Wanasimba wanaomlaumu Ahoua pengine sio wafuatiliaji wa soka.

Wanasimba wanaomlaumu Ahoua pengine sio wafuatiliaji wa soka.

Lee Van free

JF-Expert Member
Joined
Aug 14, 2024
Posts
2,246
Reaction score
7,111
Ahoua kazi yake ni mcheza mpira,anajua kabisa kufunga goli kwake ni Pesa ,utajiri na maisha mazuri.
Anajua kabisa akifunga goli hasa katika michuano hii ya CAF atazawadiwa fedha nyingi, fedha za mama,mashabiki na wafadhiri.
Anajua jina lake litaandiikwa kwenye vitabu vya CAF,Clabu ya Simba na magazeti yote Afrika.
Anajua kabisa soko lake litapanda na bei yake itapanda.
Anajua kabisa umaarufu wake utaongezeka,hakuna mtu asietaka umaarufu,hata Mimi natamani umaarufu.
Anajua atasifiwa kwa kuipeleka Simba hatua za juu.

Hayo ni machache sana,lkn Kuna mengi sana mchezaji hua anatamani kufunga magoli mengi zaidi.

Kwa kifupi mchezaji anajua mpira ni magoli na faida ya kufunga magoli kuliko hata sisi mashabiki.

Wanasimba wenzangu Ukiona mchezaji kama Ahoua au kapombe amekosa goli maana yake sio kwamba hataki,hajui,Hana uwezo au amefanya makusudi.
Anagalie ni ameshafunga mara ngapi,na ukiangalia mechi ya Znz Ahoua alifunga goli ambalo ndio linatupeleka SA tukiwa mbele.

Jamani eeh hakuna alieweza kujua mawazo ya Ahoua kuamua kupiga mwenyewe bila kutoa pasi,huenda Kuna kasoro aliiona kwa Ateba na Mutale ambayo sisi watazamaji hatukuiona.

Jamani eeh mpira pia ni mahesabu,na pengine alipiga hesabu zake kwa haraka akaona Bora ashuti yeye kuliko kutoa pasi,kwani hakuna ushahidi kua Kila pasi huzaa goli,Kuna wengine pia hukosa au hunyang'anywa.
Mfano yeye kapewa pasi na Mpanzu lkn kakosa.
Kumbukeni mpira ni mchezo wa bahati na makosa.
Unaweza kulenga goli bahati ikawa Yako ukafunga au kama sio bahati Yako ukakosa.

Ni kawaida na mara nyingi ukiwa shabiki na mtazamaji ni rahisi kukosoa na kuona wachezaji wanakosea lakini hakika sio kazi rahisi hivyo,wanaocheza ndio wanajua ugumu.
Kumbukeni timu pinzani nayo Ina kocha,imefundishwa,inacheza,inazuia,na piq inataka ushindi.

Hata kwa maaskari Kuna mafunzo ya kulenga shabaha(Range),kwa mfano wakipewa risasi kumikumi,Kuna wakati askari mmoja anaweza kupata zote na Kuna wakati anapata kadhaa.
Kumbuka siku pia hazifanani,
Mfano wawindaji Kuna siku wanafanikiwa kupiga wanyama na Kuna siku wanakosea shabaha.

Hebu tumuangalie Ahoua ameifungia Simba magoli mangapi na assist ngapi ya mechi za ndani na za nje, akiwa amekaa ndani ya Simba Kwa Muda Gani, ukilinganisha na mchezaji kama Chama mfano.
Hebu tufikirie kama Ahoua ana mwaka mmoja ndani ya Simba, lakini amefanikiwa kuchangia kuiingiza Simba nusu fainali,je akiaa miaka kama aliyokaa Chama, hatuoni kama ataisogeza mbele?

Leo hii mkifatilia taarifa za wachezaji wa Afrika kwa mwaka huu wa 2025 katika michuano hii ya shirikisho,hamuwezi kukosa jina la Ahoua

Jamani eeh kukosa magoli sio kutokujua kucheza,wachezaji wote duniani hukosa magoli.

Pamoja na yote Simba inaenda kuitoa Stellenbosch na kwenda kucheza Fainali.

Tazama video hapa chini.


