Karucee
JF-Expert Member
- Mar 11, 2012
- 18,179
- 34,431
Mie bwana, nimejilalia na dogo wangu. Simu inaingia. Namba naifahamu na nimeisevu jina. Ni mwanaume nilikuwa nasoma nae ITA na yeye kikazi yupo TRA HQ. Tangu nimemaliza chuo 2011 mawasiliano na wanafunzi wote yamepungua except mmoja ama wawili, na huyu X si mmoja wao. Nimepokea, anaeongea ni mwanamke. Hamna salamu. Wewe ni nani kwa X? Nikamwambia WTF? Akanijibu kwa ukali, nimekuliza X ni nani wako, manake ameniambia wewe ni nyumba dogo yake. Nikamuuliza woman are you serious. I was very offended. Am a married woman for crying out loud, tena niwe nyumba dogo?? WTF?? Nikamwambia mimi nina mume wangu na mtoto. Haya yote yametokana na nini? Akajibu ooh nimekuta message kwenye draft items ameandika nasafiri karibuni baby. Nikamwambia namheshimu sana huyo kaka. Nimesoma nae na ni mtu mstaarabu sana so siku ingine kabla hujakurupuka get your facts right . Akabaki oooh mi ni mafia nitakufanyizia kuwa mwangalifu. Nikamjibu do your worst. Hivi iweje unakuta message kwenye draft kwenye simu ya mwenzio, unakurupuka tuuu. Ingekuwa inbox nimetuma mimi kweli, ama at least ingekuwa kwenye sent items kweli, draft?? Halafu sina hata regular communication na yeye? Utawapigia wangapi? Kama sio kutafuta kufa na pressure.