Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,811
- 15,403
Nimechoshwa na aina ya vyakula unavyopika humu ndani, sasa hiki ni kitu gani.......!
Inawezekana chakula kikawa na kasoro ndogo tu ya kawaida ambayo siku za nyuma alikuwa wala haisemi mpaka wewe mwenyewe umweleze kuwa chakula leo kimezidi chumvi kidogo au kina kasoro fulani, na yeye kwa upendo anakujibu tu kwamba siku hazilingani na maisha yanaendelea.
Lakini inatokea ghafla tu mumeo au mpenzi wako anaanza kukosoa chakula chako kwa njia yenye kukera. Tabia hiyo siyo ya siku moja, inakuwa ndio tabia yake. Karibu kila siku haridhishwi na aina ya vyakula unavyompikia.Nawaomba wanawake wanipe uzoefu wao katika jambo hili........
Je utafanyaje iwapo utakutana na kisirani hiki.......................?