Mleta uzi wewe Ni mwanaume sina shaka kabisa na hili. Jibu maswali haya
1. Ni lini umemnunulia taulo (towel) baba yako ?
2. Ni lini umenunulia sofa set baba yako
3. Ni lini umemnunulia boxers au nguo za ndani baba yako?
4. Ni lini umenunulia sandals baba yako?
5. Ni lini umemnulia vest baba yako?
6. Ni lini umenunua mapazia Kwa ajili ya madirisha na milango kule nyumbani kwenu?
7. Ni lini umeenda kwenu likizo ukakaa angalau siku 7 na kutoa matumizi kila asubuhi au kufanya shopping ya nguvu Kama hakuna msiba wala ugonjwa Ni likizo tu?
8. Ni lini umeingia dukani kununua vyombo Kwa ajili ya kupeleka nyumbani kwenu?
9. Ni lini umewahi kuwahudumia wazazi wako Kwa miezi miwili mfululizo?
10. Ni lini umewahi kuwabadilishia Kitanda na godoro wazazi wako?
Kama wazazi wako wapo hai hayo kumi tu kati ya mengi ambayo mwanamke anayafanya. Kwa taarifa yako mwanamke ana majukumu hadi Kwa mama mkwe wake yaani mama yako wewe sasa wewe endelea kujiuliza pesa za mwanamke zinapoenda wakati wewe pesa zako zinatoka bank zinaelekea Kwenye matumizi yako binafsi zaidi.
Wanaume nyie hayo hamuyafanyi na uwezo mnao kabisa sijui pesa zenu zinaishia wapi na nyie?