Hivi kweli kina baba mimba mnaona rahisi sana kubeba? Mnafikiri kumejaa hewa humo ndani?
Binafsi nimetoka kujifungua wiki 10 zilizopita na bado sija recover fully ukizingatia mtoto alikuwa size ya wastani, na labour haikuwa ndefu sana.
Imagine unaombwa chakula cha usiku halafu una conditions hizi:
-miguu imevimba
-ingawa unaenda haja ndogo kila dakika 30 unasikia kama vile 90% ya kibofu bado kimejee WITH NO RELIEF WHATSOEVER
-unasikia kama vile kichwa cha mtoto kimeegemea kibofu
-mwili wote unauma huwezi kulalia mgongo wala ubavu, unaona nafuu ukikaa wima kwenye kochi angalau uweze kupata kausingizi
Kumbuka kwamba viungo vyako vyote vinasukumizwa kuenda juu na kubanana ili kuachia nafasi mimba ikue, kwahiyo kupumua nako ni shida. Hii ni list ya vitu kadhaa nilivoexperience, lakini najua wengine wanakuwaga na kichefuchefu na dalili zingine pia. Sasa niambie, hiyo hamu, au hata tuseme uwezo wa kufanya tendo la ndoa itatoka wapi??
Sasa, baada ya kujifungua, kumbuka hata mtoto akitoka njia ya kawaida lazima pachanike. Degree ya kuchanika inaanza from 1st to 4th degree. Mimi nilipata 1st degree (thank goodness!) ambayo haikuhitaji kushonwa. 2nd degree mpaka 4th lazima kushonwa. Kukupa mfano, 3-4th degree unaweza ukachanika kuanzia kwenye vagina mpaka nyuma (rectum). IMAGINE THAT! If you want to have nightmares, simply search "vaginal tearing" kwenye google images. You will want to hug your mother and apologize over and over.
One more thing, wengine inabidi wafanyiwe episiotomy ambayo ni wakati daktari anakata njia ya uzazi ili kupanua njia ya mtoto kupita na kuzuia kuchanika vibaya. Kumbuka wengine wakishonwa vibaya hili huleta tatizo pia.
Ukija kwenye upasuaji, do I even have to explain? Hicho ni kidonda. Mpaka kije kupona itachukua miezi.
Kama unavyoona, kutunga mimba ni raha, kuzaa ni shida, na kulea ni kazi nyingine zaidi. Hakuna muda muafaka wa kuacha kufanya mapenzi, yote inategemea na mama watoto. Kama hajisikii au hawezi, heshimu hilo na enjoy your time together alone (kama ni mtoto wa kwanza) because you will never have this precious time together every again.
Kuanza tena kufanya mapenzi inategemeana, lakini usitegemee kupata kitu baada ya siku chache. Tunakuwa tumechoka mentally na physically tunakuwa tunarecover.
My advice, take care of her so she can take care of your baby and eventually take very good care of you. Maisha ya ndoa si mchezo and not all about sex!!!!!