cheusimangala
JF-Expert Member
- Feb 27, 2010
- 2,585
- 500
Hehehe ahsante CM
Uko sahihi kwa kiasi kikubwa. . .Na mawazo yako hayako mbali sana na yangu ila wanaume wanaochukia wanaune wenzao kwakua tu wanaume waliofanikiwa kwa hili au lile ni wachache sana. Ni rare sana kukuta mwanaume amekaa chini anamsema mwanaume mwenzie kama wanawake. Yani maneno kama "muone anavyoringa na huyo bwanake. . .angejua sio wake mwenyewe mbona angejibeba" sio maneno yaliyozoeleka kwenye makundi ya wanaume. Wao ni mwendo wa "demu wa fulani mkali kweli. . .Au hajatulia" ila hawahangaiki kumkashifu huyo fulani hata kama wanatamani wangekuwepo kwenye nafasi yake.
Yani hata hako kachuki kakiwepo hakaonyeshwi kwa matendo. Kama ni huduma itatolewa, maongezi yatakuwepo na vicheko juu. Sio mtu ghafla anavuta mdomo kuleeee. . .utadhani unachangia matatizo binafsi aliyonayo.
Kuhusu kuhisi "kuchukiwa" huko nako kupo kwa kiasi fulani. Ni kama wale wanaohisi kuonewa. . .hua siku zote wanaonewa, ila sio wengi wenye hulka hiyo.
Unaona sasa...Ngabu Sr. na siasa ni kama maji na mafuta! Hapo tu tayari unanionyesha kwamba umeingia choo cha kike. Rudi ujipange upya!
Ukipatia nakupa dola 100.
Yani mm sijui nisemeje wanawake hatupendani kabisa, mm imeshanitokea nilienda crdb bank
nikamuomba dada mmoja ambae anafanya kazi pale anipatie deposit slip zilikuwa zimeisha jamani alinijibu vibaya
kwa kweli nilijisikia vibaya sana nikasema hii ni slip tu naomba, ingekuwa ni kitu cha kunielekeza kweli angenielekeza?
hatupendani hata kidogo niwa chache sana ambao kweli hatupo hivyo.
endeleza ubishi, naona mpaka nianze kukutajia orodha ya ....wako wa enzi hizo ndio utaamini
Unaona sasa...Ngabu Sr. na siasa ni kama maji na mafuta! Hapo tu tayari unanionyesha kwamba umeingia choo cha kike. Rudi ujipange upya!
Ukipatia nakupa dola 100.
Sio ubishi...ni fact kuwa Sr. na siasa hawaendani kabisa na hilo jengo ulilolitaja hakuwahi kabisa kuwa na ofisi humo.
unajua naongelea jengo gani wewe?
Si ulisema la siasa? Nilijualo mimi ni lile la Political Science
sio hilo, kwani huko ndiko ulikokuwa unapanda kule juu kuchungulia chini?
Halafu mbona umenichunia kule fesbuk? Hujaona request yangu?
CM bado mwenyewe marafiki zangu wengi ni wa kiume. . .Hawana majungu wala kugeukana hata mkifikia kutoelewana tofauti na wanawake. Kwa wanawake chuki na kukomoana ni vitu ambavyo vina nafasi kubwa sana tofauti na wanaume.ni kweli lugha zetu zimetofautiana lkn kitu ni kile kile.Labda ww uhang sana na wanaume lkn wanaume wenye wivu,roho ya kwa nini na majungu wamejaa tele.Kinachofanya sisi tuonekana haka katabia ni ketu ni sbb sisi wanawake tuko wengi kuliko wao hivyo ni rahisi hii tabia kuonekana kwa wingi kwetu zaidi yao na sbb nyingine ni kwamba sisi tumejaliwa maneno mengi hivyo mahali pakiwa na wivu tu hautajificha sbb ya maneno na vijembe vyetu na makelele mengi, mtu akiuliza nini tatizo hakuna sbb ya maana atakayopata zaidi ya huyu ana nyodo huyu ananionea wivu.
Narudia tena kusema tofauti yetu na wanaume ni ktk lugha tu wkt sisi tukioneana wivu tutasema "anaringa angejua huyo bwana ana mwanamke kila kona" wanaume wao wanasema"jamaa limbukeni kweli tokea apate shori mkali hata hatoi hi kwa washikaji maskani".Pia sisi kitu kidogo tunakivalia sana njuga kuliko wanaume ndo mana sisi tunaonekana sana kuliko wao ktk hili.
Pia nataka kuongezea kwenye kuhisi kuchukiwa.Unakuta mtu kafanikiwa,nyie wala hamumuonei wivu lkn kumbe yeye rohon mwake anahisi kawivu kanawamaliza,yeye mwenyewe sbb anadhani mnamuonea wivu anaanza vitu vya ajabu,mfano anaweza kuanza kutoa vijembe kama....kama ipo ipo tu,mwenye wivu ajinyonge...bahati ya mwenzio usiilalie mlango wazi..na pia anaweza yeye mwenyewe akawakatia mawasiliano.Nyie mnaopigwa vijembe mtaona yeye aliyefanikiwa anawafanyia nyodo,lazima mtajisikia vibaya na ni vigumu kumuombea mema na hata akiporomoka mtamcheka na kufurahia sbb nani anapenda kuona maendeleo ya mtu mwenye dharau na nyodo?
Mim naomba tu ujiulize,je ni kweli kwamba sisi wanawake tukiwa na maendeleo kushinda waume au boyfriend zetu lazima tu tutawadharau?
Kama utajibu hapana,sio wote ni baadhi ,basi jiulize kwa nini wanaume kwa kiasi kikubwa sana huwa hawafurahii
mwanamke awe na kipato kikubwa kumshinda yeye kama sio wivu?
Kama ni wivu jiulize kauli hizi umezisikia kwa wingi kiasi gani.
lol,kule fb nachangia kwa nadra - karibu twitter.
ps. kwa nini ulifanya fujo ktk ile pati ya kileleni?
Unaona sasa...yaani mimi na pati ni kama usiku na mchana. Niko low-key sana. Ndiyo maana nasema rudi ujipange upya! Umeingia choo cha kike.
jitahidi kuchomoka ila haisaidii, kesho nitaku-pm listi yako
Ndiyo. Hujaiona kwani?
Halafu leo nimekugongea kaa tano hivi.
kuna siku ulinipa like nikashangaa imeyeyuka!
Daaah...hivyo vyanzo vyako vimekupotosha!
sitegemei sana vyanzo, nilichokuwa nahitaji kutoka kwao ni pa kuanzia mengine yote nayajua toka zamani maana nawajua watu wote waliosoma vidudu na shebe (dk,smf,kmf,km,kr et al.) pamoja na wasure/mamazeri wao wote.
Daaah...hivyo vyanzo vyako vimekupotosha!
halafu ukiendeleza ubishi usio na tija nitakuwa sikupi updates mpya kuhusu nw!