Mkuu wanaume wa aina hiyo nawajua sana, huwa hawana uhuru wa kujiamulia mambo. Kuna dada mmoja anaishi na aina ya mwanaume uliyemtaja, dada anajiweza na mzee wake ni tajiri, huyo dada nimesikia anachepuka na vijana aliwazidi umri tena bila kujificha! jamaa anajua ila anauchuna tu kwa kuwa yeye ni kula kulala.
Kama kuna wanaume wa aina hii hapa jf naombe wabadili mawazo hayo na waachane mara moja na maisha ya aina hiyo kwani yanaharibu asili ya mwanaume kuwa kichwa.