Wanaume waliooa, hii yawahusu

Wanaume waliooa, hii yawahusu

Hilo la kuweka picha za mkeo ofisini, itategemea ni ofisi gani mkuu!!! Wewe umeajiriwa kwenye kampuni ya wa tu ndo ukaweke picha ya mkeo utafikiri ofisi nzima ni yako? Hiyo itakuwa ni ofisi isiyokuwa na personnel manager!!!

Linawezekana bila shida,labda kama desk unalotumia mnashea na mtu.

Jaribu kama umeipenda hiyo na kuwa firm kuitetea kwa sababu hata za kwamba ndio inakupa motisha ya kazi.michepuko hata waajiri hawaipendi wanajua itakuja kutibuka siku moja.
 
tatizo kuna midada hata uje kazini na mkeo bado watakutega tu....in short jitambue weww ni kichwa cha familia (cheo ulichoapishwa na Mungu) and respect your spouse.

Wala si utani..tena wasio kuwa na haya wanakujua na bado wanataka kula na mumeo....ni kazi lakini maisha yanasonga end of day..ni wako tu
 
Kwa hakika kuna changamoto nyingi ambazo huwa wakinababa, ama kwa ufasaha waume wa watu huwa wanapitia kwenye maeneo tofauti tofauti katika shughuli za mihangaiko.

Huenda ndio kwanza umepata ajira mpya, na hapo ukakutana na kinadada warembo ambao hata wanaweza kumfanya mtu avunje shingo. Kwa vyovyote vile msimamo wako wahitajika, kuungana nao ama kujipambanua kama mume wa mtu kwa mumtaja mkeo na watoto wako, katika lugha ambayo watarudi nyuma tu.


Baadhi yenu tayari yawezekana mmeshazoeana na wafanyakazi wenza kiasi hata cha kuongea na kutaniana katika hali ambayo sio sahihi, ama kwa urahisi - lugha ambayo usingeweza kuongea iwapo mkeo ama kiongozi wako kanisani angekuwepo eneo hilo. Kama ndivyo basi, mwanaume ukumbuke kuwa wewe ni kiongozi, rejea katika hali yako bila kuterereka.


Kuna mifano mingi ambayo haijaandikwa hapo, lakini umeshuhudia ikikutokea ama kwa rafiki yako wa karibu. Kama iliyoandikwa hapo haijakutokea, hebu tafakari hata namna ambavyo huwa unazungumza na mhudumu wa supermarket, mwanadada wa mapokezi hotelini, ama hata unapokwenda kula mgahawani, huwa unaongeaje? Ama pia kama wewe ndio uko mapokezi hotelini ama guest house, huwa unaongea kwa namna gani?


Baada ya kusema hayo, ni vema sasa tukatazama mambo matano ambayo kila mwanaume aliyeoa anatakiwa kufanya awapo mbele ya kinadada ambao hawajaolewa, kama ambavyo Gospel Kitaa imenukuu kutoka Charisma News.

1. Hakikisha pete yako ipo ON;
Licha ya kwamba kuna sehemu ambazo pete hutakiwa kuvuliwa, mathalani pale ambapo unaendesha mitambo mikubwa, na sehemu nyinginezo. Inapotokea upo sehemu ambapo kusanyiko la watu waliopo litakufanya ujifikirie kuivua ama kuiacha pete yako kidoleni, ondoka na ukimbie upesi sehemu hiyo.Kiapo chako, ndoa yako, watoto wako and vingine vingi vyote vinategemea maamuzi yatakayofanya hapo. Aliye mwaminifu katika lililo dogo sana huwa mwaminifu katika lililo kubwa pia;... Luka 16:10 imeeleza.

2. Weka picha za mkeo ofisini kwako
Iwapo uko katika mazingira magumu (umezungukwa na kinadada single, tena warembo) ni busara kuweak picha kadhaa za wewe pamoja na mkeo, hasa wakati ambao mlikuwa mnaenjoy, "fun moments" pamoja. Kwanza hilo litakukumbusha kwanini unampenda mkeo, na pia itawafanya kila wakiingia ofisini kwako wakutane nazo, na kuwafanya waelewe kuwa mnapendana. Picha hizi angalau uwe unazibadili mara kadhaa, na maana yake ni kwamba mahusiano yenu yako vizuri, atakayekuja na kukuta picha nzuri tofauti tofauti, donge lake litamuua mwenyewe. Unigeuze macho yangu, nisitazame visivyofaa... Zaburi 119:37.



