nzalendo
JF-Expert Member
- May 26, 2009
- 12,701
- 14,103
Salaam kwenu wana jamii,
Kwa kifupi sana,uanaume ni pamoja na ustahimilivu wa hali ya juu,hawa wake zetu ni watu dhaifu mno.
Ndo maana imeandikwa tuishi nao kwa akili.
Nazungumza haya kwa sababu jana usiku sikulala kwa ajili ya ugomvi uliotea kwa jirani yangu.
Kisa ati jamaa hajapelekewa maji bafuni daah,kamgarazaga mkewe kiasi cha kumvujisha damu za kutosha na wakati huo mkewe alikuwa jikoni anaandaa riziki ya usiku,zingatia mkewe si mama wa nyumbani nae katoka job vile vile,hatuelewi alimchana na kitu gani kiasi cha kumvujisha damu nyingi kivile na jamaa alikuwa hajalewa labda kuna jambo lingine ndani yake.
Mayowe na vilio vya house girl wao,mwanae wa vidudu(nursery school) pamoja na mwanae mdogo kichanga cha mizezi kadhaa ndio vilitushtua lakini sikutaka kwenda huko,mpaka pale mlinzi alipokuja kutujuza kwamba jamaa anauwa mkewe,ikabidi tuelekee kwenda kumnusuru mama huyu.
Kufika pale jamaa anaanza kutuomba msamaha sisi na kututaka kusaidia kwenda polisi kuchukua pf3 ati kaanguka na pikipiki.(kauli hii Kichanga kwa jirani kililia usiku kucha).very sad.
Jamaa walielekea huko pamoja na majirani mpaka alfajiri naondoka hakuna yeyote aliyerudi.
Wanaume tusiwapige hawa viumbe ni dhaifu mno.
Kwa kifupi sana,uanaume ni pamoja na ustahimilivu wa hali ya juu,hawa wake zetu ni watu dhaifu mno.
Ndo maana imeandikwa tuishi nao kwa akili.
Nazungumza haya kwa sababu jana usiku sikulala kwa ajili ya ugomvi uliotea kwa jirani yangu.
Kisa ati jamaa hajapelekewa maji bafuni daah,kamgarazaga mkewe kiasi cha kumvujisha damu za kutosha na wakati huo mkewe alikuwa jikoni anaandaa riziki ya usiku,zingatia mkewe si mama wa nyumbani nae katoka job vile vile,hatuelewi alimchana na kitu gani kiasi cha kumvujisha damu nyingi kivile na jamaa alikuwa hajalewa labda kuna jambo lingine ndani yake.
Mayowe na vilio vya house girl wao,mwanae wa vidudu(nursery school) pamoja na mwanae mdogo kichanga cha mizezi kadhaa ndio vilitushtua lakini sikutaka kwenda huko,mpaka pale mlinzi alipokuja kutujuza kwamba jamaa anauwa mkewe,ikabidi tuelekee kwenda kumnusuru mama huyu.
Kufika pale jamaa anaanza kutuomba msamaha sisi na kututaka kusaidia kwenda polisi kuchukua pf3 ati kaanguka na pikipiki.(kauli hii Kichanga kwa jirani kililia usiku kucha).very sad.
Jamaa walielekea huko pamoja na majirani mpaka alfajiri naondoka hakuna yeyote aliyerudi.
Wanaume tusiwapige hawa viumbe ni dhaifu mno.