Wanataaluma wamtetea Lowassa kujiunga na CCM

Wanataaluma wamtetea Lowassa kujiunga na CCM

MIMI BABA YENU

JF-Expert Member
Joined
Mar 1, 2019
Posts
319
Reaction score
755
Baadhi ya wanataalamu wamemtetea Edward Lowassa kwa uamuzi wake kujiunga tena na Chama Cha Mapinduzi (CCM), huku wakidai kuwa upinzani katika nchi umekosa ajenda za uwazi na maono.

Mhadhiri Mwandamizi, wa Chuo Kuu cha Dar es salaam, Dr Benson Bana, katika mahojiano na "Jumapili Habari" alisema kuwa sio kosa la jinai kwa wanasiasa kuhama kutoka chama kimoja cha siasa kwenda kingine, kwamba wanasiasa wanajihusisha na vyama vya siasa ambavyo wanaamini kuwa matarajio yao ya kisiasa yanaweza kutimizwa.
 
IMG-20190302-WA0001.jpg
 
Wale wote waliomtukana mzee wa watu kuwa alikuwa akijinyea ni wakati wao wa kutafuta sabuni na maji kumsafisha ili atakate

Wale waliosema mgonjwa anayesubili kufa ni wakati wao sasa kumuomba msamaha mzee wa watu

Wale waliosema kuwa ikulu hakuna wodi ya wagonjwa ni wakati wao pia kujitafakari

Wapo wengine walisema mafisadi yamemkimbia ni wakati sasa wa kutafuta jiki kumsafisha ili atakate na anukie kama waridi
 
Njaa za hawa wanaojiita wataalamu wa comments za kisiasa ndizo zinazowasumbua,hakuna yeyote aliyenyosha kidole chake wakati mmoja wao Mr.Bushiri alipoteuliwa kuwa SG wa CCM,hii inatuonyesha ni wanafiki na maoni yao sio ya kuyasikiliza sana,ni vema wanapotoa maoni yao waweke wazi misimamo yao kisiasa ili tunaowasikiliza tuwe na imani nao,huwezi kuwa na political commentator anayejifanya ni neutral kumbe ana mapenzi na chama Fulani,nchi zinazojielewa hawa huwa wanajitambulisha kuhusu misimamo yao na hata watapoandika habari kwenye gazeti au chombo chochote cha habari huwa wanajitambulisha.
 
Back
Top Bottom