Wanaume tusiwapige wake

nzalendo

JF-Expert Member
Joined
May 26, 2009
Posts
12,701
Reaction score
14,103
Salaam kwenu wana jamii,

Kwa kifupi sana,uanaume ni pamoja na ustahimilivu wa hali ya juu,hawa wake zetu ni watu dhaifu mno.
Ndo maana imeandikwa tuishi nao kwa akili.

Nazungumza haya kwa sababu jana usiku sikulala kwa ajili ya ugomvi uliotea kwa jirani yangu.

Kisa ati jamaa hajapelekewa maji bafuni daah,kamgarazaga mkewe kiasi cha kumvujisha damu za kutosha na wakati huo mkewe alikuwa jikoni anaandaa riziki ya usiku,zingatia mkewe si mama wa nyumbani nae katoka job vile vile,hatuelewi alimchana na kitu gani kiasi cha kumvujisha damu nyingi kivile na jamaa alikuwa hajalewa labda kuna jambo lingine ndani yake.

Mayowe na vilio vya house girl wao,mwanae wa vidudu(nursery school) pamoja na mwanae mdogo kichanga cha mizezi kadhaa ndio vilitushtua lakini sikutaka kwenda huko,mpaka pale mlinzi alipokuja kutujuza kwamba jamaa anauwa mkewe,ikabidi tuelekee kwenda kumnusuru mama huyu.

Kufika pale jamaa anaanza kutuomba msamaha sisi na kututaka kusaidia kwenda polisi kuchukua pf3 ati kaanguka na pikipiki.(kauli hii Kichanga kwa jirani kililia usiku kucha).very sad.

Jamaa walielekea huko pamoja na majirani mpaka alfajiri naondoka hakuna yeyote aliyerudi.

Wanaume tusiwapige hawa viumbe ni dhaifu mno.
 
Hii ni habari yenye fundisho, lakini inafanana na hadithi ya kutunga maana ndani yake hakuna uhalisia: jiulize ni MTU gani anaweza kufikia hatua ya kuwa na mlinzi nyumbani kwake na bado analelekewa maji bafuni!!!!?????, yaani nyumba inamlinzi harafu baba anaogea bafu la nje!!!???, hakuna master bedroom!!??. Ngashtuka m
 
Wanaume tupunguze umbea mambo mengine malizeni hukohuko sio lazima nasisi tuyajue.
 
aiseee kama kafanya hivi kuna jambo la siri lingine tena anakichanga jamani
 
Wanaume tupunguze umbea mambo mengine malizeni hukohuko sio lazima nasisi tuyajue.
Huu si umbea hili ni fundisho tosha,kuna uwezekano huyo mama kapoteza maisha,labda itatokea ktk vyombo habari
 
mbona mimi nina master ila sina umeme napeleka maji ya moto kila siku bafuni kwaajili ya mume wangu
 
akili yako ndo hufikiri hivyo.
 
Kama ulipata bahati ya kukaa na wazee ungeelewa unachosema, ndoa ina mambo mengi kwa sababu wamekutana watu wazima kila mmoja na background yake. Ukiona ugomvi kama huo, ujue tatizo sio maji kuna long term cause, hiyo ya maji ni short term tu, labda mume kajibiwa vibaya, kaunganisha na yale ya juzi, hakuna mtu mzima mwenye akili anayeweza kuanza kumtandika mkewe kisa hajapelekewa maji ilihali anaona mkewe yuko jikoni akiandaa maakul.
 

Kuna kitu ambacho nacho wanawake inabidi wajifunze kuwa ni vigumu sana kwa mwanamke akapigana na mwanaume akamshinda,ni wanawake wachache sana ambao wanaweza wakapigana na waume/wapenz wao wakawapiga!!shida inakuja pale linapotokea zogo hlf mwanaume akampiga mwanamke ngumi/teke/kibao au chochote hlf mwanamke akajifanya anadindisha na kutaka kupambana badala ya kutafuta jinsi ya kujinasua aidha kwa kukimbia au kujishusha!!hapo ndipo anapopewa kichapo kikali kwasababu kwa asili ni aibu kwa mwanaume kupigwa na mwanamke,hvyo akijifanya m'bishi atapigwa tu!!Onyo:Wanawake msithubutu kutunishiana misuli na wanaume mtapigwa tu!!
 
Marekani ukipiga mwanamke unaenda Jela,Kazi unafukuzwa na utakuwa kwenye News sana
 
Weka picha ijapokua yuko spitali, kutoekewa maji ndio ampe kipigo. Hapa kuna kesi mbili
1: aidha mtoa mada umetudanganya
Au
2: mwanamke ameolewa na chizi
 

me nime log in kwa ajiri yako hiyo kitu hata mm nimestuka ila nikapata jbu kwamb kila m2 kama amegombana na mwenz hawez kusema sababu wazi wazi lazma ataongea mambo kama hyo au hajui kupika au hachelewa kuludi ukijifanya unasuluhsha watakubaliana fasta kumbe moyoni wanajua kisa
 
Weka picha ijapokua yuko spitali, kutoekewa maji ndio ampe kipigo. Hapa kuna kesi mbili
1: aidha mtoa mada umetudanganya
Au
2: mwanamke ameolewa na chizi

pale imetumika lugha ya picha kwa hyo we ulitaka aseme huyu mwanamke hatak kunipa papuch n.k
 
Wewe mwanaume wa ukweli bora umewaambia,wameshawafanya wenzao mipira.Ukiwakuta makanisani na misikitini utasema mume si ndio huyu!!1 haa nyumbani bondia.
 
Samahani naona hiii hainihusu, kama mada za kitchen party vile. nimepotea njia
 
Marekani ukipiga mwanamke unaenda Jela,Kazi unafukuzwa na utakuwa kwenye News sana

HIYO SHERIA HUKU BONGO HAIFAI,WANAWAKE ZETU NI WATU WA HILA SANA ANAWEZA KUJITEGESHA ILI AKUKOMOE.:angry:
 
samahani naona hiii hainihusu, kama mada za kitchen party vile. Nimepotea njia

hujapotea njia mkuu,ukibahatika kuingia kwenye ndoa iko siku mtakwaruzana,hivyo basi kama wewe ni mwanaume yakupasa uwe na ustahimilivu wa hali ya juu,vinginevyo hasira ni hasara.
 
Mnaaziiiiiiii mungu Kashasema Tuwapige wake zetu, Wewe nani useme tusiwapige wake zetu na wakati Mnyaziiiiiii mungu kashasema...? :angry:


4:34 Sahih International
Men are in charge of women by what Allah has given one over the other and what they spend from their wealth. So righteous women are devoutly obedient, guarding in absence what Allah would have them guard. But those from whom you fear arrogance - advise them; forsake them in bed; and strike them. But if they obey you seek no means against them. Indeed, Allah is ever Exalted and Grand

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…