View: https://vm.tiktok.com/ZMBnTQTPm/
 
Mkuu mashabiki oyaoya hawawezi kukuelewa. Kwao Simba inaweza kushinda kila mechi. Tofauti na hapo utasikia, mara hatuna namba 10, hatuna box to box midfielder, hatuna striker, fulani yuko slow, Mo tuletee striker, mara fukuza fulani hafai n.k. Yaani wanawaona wachezaji wa Simba kama malaika wasiotakiwa kukosea. Na pia hawajui kuwa timu pinzani nayo inapambana kuziba mianya ya kufungwa na kutafuta ushindi pia. Wanabeza ushindi wa goli moja wakati tumeshuhudia Al Ahly na Memolodi wakitoka suluhu. Yaani bongo ni taabu kwelikweli. Kuwa kocha au mchezaji wa Simba ni shida.
 
Kwani mechi ile ahoua kakosa goli moja, alipiga mpira wa kichwa ukaenda nje, hakuna anaelalamikiwa hilo..
Ile nafasi ya mwisho aliyokosa ndio sababu ya yote, sababu alivunja moja ya msingi wa mchezo wa mpira wa miguu(simplification)
Mpira unachezwa katika namna ya kusimplify, umeona pasi aliopewa yeye na mpanzu ile ni simplification, mpanzu alikuwa na uwezo wa kushoot, lakini kushoot toka mita 20 na kumpasia mtu ambae anakuwa 1vs1 na golikipa ipi umerahisisha... Nae alitakiwa kurahisisha, wachezaji wengi wanaimbwa sababu wanaurahisiha mpira, kiasi unaonekana mchezo mwepesi

Ukiachana na hilo, bwana mdogo ubora wake ni mdogo, mpime yeye vs namba 10 za yanga, azam na singida big stars.. kuna baadhi ya timu hakai hata henchi, mfano pale yanga ni haramu kwa ahoua kukaa benchi, amuweoe benchi nani pacome au azizi ki, fikiria uwezo wa fei toto anamsogelea, jibu ni HAPANA
Vipi yule tchakei wa big stars?

Ni aidha ajifunze zaidi, ama abaki hivyo na ubora ambao haukidhi pale simba. Timu iwe bora inahitaji wachezaji wenye ubora wa juu, tizama mpanzu ni mchezaji mzuri, tizama kipa camara, abdurazak hamza, kagoma, ngoma, kapombe, tshabalala hata kibu...

Ahou ni mchezaji wa kawaida saana.
 
Mtuachie Ahou wetu.....
Huyo huyo bdo anatokea mara nyingi kwny vikosi bora CaF kila wakicheza
Huyo huyo alitupa goli la dhahabu na wale waarabu safixien kule Algeria
Huyo huyo ndo anaeweza kupiga mipira iliyokufa kwa usahihi zaidi...
Kama mnataka wacheji machachari kama Ngiri pori aka kina kasongo tafuteni timu zenu muwasajili....
Mkikaa nje ya kumi na 18 midomo mirefuuuu....
 
Mtuachie Ahou wetu.....
Huyo huyo bdo anatokea mara nyingi kwny vikosi bora CaF kila wakicheza
Huyo huyo alitupa goli la dhahabu na wale waarabu safixien kule Algeria
Huyo huyo ndo anaeweza kupiga mipira iliyokufa kwa usahihi zaidi...
Kama mnataka wacheji machachari kama Ngiri pori aka kina kasongo tafuteni timu zenu muwasajili....
Mkikaa nje ya kumi na 18 midomo mirefuuuu....
Baadhi ya mashabiki wanataka kushinda Kila mechi utadhani Simba inacheza na watoto wa chekechea
 
Mkuu mashabiki oyaoya hawawezi kukuelewa. Kwao Simba inaweza kushinda kila mechi. Tofauti na hapo utasikia, mara hatuna namba 10, hatuna box to box midfielder, hatuna striker, fulani yuko slow, Mo tuletee striker, mara fukuza fulani hafai n.k. Yaani wanawaona wachezaji wa Simba kama malaika wasiotakiwa kukosea. Na pia hawajui kuwa timu pinzani nayo inapambana kuziba mianya ya kufungwa na kutafuta ushindi pia. Wanabeza ushindi wa goli moja wakati tumeshuhudia Al Ahly na Memolodi wakitoka suluhu. Yaani bongo ni taabu kwelikweli. Kuwa kocha au mchezaji wa Simba ni shida.
Baadhi ya mashabiki wenzangu wa Simba ukweli tuna changamoto,wanazionaga kama timu nyingine zimekuja kuwaangalia TU Simba wakicheza,wanaonaga timu nyingine kama hazina haki ya kushindana,kuzuia na kishambulia.
Yani ni kama vile Simba Inacheza na watoto wa chekechea.
 
