Wanaotaka kuiondoa CCM wamekwaa kisiki

Wanaotaka kuiondoa CCM wamekwaa kisiki

Imebidi
Tutahakikisha tuko busy kupost mambo mema na mazuri yatakayokuwa yakifanywa na MM kila wakati na kuzidi kusambaza sifa zake njema kila inapotokea nafasi. Atakayefanya kazi hiyo ni sisi wengine wala si yeye! Pia tutahakikisha kila post ya kumchafua inapatiwa majibu bila kutumia ID yake inayojulikana. Ni vema aidha akatupatia majibu na sisi kuyapost ama afungue ID mpya kabisa ambazo hazijawahi kuwepo kwenye mitandao halafu ndo awe anazitumia kujibu lakini kwa kuzingatia tuliyokwishayazungumza hapo juu yaani kutofanya kwa emotion na kuepuka jazba lakini pia kushauriana na watu wa karibu kabla ya kutoa majibu kwa jambo lolote linalomhusu.


That is the best you can think

DIV 5,

angalia sisi wengine wazee sio wewe kinda wa 2012 bado unashika mfagio na kubeba kidumu
 
CCM wanaendelea ,watatafuta mbinu mbadala za kupitisha katiba ,usijidanganye kuwa Katiba itakwama kwenye kura za wananchi ,jiulize hivi anaetangaza matokeo ni nani ? Ni serikali ya CCM au unategemea tume huru ? CCM ina matatizo lakini matatizo yao hayatokei katika kukoseshana ushindi.

Haya kuna hii hatua ya mwisho ya kuandamana nani anatoa vibali vya kuandamana ? Nani anasambaratisha maandamano ? Je wananchi wamejiandaa au mmewaanda kiasi gani kuweza kupambana na polisi wa CCM ?

Je kuna hiztoria yeyote inayoonyesha ushindi ulipatika au matakwa yalisikilizwa kwa maandamano hapaa Tz? Ndio nikasema kisiki kimekwaliwa ,lazima kucha zitoke !
 
CCM ni chama nachokifananisha na mti wa MBUYU... mizizi yake imetandawaa mpaka kwenye mashina ya miti mingine... kuug'oa mti huu yataka mashoka yaliyonolewa hasa.. na wag'oaji makini wanaoujua vyema mbuyu na mizizi yake. vinginenyo ni kama kuupalilia na kuumwagilia maji ili ustawi.
 
CCM ni chama nachokifananisha na mti wa MBUYU... mizizi yake imetandawaa mpaka kwenye mashina ya miti mingine... kuug'oa mti huu yataka mashoka yaliyonolewa hasa.. na wag'oaji makini wanaoujua vyema mbuyu na mizizi yake. vinginenyo ni kama kuupalilia na kuumwagilia maji ili ustawi.

Msumeno inawezekana Mbuyu huufahamu na hii ni pengine umekulia DSM ila kama uko Dodoma au Shinyanga au baadhi ya maeneo kama Singida, Morogoro na kwingineko ungelikuwa unaujua mbuyu. Mbuyu ni mti laini sana na haufai kwa lolote isipokuwa matunda yake na pengine dawa na kutengeneza kamba. Kuifananisha ccm na mbuyu ni kuidharau kwa kiasi kikubwa maana huna haja ya kunoa shoka kwaajili ya kukata mbuyu. Shoka butu, jembe, panga linatosha kusambaratisha mbuyu. Ni kweli mizizi yake inaweza ikasambaa mpaka kwenye miti mingine kama ilivyo ccm kuwa na mapandikizi kwenye vyama vingine lakini mara nyingi mizizi ya mbuyu huwa inajipambanua na ni rahisi kuujua mzizi wa mbuyu kuliko wa mpingo au msonobali au mkwaju mfano: Shibuda ccm-CDM, Zitto ccm-CDM, Kessy CDM-ccm, Lyantonga ccm-TLP, Hamad Rashid ccm-CUF. Mizizi yake inafahamika bwanaaaaa.
 
nguvu ya ccm imebaki kwa polisi,mara tu,polisi watakapofanya kazi kwa haki ccm ni kwaheri
 
Back
Top Bottom