Wananilazimisha nimpe jina Jezebeli

Wananilazimisha nimpe jina Jezebeli

Status
Not open for further replies.
Wana Mmu habarini iam very dissapointed nimezaa na girlfriend wangu ni mnyarwanda anaitwa Yveti wazazi wake mmoja ni,mtanzania ila mama ake ni mnyarwanda na wazazi wake wote wanaishi rwanda(wana biashara zao) nilikutana,nae school of medicine sasa nimezaa,nae cha ajabu wazazi wake wanataka nimuite jina jezebeli mtoto ana siku 14 bado tunazozana maana mimi sitaki hilo jina maana lina mreflect mtu hatari sana kwenye bible ambaye alikua mwanamke katili muuaji anaejipenda for sure sijawai kuona mtu anamuita mwanae jezebel kwa sasa hv tumeamua kumpa jina baby kwa muda hadi tuafikiane ila wao hawataki kuchange mawazo sasa naombeni mnishauri hv ni mindset yangu tu kuhusu jina ama nipo sahihi nikubali hilo jina
Huyo mtoto ni wa mwanamke, ila wewe ni baba tu, inahitaji umri kuyajuwa haya.
 
Hiiii inathibitisha kwann toka mwanzo wazazi walikua wakichagua koo za kwenda kuoa..
Wakwe kama hao sijui tu.
 
Uko sahihi hilo jina sio zuri na kwa taarifa yako majina yana athari kubwa sana maishani na huwezi on a athari hiyo sasa bali inaweza leta athari hapo baadaye kwake hadi uzao wake was nne
 
Hemu elewas userious wa mada kabla hujaropoka, Akikubebea mtoto miezi 9 akakwambia jiue utajiua?
 
Watishie kama wakimuita Jezebeli nawe utabadili jina uitwe Lucifer, wenyewe watazima upuuzi wao.
 
Kiroho majina yana impact kubwa.

Nitakupa mifano miwili tu kutoka kwenye biblia:

1. Kumbuka namna Yakobo alipomkatalia mkewe Raheli kuhusu jina Benoni na badala yake akamwita Benyamini (Soma Mwanzo 35:18). Benoni ilimaanisha "Mwana wa huzuni/son of sorrow" wakati Benyamini ina maana "Mwana wa furaha/son of happiness."

2. Kumbuka pia mtu mmoja alibatizwa jina la Yabeshi na mama yake, kwa kuwa huyu mama alimzaa mtoto huyu kwa maumivu. Yabeshi ilimaanisha "Mwana wa maumivu." Hivyo huyu jamaa alipokuwa mtu mzima maisha yake yakawa ya huzuni na maumivu mpaka alipoutafuta uso wa Mungu, kumbe hakujua vilisababishwa na jina. (Soma 1 Mambo ya Nyakati 4:9-11).

Sasa, tukija kwa jina Yezebeli lina maana "binti wa baali/mungu sanamu" & ukienda kwenye kitabu cha Ufunuo wa Yohana utaona lina reflect ukahaba. Ndio maana Yezebeli mke wa mfalme Ahabu alipenda kuabudu sanamu, kumbe jina lake lilimaanisha "binti wa baali."

Je! Wewe una amini katika nini? Chaguo ni lako.

Hakika mtumishi wa mungu umetoa majibu murua kabisa mpaka nimepata hamu ya kwenda kanisani kuabudu maana yapata miaka karibu 8 toka ni fike church
 
unajua kwanini hawasikilizi mawazo yako mkuu?? wewe ni nani hasa? ulijitambulisha kwao na wazaziwakakujua wazazi wenu wanajuana? umefata taratibu hasa za kulea mimba kama baba mtarajiwa? tuanzie hapo
 
Hakuna jina baya la kike duniani kama hilo...wewe ndio baba na ndio wa kufanya maamuzi kuhusu jina,wape sababu kuwa jina hilo lina maana mbaya.
 
Thiago 3, umeuwa kwamba jamaa ataitwa Lucifer teh, teh....
 
1. kumbe umezaa na Girl friend, nilifikiri Mke!!

