Wanawake mnatuchukuliaje wanaume?

Wanawake mnatuchukuliaje wanaume?

Joel360

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2013
Posts
986
Reaction score
657
Mi huwa nawashangaa sana wanawake/ wasichana, mara sijui huwa wanatuchukuliaje. Kwasababu, utakuta unazungumza na dada mnayeheshimiana sana lakini ukitaka heshima ipungue basi mwambie naomba namba ya simu.

Ataanza kuhisi unamtaka labda unataka kumtongoza, sasa sijui ni kwanini kwani wakati huenda hata usiwe na nia hiyo anayokufikiria lakini utashangaa anakupa visababu, au atakupa lakini kwa wasiwasi sana. Sasa mi najiuliza hawa viumbe huwa wanatuchukulia sisi ni watu wa aina gani? Au ndo wanahisi tunawaza ngono muda wote?

Tena wakati mwingine utakuta upo kwenye daladala umekaa na dada fulani siti zinazofanana lakini hakusalimii, ila sasa kitendo cha weye kumsalimia tu kwanza atakujibu kwa sauti ya chini sana kama unataka unataka kumtongoza.

Hivi kwanini nyie watu mko hivi kila mtu unam-treate kama vile anakutaka, kwanini?
 
Ukiomba number mzee unasema na nia yako ya kufanya hivyo. Kuhusu kusalimia, utajua tu anayetaka salamu yako na asiyetaka pia. Kama una nia nzuri na mtu haelewi, fine...their loss.
 
Ukiomba number mzee unasema na nia yako ya kufanya hivyo. Kuhusu kusalimia, utajua tu anayetaka salamu yako na asiyetaka pia. Kama una nia nzuri na mtu haelewi, fine...their loss.

Wakati mwingine unasema fresh mkuu,.. 'bwana naomba namba yako ili ishu flani ikitokea tuwasiliane' lakini mtu atakuletea visababu vya kukataa kibao.
 
mmmjh

mkuuu kwa mfano hunijui,hatuna biashara yoyote,unaomba namba yangu itakua ya nini zaidi ya kunitongoza?
 
Mkuu mdada umekutana nae kwenye dala dala, namba yake ya nini tena? Dunia imebadilika, usalama wake muhimu, ndio maana wanakataa kutoa namba, maana km sio wizi basi ngono inahusika hapo, waombe namba wadada mnaojuana.
 
Wee kwenye daladala unataka nikupe namba ya kazi gani? huo msaada nimetangazia daladala nina matatizo??....nia nzuri nia gani na mtu humjui hakujui???
 
hivi unajua thamani ya namba ya simu ya mtu. au unadhani ni kuchukua tu. nyie ndiyo mnatoa namba zenu bila kujua athari zake. wadada komaeni hivyo hivyo.


nenda facebook na ukirudi shuleni chukua za wanafunzi wenzako zitakutosha maana shuleni kwenu kuna wanafunzi 300 wa kike
 
Mengine ni kama tunayatafuta wenyewe hivi umri huu huwezi ona dalili za mtu anayetaka kuwa karibu na wewe kweli??!!!!

Anayetaka kuwa karibu na wewe namba zinatoka zenyewe wakati wa kuagana
 
mmmjh

mkuuu kwa mfano hunijui,hatuna biashara yoyote,unaomba namba yangu itakua ya nini zaidi ya kunitongoza?

kujuana si ndipo kunapoanzia hapo?
na wakati mwingine mtu atahitaji mjuane kwa sababu nzuri tu mbali na kutaka kuanzisha uhusiano wa mapenzi au unasemaje?
 
Mkuu mdada umekutana nae kwenye dala dala, namba yake ya nini tena? Dunia imebadilika, usalama wake muhimu, ndio maana wanakataa kutoa namba, maana km sio wizi basi ngono inahusika hapo, waombe namba wadada mnaojuana.

ila kwenye daladala mara nyingi inakuwa si kuomba namba namba hata ile salamu atakujibu kwa shida sana kama unamlazimisha
 
Wee kwenye daladala unataka nikupe namba ya kazi gani? huo msaada nimetangazia daladala nina matatizo??....nia nzuri nia gani na mtu humjui hakujui???

kwennye daladala sijazungumzia namba, kwenye daladala nimezungumzia jinsi nyie mlivyowazito kutoa hata salamu
 
hivi unajua thamani ya namba ya simu ya mtu. au unadhani ni kuchukua tu. nyie ndiyo mnatoa namba zenu bila kujua athari zake. wadada komaeni hivyo hivyo.


nenda facebook na ukirudi shuleni chukua za wanafunzi wenzako zitakutosha maana shuleni kwenu kuna wanafunzi 300 wa kike

nani alikwambia mimi ni mwanafunzi?
 
Unajua tatizo wanaume na sisi tumekuwa cheap saaana siku hizi. Kama demu humjui piga kimywa hata kama kakuvutia kiasi gani. Ikitokea tatizo msaidie kama lipo ndani ya uwezo wako. Ikitokea mkakutana tena yeye ndio ataomba mawasiliano yako. Hii inaleta heshima na kuondoa dharau toka kwa hawa viumbe ambao wengi wao wanaishi kwa nguvu za kiungo kilichopo katikati ya mapaja yao.
 
Suala la namba lenyewe hapana, siwezi kutoa namba tu kama sikufahamu vizuri, mtu unaweza kuwa unaongea nae kila siku na mna heshimiana sana lakini bado huwezi juu anawaza nini juu yako, kwa kweli suala la namba hapana lazima uwe makini. hilo suala la kusalimiana na mtu mwenyewe tu, mi ukinisalimia nakujibu na stori tunatwanga - ila kuniomba namba ya simu ni kosa kubwa.
 
Back
Top Bottom