Wanawake kuweni makini

Wanawake kuweni makini

A.R.M

Member
Joined
Oct 6, 2012
Posts
89
Reaction score
21
Jamani wanawake kuweni wastaarabu. Kama mwanaume ajajaliwa kuwa na kipato kinachokutosha na wewe umejaliwa kupata pesa nyingi kuliko yeye usitumie kigezo hicho kumnyanyasa kwa maneno au mitandaoni kama alivyofanya "super women" nimepata jibu kwa nini wazee wetu walikuwa hawataki mwanamke kuwa na kipato! Bora kuwa na golikipa anaekuheshimu ataishi kwa kuridhika na kipato chako kuliko hawa wanaotafuta pesa akikuzidi kidogo tu anaanza kukuona huna bidii yoyote ya kutafuta.
 
...nimepata jibu kwa nini wazee wetu walikuwa hawataki mwanamke kuwa na kipato! Kama mwaka huu 2018 unaaamini akili za pre colonial african societies za huko 1850s, basi mkuu una shida kubwa!
 
We tafuta pesa tu, si kila siku mnatusisitiza tutafute pesa, kumbe lengo lenu lilikuwa ili tuwalee!!!
 
Ila kwa kweli mwanamke akiwa na hela kumzidi mwanaume basi jamii inayowazunguka ni lazima itajua tu kwamba mume ni tegemezi, na kingine mimi sishauri mwanaume aoe mwanamke ambaye yupo vizuri kimapato kuliko yeye, ni heri upambane na hali yako ya uchumi mpaka ikae sawa ndiyo mchukue bibie umeweke ndani, maana sauti ya mwanaume ndani ya nyumba huendana na mfukoni kukoje yani kwenye kutoa maamuzi,
 
Ninao mfano hai kuna jamaa ni rafiki yangu kazini, basi kila siku huwa analalamika vimbwanga vya bibie, binti yupo vizuri kwao ni watu wanajiweza so mzee wake kamsaidia binti yake kiuchumi so demu yupo vizuri na pia ana kazi , so jamaa na mke wake ni mvutano ndani ya ndoa kila siku, sasa jamaa kaletewa proposal wajenge jamaa anataka wajenge nyumba ya design fulani hivi ni nzuri ila demu hataki anataka idea yake ifuatwe ni matatizo... Mwanamke akiwa vizuri ndani ya nyumba tegemea kutofautiana na mwenzako mara kwa mara
 
Usilalamike, we tafuta pesa alafu mengine yatajileta yenyewe
 
Usiombe ukadhaulika kwa mke mpaka kwa mama mkwe....
Kweli hela inaongeza heshima
 
Back
Top Bottom