Waongoza mijadala kwenye TV wadhaifu.

Waongoza mijadala kwenye TV wadhaifu.

Jacobus

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2011
Posts
4,707
Reaction score
1,729
Nimekuwa nikibahatika kuona mijadala hasa kwenye televisions za Star(Startv) na ITV kuhusiana na mambo mbalimbali.
Kitu nilichogundua mpaka sasa ni kuwa kama patakuwa na mada inayohusisha vyama vya siasa mfano pawe na mwakilishi wa CCM, CHADEMA, CUF n.k. basi uongoza mjadala atazidiwa (sijui makusudi au ushabiki) na mmoja wa waalikwa kwa kwenda NJE kabisa na mada husika.
Niliona kwenye Startv wakati Yahya Mohamed akiongoza mjadala uliowahusisha mh Migulu Nchemba (CCM), mh Zito Kabwe (CHADEMA) na Julius Mtatilo (CUF). Wale wa CHADEMA na CUF walijikita HASWA kwenye mada lakini wa CCM yeye aliamua kuingiza ya kwake na kumshambulia Zito na chama chake huku Yahya akiangalia tuu bila ya kumkosoa.
Jana pia nilibahatika kuona mjadala kwenye ITV (Kipima Joto), muongozaji ni mtangazaji mahiri bwana Masako. Kwenye mjadala huo licha ya kuhusisha CCM (mh Ndugai) na CHADEMA (mh Lisu) pia palikuwa na waalikwa wawili toka asasi nyingine. Kama kawaida (hii naamini sasa) mh Ndugai akatoka kwenye mada husika na kuanza kumshambulia Lisu na chama chake bila hata bwana Masako kumkatiza mpaka pale mh Lisu alipoingilia kati.
Sasa kama hakuna nidhamu ya kujadili MADA husika basi pasiwe na ajenda bali iwe kama mkutano tu wa kisiasa.
 
Kweli lakini kwa mjadala wa jana ITV Masako alijitahidi sana kuzuia Ndugai ambaye mara nyingi alikuwa anakwenda nje ya mada kwa kuzungumzi mambo ya Mwembe yanga, simu na meseji walizotumiwa yeye na Makinda na alionekana kuwa na hasira mara kwa mara na kuwakatiza wenzake wanapoongea hasa anapoongea Lissu na ndio sababu kuu iliyokuwa inamtoa kwenye mada. Tundu alijaribu sana kukumbusha kuwa mjadala unahusu Kanuni za bunge lakini kama ruksa ya kutoka nje mada ipo basi kwake ni kazi ndogo sana!Kwa asilimia kubwa Masako alifanya kazi yake vizuri ila ni kazi kubwa sana kumthibiti mtu asiyekuwa na hoja au uelewa wa jambo linalojadiliwa kwani atajadili mambo mengine kwa jazba ili kuonesha kuwa anaonewa na hatimaye kuvuruga mjadala kama ilivyojitokeza jana kupitia ITV
 
Na kwa nini nyakati zote hizo mbili na wasimamizi tafauti chama kinacho shambuliwa ni chadema ? wao chadema hawana uwezo wa kujittetea, au wanamadudu mengi ?
 
Kweli lakini kwa mjadala wa jana ITV Masako alijitahidi sana kuzuia Ndugai ambaye mara nyingi alikuwa anakwenda nje ya mada kwa kuzungumzi mambo ya Mwembe yanga, simu na meseji walizotumiwa yeye na Makinda na alionekana kuwa na hasira mara kwa mara na kuwakatiza wenzake wanapoongea hasa anapoongea Lissu na ndio sababu kuu iliyokuwa inamtoa kwenye mada. Tundu alijaribu sana kukumbusha kuwa mjadala unahusu Kanuni za bunge lakini kama ruksa ya kutoka nje mada ipo basi kwake ni kazi ndogo sana!Kwa asilimia kubwa Masako alifanya kazi yake vizuri ila ni kazi kubwa sana kumthibiti mtu asiyekuwa na hoja au uelewa wa jambo linalojadiliwa kwani atajadili mambo mengine kwa jazba ili kuonesha kuwa anaonewa na hatimaye kuvuruga mjadala kama ilivyojitokeza jana kupitia ITV
Ok lakini baada ya kukumbushwa na mh Tundu Lisu. Halafu tumejionea wenyewe kuwa ikiwa kwenye mjadala tu Ndugai haheshimu wenzie waongeapo sasa akiwa kwenye kiti si ndio afanyavyo!
 
Nimekuwa nikibahatika kuona mijadala hasa kwenye televisions za Star(Startv) na ITV kuhusiana na mambo mbalimbali.
Kitu nilichogundua mpaka sasa ni kuwa kama patakuwa na mada inayohusisha vyama vya siasa mfano pawe na mwakilishi wa CCM, CHADEMA, CUF n.k. basi uongoza mjadala atazidiwa (sijui makusudi au ushabiki) na mmoja wa waalikwa kwa kwenda NJE kabisa na mada husika.
Niliona kwenye Startv wakati Yahya Mohamed akiongoza mjadala uliowahusisha mh Migulu Nchemba (CCM), mh Zito Kabwe (CHADEMA) na Julius Mtatilo (CUF). Wale wa CHADEMA na CUF walijikita HASWA kwenye mada lakini wa CCM yeye aliamua kuingiza ya kwake na kumshambulia Zito na chama chake huku Yahya akiangalia tuu bila ya kumkosoa.
Jana pia nilibahatika kuona mjadala kwenye ITV (Kipima Joto), muongozaji ni mtangazaji mahiri bwana Masako. Kwenye mjadala huo licha ya kuhusisha CCM (mh Ndugai) na CHADEMA (mh Lisu) pia palikuwa na waalikwa wawili toka asasi nyingine. Kama kawaida (hii naamini sasa) mh Ndugai akatoka kwenye mada husika na kuanza kumshambulia Lisu na chama chake bila hata bwana Masako kumkatiza mpaka pale mh Lisu alipoingilia kati.
Sasa kama hakuna nidhamu ya kujadili MADA husika basi pasiwe na ajenda bali iwe kama mkutano tu wa kisiasa.