2. Je Girl friend wako anaamini NIni? Usikute mwenzako yuko kukamilisha commitment kwa mungu wake...mchunguze vizuri sana ktk hili, je tabia zake ulizikutaje? mlikutana ktk mazingira gani?
kuna wengi sana ambao ni ma-argent wa shetani ktk ulimwengu, ukiwa unafikiri kuwa ni watu wa kawaida.

jambo lingine, girlfriend wako anaweza kuwa hajui au anajua maana ya hilo jina; ila inawezekena yuko possessed by a spirit inayo-demand jina la Jezebel, just to accomplish a certain mission.

kama wengine walivyotangulia kusema...hilo jina ni miongoni ma majina mabaya sana, yakiwa na direct connection na Ukahaba(HARLOT), pamoja na kuabudu miungu(IDIOLATRY)...Ambao ktk hizi kuna laana (CURSE).

Kama ukimwita mtoto wako hilo jina,...usitegemee kuwa atakuwa a normal, dont expect any good thing kutoka kwake, jiandae pia na wewe kuwa inflicted with spiritial challenges,

kwa sababu " the name invokes spirits(demons) associated with it"






Wana Mmu habarini iam very dissapointed nimezaa na girlfriend wangu ni mnyarwanda anaitwa Yveti wazazi wake mmoja ni,mtanzania ila mama ake ni mnyarwanda na wazazi wake wote wanaishi rwanda(wana biashara zao) nilikutana,nae school of medicine sasa nimezaa,nae cha ajabu wazazi wake wanataka nimuite jina jezebeli mtoto ana siku 14 bado tunazozana maana mimi sitaki hilo jina maana lina mreflect mtu hatari sana kwenye bible ambaye alikua mwanamke katili muuaji anaejipenda for sure sijawai kuona mtu anamuita mwanae jezebel kwa sasa hv tumeamua kumpa jina baby kwa muda hadi tuafikiane ila wao hawataki kuchange mawazo sasa naombeni mnishauri hv ni mindset yangu tu kuhusu jina ama nipo sahihi nikubali hilo jina
 
Wana Mmu habarini iam very dissapointed nimezaa na girlfriend wangu ni mnyarwanda anaitwa Yveti wazazi wake mmoja ni,mtanzania ila mama ake ni mnyarwanda na wazazi wake wote wanaishi rwanda(wana biashara zao) nilikutana,nae school of medicine sasa nimezaa,nae cha ajabu wazazi wake wanataka nimuite jina jezebeli mtoto ana siku 14 bado tunazozana maana mimi sitaki hilo jina maana lina mreflect mtu hatari sana kwenye bible ambaye alikua mwanamke katili muuaji anaejipenda for sure sijawai kuona mtu anamuita mwanae jezebel kwa sasa hv tumeamua kumpa jina baby kwa muda hadi tuafikiane ila wao hawataki kuchange mawazo sasa naombeni mnishauri hv ni mindset yangu tu kuhusu jina ama nipo sahihi nikubali hilo jina

Maisha umeyacomplicate mwenyewe kwa kuacha wanawake wote hapa bongo na kwenda kwa mhutu/mtutsi...ina maana huwajui hao watu au uliamua tu kutia masikio pamba??..hapo tatizo wala sio jina tatizo ni hao viumbe ambao maisha ya kuua kwao sio tatizo...pole sana na bado utawajua zaidi hao viumbe kadri muda utakavyosonga...
 
unajua kwanini hawasikilizi mawazo yako mkuu?? wewe ni nani hasa? ulijitambulisha kwao na wazaziwakakujua wazazi wenu wanajuana? umefata taratibu hasa za kulea mimba kama baba mtarajiwa? tuanzie hapo

Mkuu wazazi wanajuana baba yangu anajuana na mama ake pia kuhusu kulea mimba walishauri akae kule hadi mtt akijifungua mm nilikua natuma pesa tu au kwenda kumtembelea
 
Kwa tamaduni za kabila langu ni kwamba,ukizaa na binti ilhali hujamtolea mahari basi mwenye mamlaka ya kumpa jina ni binti mwenyewe hata kama mnaishi pamoja kama mke na mme.(Hii ni kwa mtoto wa kwanza.)

Hii iliwekwa makusudi tu ili wanaume watoe mahari on time kukwepa kadhia hii maana ni fedheha.

Sasa yawezekana hii kitu kwa upande wako inafanywa makusudi tu kumpa jina baya ili utoe mahari and upate authority ya kutoa jina la upande wako.

So yawezekana wanakushinikiza kijanja tu especially kama mmeshatambulishana.

Baba Baby Jiongeze!!

Kama wanalipenda sana hilo jina mbona hawakumpa binti yao?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom