Kabakabana
JF-Expert Member
- Aug 5, 2011
- 5,550
- 1,166
- Thread starter
-
- #141
Kisa chako si cha ajabu kufanywa na baadhi ya wanaume na hata baadhi ya wanawake. Lakini kuuliza "Wanaume mna tatizo gani?" ni kuwachanganya wanaume na hata wanawake wote katika kapu moja.
Katika kuzungumzia "urafiki baina ya wanaume na wanawake", wengi hapa walikuja na wazo kuwa "kitu hicho hakiwezekani", wanaamini ama mnakuwa wapenzi au kila mmoja kivyakevyake; [jambo ambalo mimi ninapingana nalo]. Urafiki baina ya mwanamume na mwanamke unawezekana, cha muhimu ni kuweka mipaka tangu mwanzo, jambo ambalo wewe ulifanya kwenye 1. nyekundu la kumpa nambari ya simu lakini ukakosea zaidi kwenye 2. nyekundu kwa kumfanya rafiki mtu ambaye ulijua kuwa alikuwa hakutaki kama rafiki tu.
Na hiyo 3. nyekundu bado nina mashaka kuwa "rafiki yako" kwa maana ya rafiki anafika hadi anaolewa ukiwa hujui bwana arusu ni nani. Lakini hayo yote ni maangalizo tu, ninachotaka kukushauri, kama walivyo kushauri wengine, kwa heshima ya huyo "shoga yako", achana kabisa kabisana huyo fataki na hata na shoga yako. Kuwa kwako karibu na shoga yako ni sawa na kuwa karibu na huyo jamaa.
Alikupenda, wewe hukumpenda, Alipomaanisha wewe hukua tayari kuona utayari wake, Sasa wenzako wameona na wameshamaliza kila kitu, Mwache aangalie ndoa yake
Siku naoa nami ktk kudensi nilimwambia mdada mwingine nampenda akachekelea kweli!....mwalimu wenu mmoja!
kawaida hiyo kwani moyo unavyumba vingi vya kuhifadhi mapendo. Ila kimsingi ulimdhulumu kukupenda kwani bado anahitaji nafsi yako. We mpage tu kihalali
Ulikuwa unatoka nae out halafu unamdengulia sasa imekula kwako na roho inauma. Thats the game man plays hata kina dada,unakuwa na watu wawili stand by,mmoja akizingua anachukua yule aliyetayari,ni mambo ya sampling tu kabakabana
South America huko ati-Brazil!
Wanaume hatuna matatizo ila wakati mwingine tunazidiwa nguvu na hawa wenzetu. Lakini mwanaume kutongoza ni kitu cha kawaida. na je, nauliza wanawake mna matatizo gani kuwakubalia wanaume ambao mna uhakika kuwa wameoa lakini bado mnatoka nao na kuwapa kile wanachotaka?
Pole sana! Kwa kuwa jamii yetu haikubali/ haitambui urafiki wa mwanamke na mwanamume basi tumia tukio kama "uzoefu" mbele ya safari.wewe ni mtu wa kwanza kwa kunielewa,nakushukuru sana.
Mimi nilikuwa busy na mbali kwa muda, kwahiyo hata sikuwaza mambo ya kuuliza bwana harusi ni nani.
niliönana nae kwa drinks mara kadhaa kama mara 3 au 4 baada ya siku ile.,kupata a drink na mtu ina maanisha hujatulia?ahsante kwa kunifahamisha.