Wapendekeza awamu urais iwe miaka saba

Wapendekeza awamu urais iwe miaka saba

Power G

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2011
Posts
3,884
Reaction score
1,200
Baadhi ya wajumbe wa Bunge Katiba wamependekeza kuongezwa muda wa rais kukaa madarakani kutoka miaka mitano ya sasa hadi saba katika kipindi kimoja.

Wajumbe hao wanadaiwa kutoa wazo hilo ndani ya Kamati Namba 12 ilipokuwa ikijadili sura ya saba ya Rasimu ya Katiba, inayohusu Serikali, Rais, Makamu wa Rais na Baraza la Mawaziri katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Habari zilizolifikia gazeti hili na kuthibitishwa na mwenyekiti wa kamati hiyo, Paul Kimiti, wazo la kutaka kuongezwa kwa muda huo lilijengwa katika msingi kwamba miaka saba itamwezesha kiongozi huyo mkuu wa nchi kutekeleza vyema ahadi alizotoa kwenye uchaguzi.


“Ni mtazamo wa baadhi ya wajumbe kuwa pamoja na hilo kuongeza miaka kutaepusha utumiaji wa fedha nyingi ndani ya muda mfupi kutokana na gharama za uchaguzi,” kilisema chanzo chetu ndani ya kamati.


“Waliona kwa nchi zenye uchumi mchanga, suala la kufanya uchaguzi kila baada ya miaka mitano linagharimu ukuaji katika sekta ya maendeleo kutokana na gharama kubwa za uchaguzi huo”.


Kimiti alisema licha ya hoja hiyo kuwa na mashiko, wajumbe walisema ikiwa muda wa kukaa madarakani utaongezwa, hauwezi kuwa kwa rais pekee, bali kwa wabunge na nafasi nyingine kama madiwani.

Source: Mwananchi .

Maoni yangu:- Hiyo ndiyo CCM yenye kutuletea katiba mpya watz!!
 
Baadhi ya wajumbe wa Bunge Katiba wamependekeza kuongezwa muda wa rais kukaa madarakani kutoka miaka mitano ya sasa hadi saba katika kipindi kimoja.

Wajumbe hao wanadaiwa kutoa wazo hilo ndani ya Kamati Namba 12 ilipokuwa ikijadili sura ya saba ya Rasimu ya Katiba, inayohusu Serikali, Rais, Makamu wa Rais na Baraza la Mawaziri katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Habari zilizolifikia gazeti hili na kuthibitishwa na mwenyekiti wa kamati hiyo, Paul Kimiti, wazo la kutaka kuongezwa kwa muda huo lilijengwa katika msingi kwamba miaka saba itamwezesha kiongozi huyo mkuu wa nchi kutekeleza vyema ahadi alizotoa kwenye uchaguzi.


"Ni mtazamo wa baadhi ya wajumbe kuwa pamoja na hilo kuongeza miaka kutaepusha utumiaji wa fedha nyingi ndani ya muda mfupi kutokana na gharama za uchaguzi," kilisema chanzo chetu ndani ya kamati.


"Waliona kwa nchi zenye uchumi mchanga, suala la kufanya uchaguzi kila baada ya miaka mitano linagharimu ukuaji katika sekta ya maendeleo kutokana na gharama kubwa za uchaguzi huo".


Kimiti alisema licha ya hoja hiyo kuwa na mashiko, wajumbe walisema ikiwa muda wa kukaa madarakani utaongezwa, hauwezi kuwa kwa rais pekee, bali kwa wabunge na nafasi nyingine kama madiwani.

Source: Mwananchi .

Maoni yangu:- Hiyo ndiyo CCM yenye kutuletea katiba mpya watz!!

Eee mungu tuepushe na hili janga lisitufike kwani huu muda wa miaka mitano mitano uliokuwepo tulitaman hata upunguzwe kwa sababu ya kuona jinsi maisha yanavyozidi kuwa magumu kwa viongozi kujisaau kabisa na kutuacha wananchi tukiangamia.....Wanataka iwe hivyo ili kula ya wateule wa rais izidi kuwa pana na mmbadilisho wa mawaziri miozigo kama kawa?/???????????????KIAMA
 
Eee mungu tuepushe na hili janga lisitufike kwani huu muda wa miaka mitano mitano uliokuwepo tulitaman hata upunguzwe kwa sababu ya kuona jinsi maisha yanavyozidi kuwa magumu kwa viongozi kujisaau kabisa na kutuacha wananchi tukiangamia.....Wanataka iwe hivyo ili kula ya wateule wa rais izidi kuwa pana na mmbadilisho wa mawaziri miozigo kama kawa?/???????????????KIAMA
Hii ndiyo katiba ambayo ccm wamebaki wakijitungia baada ya UKAWA kuondoka, tutegemee katiba ya mazingaombwe zaidi!!
 
Nhnnnn.....haya majanga! miaka hii 5 kuimaliza imekuwa mbide...kama ingekuwa saba je.
 
Nchi hii inanipa hasira sana
 
Hapa suala si rais kukaakipindi cha miaka saba saba badala ya mitano mitano,kikubwa ni huyo rais ana deliver nn ndani ya hicho kipindi? Kama anashindwa kuleta maendeleo ndani ya miaka kumi hiyo miaka kumi na nne ndo ataweza? Tatizo la baadhi ya wajumbe ni ulevi wa hizo posho, waongee vitu vyenye tija kuliko porojo hizo.kwa kiongozi mwenye focus na vision juu ya taifa lake na watu wake miaka kumi ni mingi. Tatizo muda mwingi wanautumia kushughurikia mambo yao personal badala ya kulitumikia taifa.
 
Mimi nashindwa kuelewa, sasa kulikuwa na maana gani huyu dhaifu kuunda kamati ya Warioba kama hawa mburura walikuwa na uwezo Wa kuandika rasmu bila kuwazungukia RAIA? Mara tunasikia mahakama ya kadhia, na sasa umri Wa kukaa madarakani iwe seven hivi kama taifa tunaenda wapi?Tanzanian youth wake up!!
 
Watanzania tunakaa kwenye keyboard kuandika porojo na kulalamika ni upuuzi mtupu
Ushauri tokeni kwenye keyboard tuingie barabarani tupaze sauti zetu kuitetea Tanganyika yetu.
 
Mi nadhani hawa wajumbe wa BMK hawajui wanachotakiwa kufanya Dodoma. Hawa walikuwa ni wananchi wa kawaida na walitoa maoni yao wakati tume inakusanya maoni...
 
Back
Top Bottom