Ngongo
JF-Expert Member
- Sep 20, 2008
- 18,800
- 30,725
Serikali imebaini kuwapo mpango mchafu wa kutaka kuvuruga ziara ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Ban Ki-moon nchini, imeelezwa.Akizungumza jana Dar es Salaam, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe, alisema kuna kundi la watu wanaojiita 'Wazee wa Pemba' linapanga siku hiyo kuingilia ratiba ya mgeni huyo na kufanya maandamano.
Katibu Mkuu wa UN anatarajia kufanya ziara kuanzia kesho hadi Jumamosi, kutokana na mwaliko aliopewa na Rais Jakaya Kikwete walipokutana New York, Marekani, Septemba mwaka jana.
Waziri alisema baada ya Serikali kulibaini hilo, hivi sasa inalifanyia kazi ikiwa ni pamoja na lile la wapinzani wa Ba Ki-moon kutoka nje ya nchi, wanaopanga kutumia baadhi ya vyombo vya habari kuandika habari mbaya kumhusu."Ombi letu ni kuhakikisha watu hao hawafanikiwi katika azma yao ya kutumia vyombo vya habari vya hapa nchini kuandika mambo mabaya ya kumchafulia jina mgeni wetu," alisema Waziri Membe.
Waziri alisema ziara ya Ban Ki-moon ina lengo kuu moja, la kuimarisha uhusiano baina ya Tanzania na UN. Katibu Mkuu akiwa nchini mbali ya kufanya mazungumzo na Raia Kikwete, pia atatembelea miradi inayosimamiwa na mashirika mbalimbali ya UN na mradi wa majaribio wa ONE UN.
Pia atakwenda Zanzibar keshokutwa na kufanya mazungumzo na Rais Amani Abeid Karume na kuzindua jengo la UN Zanzibar, kisha atakwenda Arusha kutembelea Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR). Katibu Mkuu huyo aliipa heshima kubwa Tanzania ya kumteua Mtanzania kushika nafasi ya Naibu Katibu Mkuu wa UN, Dk Asha-Rose Migiro, ambaye ni mwanamke wa kwanza duniani kushika wadhifa huo.
Waziri Membe alisema Ki-moon ni rafiki mkubwa wa Tanzania na Afrika, kwani hata kabla ya kuwa na nafasi aliyo nayo sasa, akiwa waziri wa mambo ya nje wa Korea Kusini, aliishawishi serikali yake kuipa Tanzania misaada. Miongoni mwa misaada hiyo ni kujenga daraja la Malagarasi, Kigoma, ujenzi wa vyuo vya ufundi, ujenzi wa hospitali ya kufundishia chuo kikuu Muhimbili na mingine mingi.
Alitoa mwito kwa wananchi kumpokea kwa wingi na kwa heshima kubwa. Mei 12 mwaka jana wazee 12 walikamatwa na Polisi Zanzibar kwa tuhuma za kudai Pemba ijitenge na Zanzibar, kwa madai kuwa ilikuwa imesahaulika kwa maendeleo. Kwa mujibu wa ofisa usalama wa Chama cha Wananchi (CUF), aliyetajwa kwa jina la Said Miraji, wazee hao walikamatwa usiku.
Wazee hao wiki moja kabla walikuwa wamewasilisha madai yao kwa Ofisa Mwandamizi wa UN, Dar es Salaam, Oscar Fernandez-Taranco, wakimtaka awasilishe madai yao hayo kwa Ki-moon.Baada ya kukamatwa kwa wazee hao, CUF ilisema ilikuwa imewaagiza wabunge wake kutunza familia za wazee hao, huku chama hicho kikishughulikia hatima yao.
Miraji alithibitisha kuwa waliokamatwa walikuwa wafuasi wa CUF. Mwezi mmoja kabla ya kukamatwa kwao, wazee hao walikuwa wamemtaka aliyekuwa Balozi wa Marekani nchini, Mark Green, kuwasilisha ujumbe wao kwa Rais George Bush, ili awasaidie kujitenga na Muungano wa Zanzibar na Bara.
SOURCE:Habari leo.
Duh hii kali.Membe anataka kutuaminisha wazee wapemba wanataka kuvuruga ziara ya Ki-moon,hawana hoja ya msingi.Kwa maoni yangu naamini wazee wa Pemba wanataka kuwasilisha malalamiko ya mauaji ya ndugu zao wakati wa uchaguzi mkuu 1995.Serekali kwa upande wake wanaona hizo ni vurugu hawataki jumuiya ya kimataifa na hasa katibu mkuu kujua maafa yaliyowakuta ndugu zetu wa Pemba.Chonde chonde Membe wazee wa kipemba wapewe nafasi ya kuwasilisha malalamiko pengine wahusika wakuu wa mauaji wataweza kufikishwa mahakamani.
Katibu Mkuu wa UN anatarajia kufanya ziara kuanzia kesho hadi Jumamosi, kutokana na mwaliko aliopewa na Rais Jakaya Kikwete walipokutana New York, Marekani, Septemba mwaka jana.
Waziri alisema baada ya Serikali kulibaini hilo, hivi sasa inalifanyia kazi ikiwa ni pamoja na lile la wapinzani wa Ba Ki-moon kutoka nje ya nchi, wanaopanga kutumia baadhi ya vyombo vya habari kuandika habari mbaya kumhusu."Ombi letu ni kuhakikisha watu hao hawafanikiwi katika azma yao ya kutumia vyombo vya habari vya hapa nchini kuandika mambo mabaya ya kumchafulia jina mgeni wetu," alisema Waziri Membe.
Waziri alisema ziara ya Ban Ki-moon ina lengo kuu moja, la kuimarisha uhusiano baina ya Tanzania na UN. Katibu Mkuu akiwa nchini mbali ya kufanya mazungumzo na Raia Kikwete, pia atatembelea miradi inayosimamiwa na mashirika mbalimbali ya UN na mradi wa majaribio wa ONE UN.
Pia atakwenda Zanzibar keshokutwa na kufanya mazungumzo na Rais Amani Abeid Karume na kuzindua jengo la UN Zanzibar, kisha atakwenda Arusha kutembelea Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR). Katibu Mkuu huyo aliipa heshima kubwa Tanzania ya kumteua Mtanzania kushika nafasi ya Naibu Katibu Mkuu wa UN, Dk Asha-Rose Migiro, ambaye ni mwanamke wa kwanza duniani kushika wadhifa huo.
Waziri Membe alisema Ki-moon ni rafiki mkubwa wa Tanzania na Afrika, kwani hata kabla ya kuwa na nafasi aliyo nayo sasa, akiwa waziri wa mambo ya nje wa Korea Kusini, aliishawishi serikali yake kuipa Tanzania misaada. Miongoni mwa misaada hiyo ni kujenga daraja la Malagarasi, Kigoma, ujenzi wa vyuo vya ufundi, ujenzi wa hospitali ya kufundishia chuo kikuu Muhimbili na mingine mingi.
Alitoa mwito kwa wananchi kumpokea kwa wingi na kwa heshima kubwa. Mei 12 mwaka jana wazee 12 walikamatwa na Polisi Zanzibar kwa tuhuma za kudai Pemba ijitenge na Zanzibar, kwa madai kuwa ilikuwa imesahaulika kwa maendeleo. Kwa mujibu wa ofisa usalama wa Chama cha Wananchi (CUF), aliyetajwa kwa jina la Said Miraji, wazee hao walikamatwa usiku.
Wazee hao wiki moja kabla walikuwa wamewasilisha madai yao kwa Ofisa Mwandamizi wa UN, Dar es Salaam, Oscar Fernandez-Taranco, wakimtaka awasilishe madai yao hayo kwa Ki-moon.Baada ya kukamatwa kwa wazee hao, CUF ilisema ilikuwa imewaagiza wabunge wake kutunza familia za wazee hao, huku chama hicho kikishughulikia hatima yao.
Miraji alithibitisha kuwa waliokamatwa walikuwa wafuasi wa CUF. Mwezi mmoja kabla ya kukamatwa kwao, wazee hao walikuwa wamemtaka aliyekuwa Balozi wa Marekani nchini, Mark Green, kuwasilisha ujumbe wao kwa Rais George Bush, ili awasaidie kujitenga na Muungano wa Zanzibar na Bara.
SOURCE:Habari leo.
Duh hii kali.Membe anataka kutuaminisha wazee wapemba wanataka kuvuruga ziara ya Ki-moon,hawana hoja ya msingi.Kwa maoni yangu naamini wazee wa Pemba wanataka kuwasilisha malalamiko ya mauaji ya ndugu zao wakati wa uchaguzi mkuu 1995.Serekali kwa upande wake wanaona hizo ni vurugu hawataki jumuiya ya kimataifa na hasa katibu mkuu kujua maafa yaliyowakuta ndugu zetu wa Pemba.Chonde chonde Membe wazee wa kipemba wapewe nafasi ya kuwasilisha malalamiko pengine wahusika wakuu wa mauaji wataweza kufikishwa mahakamani.