Wanawake mnatuchukuliaje wanaume?

Wanawake mnatuchukuliaje wanaume?

Unajua tatizo wanaume na sisi tumekuwa cheap saaana siku hizi. Kama demu humjui piga kimywa hata kama kakuvutia kiasi gani. Ikitokea tatizo msaidie kama lipo ndani ya uwezo wako. Ikitokea mkakutana tena yeye ndio ataomba mawasiliano yako. Hii inaleta heshima na kuondoa dharau toka kwa hawa viumbe ambao wengi wao wanaishi kwa nguvu za kiungo kilichopo katikati ya mapaja yao.

ni kweli mkuu hapo umenena.
 
Suala la namba lenyewe hapana, siwezi kutoa namba tu kama sikufahamu vizuri, mtu unaweza kuwa unaongea nae kila siku na mna heshimiana sana lakini bado huwezi juu anawaza nini juu yako, kwa kweli suala la namba hapana lazima uwe makini. hilo suala la kusalimiana na mtu mwenyewe tu, mi ukinisalimia nakujibu na stori tunatwanga - ila kuniomba namba ya simu ni kosa kubwa.

unaonekana unajielewa kuliko wale ambao ukimsalimia kukujibu kazi ukimuongelesha anahisi unataka kumtongoza yani ni shida tupu.
 
mimi sasa nakuja kivingine, wanaume sijui tuwaelewe vipi. Wanawake wakiwa wanatoa namba ovyo wanawaita malaya, wakiwa serious na who to give their mob numbers mnawashangaa.

Sasa nikuulize mkuu mtoa mada, hivi wanawake wangekuwa wanatoa namba kwa kila wanaemkuta hiyo space ya kuweka namba ingetoshea?? "Sometimes people don't know what they need in their lifetime"

FIKIRIA NA UCHUKUA HATUA.

sawa nimekuelewa ila inakuaje mtu akufikirie mambo mengine kabisa wakati unamuom?
 
hahah mkuu wamesha kugundua wakuchangamkie kwa salam af upate mwanya wa kuomb namba wakat ckujui hunijui tumekutan kwenye ice tu, pil wengne wana mawazo meng uwaache hvyo hujua nn kinamsib katk akil yake watu wanatembea ila mawazo, mipango meng utajumiz akil yako kisa salamu na namba ya cm bure.

sawa nimeelewa.
 
Na hiyo ndio sababu inayopelekea wanawake wa siku hizi kuchelewa kuolewa maana wao huhisi kila mtu ni muhuni, sasa we utajuaje kama huyu ni mwema au mbaya bila ya kumpa nafasi na uone mwelekeo wake??

afadhali umenisaidia kuuliza mkuu
 
kumbuka MUNGU alimuumba mwanamke kutoka ubavuni kwetu so lazima watakuwa dhaifu mbele ya mwanamke
same applied about their thoughts
 
Mi huwa nawashangaa sana wanawake/ wasichana, mara sijui huwa wanatuchukuliaje. Kwasababu, utakuta unazungumza na dada mnayeheshimiana sana lakini ukitaka heshima ipungue basi mwambie naomba namba ya simu.

Ataanza kuhisi unamtaka labda unataka kumtongoza, sasa sijui ni kwanini kwani wakati huenda hata usiwe na nia hiyo anayokufikiria lakini utashangaa anakupa visababu, au atakupa lakini kwa wasiwasi sana. Sasa mi najiuliza hawa viumbe huwa wanatuchukulia sisi ni watu wa aina gani? Au ndo wanahisi tunawaza ngono muda wote?

Tena wakati mwingine utakuta upo kwenye daladala umekaa na dada fulani siti zinazofanana lakini hakusalimii, ila sasa kitendo cha weye kumsalimia tu kwanza atakujibu kwa sauti ya chini sana kama unataka unataka kumtongoza.

Hivi kwanini nyie watu mko hivi kila mtu unam-treate kama vile anakutaka, kwanini?

sasa unamwomba namba ili iweje? mwache tu.
wanawake ndio walivyo halafu wanaume nasi unakuta tunawapapalikia sana wanawake,,, huo ni udhaifu, , mi mtu really sijawahi omba namba kwa msichana yeyote labda ye ndio aombe napo sio lazima apate,, maana kama ni maongezi ya kawaida tutaongea kukikutana face to face au kwa njia nyingine. . . sio eti ninwombe namba kwa ajili ya kuchati tu.
 
sasa unamwomba namba ili iweje? mwache tu.
wanawake ndio walivyo halafu wanaume nasi unakuta tunawapapalikia sana wanawake,,, huo ni udhaifu, , mi mtu really sijawahi omba namba kwa msichana yeyote labda ye ndio aombe napo sio lazima apate,, maana kama ni maongezi ya kawaida tutaongea kukikutana face to face au kwa njia nyingine. . . sio eti ninwombe namba kwa ajili ya kuchati tu.

ni kweli kaka labda si ndo huwa tunawapapatikia sana hawa viumbe, ndo mana huwa wanatuhisi ivo.
 
Back
Top Bottom