3. Epuka macho kwa macho muda mrefu
Hapa haina maana kwamba uwe unaongea huku humtazami mtu kabisa, la hasha. Ila ni kwamba unapomtazama mtu, macho nayo huongea, kwahiyo inategemea umemtazama kwa namna gani. Kama ukivaa sura ya kazi, basi mambo yote yataenda vema, ila unapotazama kitofauti - ni kama vile unamkaribisha kwa mambo mengine. Hivyo ni vema kuwa makini unaposafirisha macho yako kwake, usije ukaishia kuzini nae. Lakini mimi nawaambia, Kila mtu amtazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake. Mathayo 5:28.

Lecture inaendelea zaidi hapa;
Gospel Kitaa™: MUME WA MTU, FANYA HAYA MBELE YA WANAWAKE SINGLE, UJINUSURU
nani kakudanganya? wanaume wenye wake siku hizi ndiyo wanatafutwa! karagabaho.
 
...loh! na kila mtu amtazamaye mwanaume kwa kumtamani je?

Vice versa is not true, hahaha! Na imeandikwa usimtamani mke wa mwenzio na mme wa mwenzio andiko liko kimya, au mi ndo sielewi!
 
Hilo la kuweka picha za mkeo ofisini, itategemea ni ofisi gani mkuu!!! Wewe umeajiriwa kwenye kampuni ya wa tu ndo ukaweke picha ya mkeo utafikiri ofisi nzima ni yako? Hiyo itakuwa ni ofisi isiyokuwa na personnel manager!!!

unafanya kazi wapi?!! sijawahi kuskia ofisi inakuzuiya kuweka picha ya familia yako mezani au juu ya shelf?!!! personalization ya ofisi inakufanya urelax na kuwa na mood; kama wewe ndiyo manager na unazuiya hali hiyo basi ndugu yangu rudi shuleni ukajiupdate.
 
Wakija watasema hivi "wenzio tunalilia tuwekwe moyoni wewe unalilia uwekwe ofisino?" blessed article nzuri
 
unafanya kazi wapi?!! sijawahi kuskia ofisi inakuzuiya kuweka picha ya familia yako mezani au juu ya shelf?!!! personalization ya ofisi inakufanya urelax na kuwa na mood; kama wewe ndiyo manager na unazuiya hali hiyo basi ndugu yangu rudi shuleni ukajiupdate.

Nafikri hujaelewa unachobishania!!

Haya ndo yanayowagharimu ninyi .com mpaka mnapoteza kazi kwa upuuzi huu. Kwa nini kama picha ya mkeo na familia yako usiweke kwenye Laptop yako ili hata ukiwa kazini unakuwa nayo. Sasa wewe mburura ukabandike picha ya mkeo kwenye ofisi ya watu? Mwingine kwa ujinga huo niliwahi kumshuhudia ameweka picha za familia kwenye computer ya ofisi, sasa hiyo inalipa kweli? Upuuzi!!!!!!!!!!!!!!!
 
Nafikri hujaelewa unachobishania!!

Haya ndo yanayowagharimu ninyi .com mpaka mnapoteza kazi kwa upuuzi huu. Kwa nini kama picha ya mkeo na familia yako usiweke kwenye Laptop yako ili hata ukiwa kazini unakuwa nayo. Sasa wewe mburura ukabandike picha ya mkeo kwenye ofisi ya watu? Mwingine kwa ujinga huo niliwahi kumshuhudia ameweka picha za familia kwenye computer ya ofisi, sasa hiyo inalipa kweli? Upuuzi!!!!!!!!!!!!!!!

mbona povu linakutoka BILA HATA KUJIBU SWALI! Kama kuna ofisi inazuiya kuweka picha ya mkeo kwenye dawati lako sema ni ofisi gani? Hata ofisini kwa obama nina imani hakosi picha ya mpendwa/wapendwa wake. SIPENDI KUBISHANA, NAPENDA KUJADILI, so far sijawahi kusikia ofisi yenye marufuku ya kuweka picha, au mwenzetu usiye mpuuzi ulishawahi kusikia?
 
Kama ndani ya nyumba hakujatibuka hayo yote yanazingatiwa! ndoa ikishakwaruzika tu kila mmoja anatafuta mahali pa kumpatia faraja!
 
Kwa hakika kuna changamoto nyingi ambazo huwa wakinababa, ama kwa ufasaha waume wa watu huwa wanapitia kwenye maeneo tofauti tofauti katika shughuli za mihangaiko.

Huenda ndio kwanza umepata ajira mpya, na hapo ukakutana na kinadada warembo ambao hata wanaweza kumfanya mtu avunje shingo. Kwa vyovyote vile msimamo wako wahitajika, kuungana nao ama kujipambanua kama mume wa mtu kwa mumtaja mkeo na watoto wako, katika lugha ambayo watarudi nyuma tu.