Binafsi siamini sana kwenye Namba.
Kama namba zinasema ukweli.

George Mpole.
Fiston Mayele.
HAWA WALIKUWA WANAWANIA KIATU CHA MFUNGAJI BORA.

Molinga ameondoka yanga akiwa na Magoli 12 akiwa ndio mfungaji wao wa Msimu.

Isitoshe hata Fredy na Saido waliondoka simba wakiwa Wafungaji Bora ndani ya Klabu yao.

Huyo mchezaji wenu Goigoi simtaki kabisa (lile ni Gharasa).

Mimi sio muumini wa Namba
Sizipendi Namba.
 
Binafsi siamini sana kwenye Namba.
Kama namba zinasema ukweli.

George Mpole.
Fiston Mayele.
HAWA WALIKUWA WANAWANIA KIATU CHA MFUNGAJI BORA.

Molinga ameondoka yanga akiwa na Magoli 12 akiwa ndio mfungaji wao wa Msimu.

Isitoshe hata Fredy na Saido waliondoka simba wakiwa Wafungaji Bora ndani ya Klabu yao.

Huyo mchezaji wenu Goigoi simtaki kabisa (lile ni Gharasa).

Mimi sio muumini wa Namba
Sizipendi Namba.
Hata kama huzipendi , ndizo zinazoamua kwenye soka. Aliyefunga goli 3 na kufungwa goli 2, aliyeshinda ni mwenye goli tatu. Haijalishi kachezaje. Hata anayeongoza ligi au kutwaa ubingwa , ni yule mwenye idadi kubwa ya pointi. Namba hazindanganyi. Unafananisha babu Pacome na Ahoua.!?
 
Hata kama huzipendi , ndizo zinazoamua kwenye soka. Aliyefunga goli 3 na kufungwa goli 2, aliyeshinda ni mwenye goli tatu. Haijalishi kachezaje. Hata anayeongoza ligi au kutwaa ubingwa , ni yule mwenye idadi kubwa ya pointi. Namba hazindanganyi. Unafananisha babu Pacome na Ahoua.!?
Duuh!

Kwahiyo kwako Ahoua ni bora kuliko Pacome?
 
Hata kama huzipendi , ndizo zinazoamua kwenye soka. Aliyefunga goli 3 na kufungwa goli 2, aliyeshinda ni mwenye goli tatu. Haijalishi kachezaje. Hata anayeongoza ligi au kutwaa ubingwa , ni yule mwenye idadi kubwa ya pointi. Namba hazindanganyi. Unafananisha babu Pacome na Ahoua.!?
Namfananisha Mayele na George mpole.

Hapo ndio utajua namba zinadanganya ama hazidanganyi.

Otherwise uwe kichaa ,
Huwezi ukafananisha Uwezo wa Ahoua na Pakome.
 
Ahoua kazi yake ni mcheza mpira,anajua kabisa kufunga goli kwake ni Pesa ,utajiri na maisha mazuri.
Anajua kabisa akifunga goli hasa katika michuano hii ya CAF atazawadiwa fedha nyingi, fedha za mama,mashabiki na wafadhiri.
Anajua jina lake litaandiikwa kwenye vitabu vya CAF,Clabu ya Simba na magazeti yote Afrika.
Anajua kabisa soko lake litapanda na bei yake itapanda.
Anajua kabisa umaarufu wake utaongezeka,hakuna mtu asietaka umaarufu,hata Mimi natamani umaarufu.
Anajua atasifiwa kwa kuipeleka Simba hatua za juu.

Hayo ni machache sana,lkn Kuna mengi sana mchezaji hua anatamani kufunga magoli mengi zaidi.

Kwa kifupi mchezaji anajua mpira ni magoli na faida ya kufunga magoli kuliko hata sisi mashabiki.