Mhmm! Naamini huo ni mtazamo wako. Mbona wa CDM akitoka nje ya mada na kuzungumza kwa jazba, huwa mnasema CDM YAMGALAGAZA CCM? Yale yale yakifanywa na CDM mnasifia, yakifanywa na CCM mnaponda. Hajui mfanyalo. NI MTAZAMO TU
 
Na kwa nini nyakati zote hizo mbili na wasimamizi tafauti chama kinacho shambuliwa ni chadema ? wao chadema hawana uwezo wa kujittetea, au wanamadudu mengi ?

Duh! huyu mkongwe wa JF kumbe bado yupo humu!

aiseee! karibu tena mkuu uchangamshe baraza!
 
Nimekuwa nikibahatika kuona mijadala hasa kwenye televisions za Star(Startv) na ITV kuhusiana na mambo mbalimbali.
Kitu nilichogundua mpaka sasa ni kuwa kama patakuwa na mada inayohusisha vyama vya siasa mfano pawe na mwakilishi wa CCM, CHADEMA, CUF n.k. basi uongoza mjadala atazidiwa (sijui makusudi au ushabiki) na mmoja wa waalikwa kwa kwenda NJE kabisa na mada husika.
Niliona kwenye Startv wakati Yahya Mohamed akiongoza mjadala uliowahusisha mh Migulu Nchemba (CCM), mh Zito Kabwe (CHADEMA) na Julius Mtatilo (CUF). Wale wa CHADEMA na CUF walijikita HASWA kwenye mada lakini wa CCM yeye aliamua kuingiza ya kwake na kumshambulia Zito na chama chake huku Yahya akiangalia tuu bila ya kumkosoa.
Jana pia nilibahatika kuona mjadala kwenye ITV (Kipima Joto), muongozaji ni mtangazaji mahiri bwana Masako. Kwenye mjadala huo licha ya kuhusisha CCM (mh Ndugai) na CHADEMA (mh Lisu) pia palikuwa na waalikwa wawili toka asasi nyingine. Kama kawaida (hii naamini sasa) mh Ndugai akatoka kwenye mada husika na kuanza kumshambulia Lisu na chama chake bila hata bwana Masako kumkatiza mpaka pale mh Lisu alipoingilia kati.
Sasa kama hakuna nidhamu ya kujadili MADA husika basi pasiwe na ajenda bali iwe kama mkutano tu wa kisiasa.

CCM ni lazima watoke nje ya mada kwa sababu wakijikita kwenye mada watajikaanga bila mafuta!

ni kweli waendesha mada; baadhi yao mara nyingi wanashindwa kuwakemea watu wa CCM kwa woga na udhaifu wa kitaaluma; wanafikiri CCM bado inashika hatamu kwa hiyo watapoteza kibarua, none the less kukisha kucha kumekucha tu; watazuga mpaka watakwama;

Kama Ndugai jana alionyesha udhaifu wa hoja na haiba kiasi kwamba hata Masako bila kuingilia watanzania waliona kwamba anapwaya na kudhihirisha taswira ya udhaifu wa uongozi mzima wa bunge la jamhuri
 
Na kwa nini nyakati zote hizo mbili na wasimamizi tafauti chama kinacho shambuliwa ni chadema ? wao chadema hawana uwezo wa kujittetea, au wanamadudu mengi ?
Mie sio mwanasiasa ila kwa mfano mjadala wa ITV ulihusu KANUNI ZA BUNGE lakini mh Ndugai akatupeleka Mwambe Yanga walipofanya mkutano CHADEMA, kwa busara za waalikwa wengine walimkumbusha Masako kurejea kwenye mada!!!!!!!!!!
 
Suala la waendesha mijadala ktk tv au redio liko mtambuka kiasi,wakati mwingine ushabiki na kwingine ni kukosa udhaifu kama ulivyosema.Nakumbuka wakati wa sakata la sensa huyohuyo Masako aliendesha kipindi juu ya suala la waislamu kupinga kuhesabiwa.Ktk kuchangia mtazamaji m1 akapiga simu akamuuliza kwa nini hakuwaalika viongozi wa waislamu wanaoongoza vuguvugu la kutohesabiwa tukasikia utetezi wao? Masako akajibu "tutawapataje wenyewe ni kama wahuni tu hawajulikani wapi wanaishi au ofisi zao!" Jbu lile lilinishangaza maana siku chache tu nilisikia Rais alikutana nao kutafuta ufumbuzi wa suala lile,sasa mtangazaji anadai eti ni wahuni fulani ambao hawezi kuwapata! Je,Rais anaweza kuwapata wahuni lakini kituo cha tv/mtangazaji asiwapate? Ni kweli wahuni wanawezaje kuisumbua serikali kiasi kile?....nilipata shida juu ya uwezo wa mzee yule kuendesha mjadala ule ambao uliegemea upande m1. mifano ni mingi kuhusu waendesha mijadala na uwezo wao ulivyo dhaifu....
 
Back
Top Bottom