Wanawake msikurupuke kutukana watu wakipiga simu

Wanawake msikurupuke kutukana watu wakipiga simu

NIMPENDENANI

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2014
Posts
6,114
Reaction score
5,397
Habari zenu wanna MMU,

Jana mchana nilikwenda shopping kununua vitu vidogo, wakati niko kwenye car park nikaona mfuko nakini ulikua wazi na ndani kuna simu, wallet cheque ambayo imesha sainiwa na karatasi nyengine. Nikazichukua kufika nyumbani nikasema nitaangalia ili nimpigie mwenyewe, nikajisahau mpaka saa 12 jioni ndio nikakumbuka nikasema wacha niangalie kama kuna number naweza kuipata manake simu ilikua off, sikupata number option nilokua nayo nikuweka simu kwenye charge.

Haya nikaiweka nikaendelea na homework za watoto narudi kuangalia simu naona sms na missed call kibao kwenye screen simu imefungwa na Passward. Nikasema wacha nisubiri atapiga ili nipokee kweli hata 5min bado kapiga mtu nikapokea ile kusema hallow yanianza matusi kupitiliza mwanamke anatukana utadhani hana hana wazazi nikamuacha achambe alipo maliza ananambia changudoa mwenzio.

Ananizingua mimi eti simu na pesa ametupa anadhani mimi sasa kwa taarifa yako mimi nimeathirika na wewe pia umeathirika usione hela anazokupa ukajua mzima anavirusi akanikatia simu niliacha uchungu nilipo sikia huko kuathirika.

Baada ya kama mda wa 30min akapiga jamaa nikapokea akaniomba msamaha nikamwambia aje asubuhi kazini kuchukua mzigo wake na kweli amefika nikampa ameomba msamaha sana, nikajiuliza ivi wanawake wengine wanakua sababu ni shule ndogo au tabia za ajabu wanatoka nazo makwao yani yule mwanamke ni wale kigodoro type.
 
Inawezekana amepita shule, literally. Attended school, not the books. Wapo wengi sana.
 
Hahahah umenikumbusha zamani nilikuwa nina hasira mtu apokee simu sio yake.

Basi bwana mwenye simu na aliyepokea simu majina yanafanana halafu ni ndugu, sasa sauti ya muhusika naifahamu, namwambia namtaka fulani (nataja jina), ananiambia ndio mimi, kila nikisema sio wewe yeye anabisha, "nilishusha mafuriko ya maneno mabaya" hakutegemea nikamwambia kama kakutuma uchezee akili yangu siku nyingine hutarudia.

Duuuh huu ndio ulikuwa mwisho wa kuongea hovyo kwenye simu, maana nikaitwa kutambulishwa yule nilomtukana, nilitambulishwa vizuri utapenda,"kaka fulani huyu ndo fulani mke wangu mtarajiwa"(hapo nyumbani washapeleka posa washapangiwa mahari ndo wanajipanga wapeleke), nae akajibu, "anhaaa, nashukuru kukufahamu, lakini si ndio huyu ulozaa nae" akajibu ndio basi kaka yake akamalizia, "kama ndio huyu nafurahi sana maana nilishasikia sifa zake kabla, anafaa"

Mimi macho chini pale nikaanza tena kuomba samahani, nashukuru alikuwa muelewa akanisamehe na hakuna aliyejua zaidi ya sisi watatu, ila nilijifunza sana siku ile(huyu ndugu yake alikuwa anaishi mbali hivyo sikuwa namfahamu kabla na jina nilishatajiwa ila nilisahau). Sitarudia teeeeenaaaaaaaa
 
Back
Top Bottom