndoa hizi za bluetooth mnanichekeshaga sana. Unakuta unabana kabisa pua eti, "Siwezi kuacha ajira, coz wazazi hawatanielewa maana walinisomesha", heee! Unataka kueleweka kwa wazazi ama unataka kueleweka kwa mumeo? Shida yenu (baadhi yenu), vielimu vyenu vimeshawapotezea utii na unyenyekevu kiasi kwamba mnaamua ya kwenu ndani ya ndoa as if bado mko mabachela. Mie ni mmoja ya wanaume wanaosisitiza wanawake wafanye kazi (akiwemo mke wangu), lakini niko aggressive sana linapokuja suala la mke kuthamini maslahi ya ndoa na familia kwa MAJADILIANO. Ukishabana pua yako na kuanza kuwasikiliza wazazi maana yake ni kwamba hamuwezi kufikia muafaka na mumeo kwa suala hili la ndoa ya bluetooth! OLE WAKO NIKUKUTE, maana bakora za mgongo zitakuhusu!

HEBU TUOMBE....

Mungu wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukikemea na kukomesha ndoa zote za bluetooth maana zimekuwa kiota cha michepuko na kuathirika kwa malezi ya watoto. Kabla mwaka huu haujaisha, ndoa nyingi za bluetooth zisiwepo hasa kwa huyu alienisoma na kunielewa, Ameeeen!

MAANA....

Kuna wengine mnapolia kuhusu ndoa, kumbe inabidi tukemee tu kifo, ili mpoteze ajira mkaokoe ndoa! [HASHTAG]#SmartMind[/HASHTAG]
 
ndefuuu sanaaaa
ila maudhui yalikuwa safi kama ingekuwa fupi

ila ndio mambo ya kuoana watu wote mmeajiriwa, tukiwaambia hapa oeni walo ishia la saba hamtaki, sasa mtajua wenyewe, na kama hivi Magufuli kataza kuhama lazma ndoa nyingi zitakuwa hatarini. au wale wanao hamia dodoma nusu nusu wale, kazi kwenu.
 
Back
Top Bottom