Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,437
- 5,235
Wanawake wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) leo Jumamosi Agosti 9, 2025 wamekutana katika kongamano maalumu lililofanyika kwenye viwanja vya Tabata Shule, jimbo la Segerea mkoani Dar es Salaam.
Tukio hilo limeandaliwa na aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalum kupitia CHADEMA, Agnesta Kaiza, ambaye kwa sasa amejiunga na CHAUMMA na ametangaza rasmi kutia nia ya kugombea ubunge wa Segerea kupitia chama hicho.
Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Mgeni rasmi katika kongamano hilo ni Devotha Minja ambaye ni mgombea mwenza wa Urais wa Tanzania kupitia CHAUMMA, ambaye alipata nafasi ya kuzungumza na washiriki na kuwatia moyo katika harakati za kisiasa na kijamii. Kongamano hilo lilipambwa na matukio mbalimbali ya picha, yakionesha mshikamano na matumaini ya wanawake wa Segerea.
Tukio hilo limeandaliwa na aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalum kupitia CHADEMA, Agnesta Kaiza, ambaye kwa sasa amejiunga na CHAUMMA na ametangaza rasmi kutia nia ya kugombea ubunge wa Segerea kupitia chama hicho.
Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Mgeni rasmi katika kongamano hilo ni Devotha Minja ambaye ni mgombea mwenza wa Urais wa Tanzania kupitia CHAUMMA, ambaye alipata nafasi ya kuzungumza na washiriki na kuwatia moyo katika harakati za kisiasa na kijamii. Kongamano hilo lilipambwa na matukio mbalimbali ya picha, yakionesha mshikamano na matumaini ya wanawake wa Segerea.