Uta Uta
JF-Expert Member
- Feb 2, 2016
- 3,740
- 8,765
Wanawake ni viumbe muhimu sana hapa duniani. Umuhimu wao upo ktk nyanja mbali mbali kwanza wao ndio mama zetu waliotuzaa, pili wao ndio wake zetu na pia wao ndio wenye uwezo wa kipekee wa kutuondelea msongo wa mawazo na maisha pia.
Mi nawaheshimu sana wanawake na ikitokea mtu amewasema vibaya huwa nahuzunika sana. Ila leo na mimi nainua mkono kwa hii dosari ndogo ninayoiona mara kwa mara. Mnapokuwa ktk daladala huwa hamuwatendei vizuri wanawake wenzenu, utakuta amepanda mama ana mtoto mgongoni au anatumbo kubwa amesimama na wanawake mliobaki hamna watoto wala nn ila mnawaacha wenzenu wamesima na watoto mgongoni au na tumbo (mimba) kubwa na ninyi bila kujali.
Mara zote nawaona wanaume ndio wakijali hali hizi. Kinachonishangaza ninyi mnaujua vizuri uchungu wa kusimama na mtoto au mimba kwa mda mrefu kuliko wanaume. Lakini kwa nn eneo hili mnakosa huruma? Au mpaka ianzishwe taasisi ya kutetea wamama vijacho na wanaonyonyesha?
Naomba nyie muwe mfano wa kuwasaidia wanawake wenzenu. Na mwisho nawapongeza sana wanaume kwa kuwa na huruma ktk eneo hili naomba muendelee na moyo huo.
Asanteni nawasilisha
Mi nawaheshimu sana wanawake na ikitokea mtu amewasema vibaya huwa nahuzunika sana. Ila leo na mimi nainua mkono kwa hii dosari ndogo ninayoiona mara kwa mara. Mnapokuwa ktk daladala huwa hamuwatendei vizuri wanawake wenzenu, utakuta amepanda mama ana mtoto mgongoni au anatumbo kubwa amesimama na wanawake mliobaki hamna watoto wala nn ila mnawaacha wenzenu wamesima na watoto mgongoni au na tumbo (mimba) kubwa na ninyi bila kujali.
Mara zote nawaona wanaume ndio wakijali hali hizi. Kinachonishangaza ninyi mnaujua vizuri uchungu wa kusimama na mtoto au mimba kwa mda mrefu kuliko wanaume. Lakini kwa nn eneo hili mnakosa huruma? Au mpaka ianzishwe taasisi ya kutetea wamama vijacho na wanaonyonyesha?
Naomba nyie muwe mfano wa kuwasaidia wanawake wenzenu. Na mwisho nawapongeza sana wanaume kwa kuwa na huruma ktk eneo hili naomba muendelee na moyo huo.
Asanteni nawasilisha