Baadhi yenu tayari yawezekana mmeshazoeana na wafanyakazi wenza kiasi hata cha kuongea na kutaniana katika hali ambayo sio sahihi, ama kwa urahisi - lugha ambayo usingeweza kuongea iwapo mkeo ama kiongozi wako kanisani angekuwepo eneo hilo. Kama ndivyo basi, mwanaume ukumbuke kuwa wewe ni kiongozi, rejea katika hali yako bila kuterereka.


Kuna mifano mingi ambayo haijaandikwa hapo, lakini umeshuhudia ikikutokea ama kwa rafiki yako wa karibu. Kama iliyoandikwa hapo haijakutokea, hebu tafakari hata namna ambavyo huwa unazungumza na mhudumu wa supermarket, mwanadada wa mapokezi hotelini, ama hata unapokwenda kula mgahawani, huwa unaongeaje? Ama pia kama wewe ndio uko mapokezi hotelini ama guest house, huwa unaongea kwa namna gani?


Baada ya kusema hayo, ni vema sasa tukatazama mambo matano ambayo kila mwanaume aliyeoa anatakiwa kufanya awapo mbele ya kinadada ambao hawajaolewa, kama ambavyo Gospel Kitaa imenukuu kutoka Charisma News.

1. Hakikisha pete yako ipo ON;
Licha ya kwamba kuna sehemu ambazo pete hutakiwa kuvuliwa, mathalani pale ambapo unaendesha mitambo mikubwa, na sehemu nyinginezo. Inapotokea upo sehemu ambapo kusanyiko la watu waliopo litakufanya ujifikirie kuivua ama kuiacha pete yako kidoleni, ondoka na ukimbie upesi sehemu hiyo.Kiapo chako, ndoa yako, watoto wako and vingine vingi vyote vinategemea maamuzi yatakayofanya hapo. Aliye mwaminifu katika lililo dogo sana huwa mwaminifu katika lililo kubwa pia;... Luka 16:10 imeeleza.

2. Weka picha za mkeo ofisini kwako
Iwapo uko katika mazingira magumu (umezungukwa na kinadada single, tena warembo) ni busara kuweak picha kadhaa za wewe pamoja na mkeo, hasa wakati ambao mlikuwa mnaenjoy, "fun moments" pamoja. Kwanza hilo litakukumbusha kwanini unampenda mkeo, na pia itawafanya kila wakiingia ofisini kwako wakutane nazo, na kuwafanya waelewe kuwa mnapendana. Picha hizi angalau uwe unazibadili mara kadhaa, na maana yake ni kwamba mahusiano yenu yako vizuri, atakayekuja na kukuta picha nzuri tofauti tofauti, donge lake litamuua mwenyewe. Unigeuze macho yangu, nisitazame visivyofaa... Zaburi 119:37.



3. Epuka macho kwa macho muda mrefu
Hapa haina maana kwamba uwe unaongea huku humtazami mtu kabisa, la hasha. Ila ni kwamba unapomtazama mtu, macho nayo huongea, kwahiyo inategemea umemtazama kwa namna gani. Kama ukivaa sura ya kazi, basi mambo yote yataenda vema, ila unapotazama kitofauti - ni kama vile unamkaribisha kwa mambo mengine. Hivyo ni vema kuwa makini unaposafirisha macho yako kwake, usije ukaishia kuzini nae. Lakini mimi nawaambia, Kila mtu amtazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake. Mathayo 5:28.

Lecture inaendelea zaidi hapa;
Gospel Kitaa™: MUME WA MTU, FANYA HAYA MBELE YA WANAWAKE SINGLE, UJINUSURU

Full of TITO and GIGO i.e Trash In Trash Out and Gabbage In Gabbage Out...............Hopeless Fellow indeed!!!!!!!!!!!!!
 
Haya mawazo ni ya zama za kale za mawe tena kule kijijini mpakani na burundì au nanjìlinji. Hata ingekuwa ofsi yako binafsi ndo ujaze mapicha ya mkeo? Yanaöngeza uzalishaji? Inaelekea mtoa mada hajui upana wa neno ofisi! Mpìgadebe.konda,dreva wote,polisi,mvuvi, picha za wake zao wabandke wapì? Ndo maana nch inakuwa maskini sababu mud wote mnakaa mmejfungia ofsini mnaangalia matako ya wake znu ktk picha. Nini kaz ya hizi mobile digital devices ie tablets,smtphones etc?
 
Hivi bado kuna kuaminiana kwenye ndoa siku hizi? Manake naona kama ndoa inakuwepo tu nyumbani mtu na mwenzie, baada ya hapo kila mtu na michakato yake anayoijua yeye mwenyewe.
 
Back
Top Bottom