Wanasimba wenzangu Ukiona mchezaji kama Ahoua au kapombe amekosa goli maana yake sio kwamba hataki,hajui,Hana uwezo au amefanya makusudi.
Anagalie ni ameshafunga mara ngapi,na ukiangalia mechi ya Znz Ahoua alifunga goli ambalo ndio linatupeleka SA tukiwa mbele.

Jamani eeh hakuna alieweza kujua mawazo ya Ahoua kuamua kupiga mwenyewe bila kutoa pasi,huenda Kuna kasoro aliiona kwa Ateba na Mutale ambayo sisi watazamaji hatukuiona.

Jamani eeh mpira pia ni mahesabu,na pengine alipiga hesabu zake kwa haraka akaona Bora ashuti yeye kuliko kutoa pasi,kwani hakuna ushahidi kua Kila pasi huzaa goli,Kuna wengine pia hukosa au hunyang'anywa.
Mfano yeye kapewa pasi na Mpanzu lkn kakosa.
Kumbukeni mpira ni mchezo wa bahati na makosa.
Unaweza kulenga goli bahati ikawa Yako ukafunga au kama sio bahati Yako ukakosa.

Ni kawaida na mara nyingi ukiwa shabiki na mtazamaji ni rahisi kukosoa na kuona wachezaji wanakosea lakini hakika sio kazi rahisi hivyo,wanaocheza ndio wanajua ugumu.
Kumbukeni timu pinzani nayo Ina kocha,imefundishwa,inacheza,inazuia,na piq inataka ushindi.

Hata kwa maaskari Kuna mafunzo ya kulenga shabaha(Range),kwa mfano wakipewa risasi kumikumi,Kuna wakati askari mmoja anaweza kupata zote na Kuna wakati anapata kadhaa.
Kumbuka siku pia hazifanani,
Mfano wawindaji Kuna siku wanafanikiwa kupiga wanyama na Kuna siku wanakosea shabaha.

Hebu tumuangalie Ahoua ameifungia Simba magoli mangapi na assist ngapi ya mechi za ndani na za nje, akiwa amekaa ndani ya Simba Kwa Muda Gani, ukilinganisha na mchezaji kama Chama mfano.
Hebu tufikirie kama Ahoua ana mwaka mmoja ndani ya Simba, lakini amefanikiwa kuchangia kuiingiza Simba nusu fainali,je akiaa miaka kama aliyokaa Chama, hatuoni kama ataisogeza mbele?

Leo hii mkifatilia taarifa za wachezaji wa Afrika kwa mwaka huu wa 2025 katika michuano hii ya shirikisho,hamuwezi kukosa jina la Ahoua

Jamani eeh kukosa magoli sio kutokujua kucheza,wachezaji wote duniani hukosa magoli.

Pamoja na yote Simba inaenda kuitoa Stellenbosch na kwenda kucheza Fainali.

Tazama video hapa chini.


View: https://vm.tiktok.com/ZMBnTQTPm/

mbona za MOrata na Yakubu hamna
 
Ahoua ana mengi ya kuifanyia Simba. Hii prèsure anayopewa ni sahihi kwake.

Huyu si mchezaji wa kuunganisha timu kwenye mechi ndogo ishinde goli 8 kama watani zetu, ni mchezaji anayetakiwa kuivusha Simba kwenye mechi muhimu.

Mechi muhimu zinakuja msimu ujao, Sasa ni yeye kuamua hii Pressure aitumie kujiimarisha. Asiangalie namba za NBC, zina umuhimu sana ila si kipimo cha umuhimu wake kwa Simba.

Tunatamani tubebe kombe la ubingwa Africa , lina pesa lina value na lina heshima.

Hata Yanga naamini haisajili kina Pacome ili washinde goli 8 au tisa mashindano ya ndani pekee, nia ni mashindano yenye pesa.
 
Namfananisha Mayele na George mpole.

Hapo ndio utajua namba zinadanganya ama hazidanganyi.

Otherwise uwe kichaa ,
Huwezi ukafananisha Uwezo wa Ahoua na Pakome.
George Mpole na Mayele umewafananisha kwenye nini!?
 
Ningekuwa Tajiri wa Simba
Ahua + Mpanzu
Wengine wote nawatimua kule mbele nawatimua
 
Back
Top Bottom