Wanne wafariki katika ajali ya basi Tabora

Kadhakan

Senior Member
Joined
Jul 20, 2026
Posts
115
Reaction score
175
Watu wanne, wakiwemo Watoto wawili wamefariki dunia baada ya basi la Kampuni ya Miza Express lililokuwa likitoka Mpanda kuelekea Bariadi kupata ajali katika eneo la Kijiji cha Ngukumo, Wilaya ya Nzega Mkoani Tabora.

Ajali hiyo imetokea majira ya saa 9 usiku, baada ya basi hilo kuacha njia na kutumbukia bondeni, kilomita chache kabla ya kufika Makao Makuu ya Wilaya ya Nzega.

Baadhi ya Abiria walijeruhiwa na kukimbizwa katika Hospitali ya Wilaya ya Nzega kwa ajili ya matibabu, huku wengine waliokuwa wamenasa ndani ya basi wakilazimika kuokolewa na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kwa kushirikiana na Polisi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, ACP Twawa Juma Lulengelule amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema waliofariki ni Wanaume watatu na Mwanamke mmoja.

Amesema uchunguzi wa awali umebaini kuwa chanzo cha ajali hiyo ni Dereva kukosa umakini na kushindwa kulimudu basi, ambalo lilitoka nje ya barabara, kugonga vyuma vya kingo za barabara na kisha kupinduka na kutumbukia bondeni.

 
Hicho kipande (Puge-Nzega Mjini) kipo lonely mno hata upite mchana,itakuwa ni uzembe au ubovu wa chombo tu.
 
Kabila gani wanaishi huko wamefyeka miti na kuiacha nchi uchi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…