Wanangu na nyie mtazaa tu

Wanangu na nyie mtazaa tu

Mzazi haupaswi kutoa kauli yeyeto negative kwa mwanao hata iwe amekutenda vipi,watamkie baraka TU maana kauli zinaumba.
Mungu alipomaliza uumbaji akamuachia mwanadamu.
Ndo maana tunaumba vitu,maisha yetu kupitia kauli zetu.
Maisha unayoyapitia ni matokeo ya ulimi wako au wa watu
 
Wakati dingi anatwambia hii kauli mimi na mdogo wangu, hapo alikuwa amevimba kwa hasira akiwa hana cha kufanya.

Nakumbuka enzi hizo na mdogo wangu, mimi nikiwa kidato cha nne, mdogo wangu akiwa cha 3. Tulikuwa watundu japo sio watukutu. Kuna siku tuliondoka home bila kuaga, alaf kuna kazi tuliambiwa na mshua tuifanye ila tukasahau.

Tulirejea nyumbani majira ya saa kumi na moja kosoro jioni, njaa kali hatukuwa tumekula kitu tokea asubuhi. Kufika home, mzee alitugombeza sana, alafu akasema kwavile tumeona tumeshakua basi hataki tena kutuona nyumbani, akatusukumizia nje kisha akafunga mlango. (Hapo kumbuka tuna njaa ya hatari na home hawakutuwekea chakula siku hiyo).

Tulikaa pale nje, njaa kali. Nyumba yetu ilikuwa imezungukwa na midizi, na uzuri kulikuwa na ndizi mbivu zimeiva, faza alisema angezitoa jioni. Tulipoona mkungu bado upo, tukakubaliana na dogo tule zile ndizi. Dogo akaenda kufunga ule ule mlango ambao baba alitufungia kwa ndani, dogo akaufunga kwa nje ili kumdhibiti mzee endapo atataka kutoka.

Tulijitahidi sana kuukata taratibu ule mgomba walau usitoe kishindo chochote, ila dingi kwavile alizijua akili zetu, naona machale yakamcheza, ghafla akaja. Kufika mlango anakuta mlango umefungwa kwa nje, kuja kuchungulia kwenye dirisha la jikoni anatukuta vidume tunaushambulia ule mkungu bila wasiwasi.

Alitwangalia pale dirishani, mwishowe akatwambia "Na nyie mtazaa tu"

Siku ikaisha, miaka mingi ikasogea. Sasa hivi nina mtoto wa kiume mkubwa tu, umri miaka 5 anaishi kwa babu na bibi yake (wazazi wangu). Kwavile mimi niko mbali, huwa nina kawaida ya kumpigia simu na kuongea nae mara kwa mara.

Last week nimekaa sehemu na rafiki zangu, nikaona ngoja nimpigie baba ili niongee na mwanangu, nikaongea nae vizuri tu huku nikijaribu kumuuliza mambo kadhaa kadhaa ya shule.

Katika kuendelea kuuliza, ghafla dogo akaniambia "BABA UNAMASWALI SANA , PUMBAVU WEE" kasauti kake kalisikika na wote waliokuwa karibu na mimi pale, na upande wa pili nikasikia bibi yake anakachapa. Nikakata simu.

Baadae faza akanipigia simu, akaniambia "mwanangu nilikwambia na wewe utazaa tu". Sikumjibu,nilikaa kimya tu, then tukaendelea na story zingine.

Dah, haya mambo aisee.

Analyse.
Pole sana mwamba hapa Kuna jirani yangu watoto wake wawili wa kiume wametushia kumfanyia kitu kibaya baada ya huyo jirani kuwa mtata na kumchapa mmojawapo wa hao vijana wake wawili kisa ni kwamba dogo alipeleka grender kwenye ofisi ya kuchomea Ili fundi aitumie matokeo yake fundi akaenda kunywa chai akamuachia dogo ofisi dogo nae akasepa ofisi ikabaki bila mtu na Iko wazi , huyo jirani akazinguana na fundi Kwa Nini kaacha ofisi bila mtu , fundi akawaka na akasema amlaumu mwanae maanda ndio kamuachia ofisi na alitakiwa kupaka rangi baadhi ya magril Sasa huyo jirani akamwendea dogo na KUMPA kichapo , dogo kasusa na kumwambia dingi yake kwamba hatokaa akanyage kwenye ile ofisi , Mzee akafikiri utani asubuhi yake jirani kamuamsha mwanae huyo aende akafungue ofisi Kuna fundi anakuja kufanya KAZI dogo akagoma kabisa na kumuwekea ugumu babake, baba alivyotishia kumchapa dogo akadinda na kudai akidhubutu kurusha ngumi dogo nae atarudisha na atamfanyia kitu kibaya ikiwemo kumfikisha kwenye vyombo vya dola, dogo YUPO form four, jirani alipagawa akafikia hatua ya kufungashia virago vyake mwanae nje atafute pa kwenda, haya yote yanafanyika mke wa jirani alikuwa kanisani, basi jirani akanifuata nimpe ushauri juu ya huyo mtoto wake maana mtoto alifikia hatua ya kumwambia baba yake kwamba hapa ni Kwa mama yake kama kuondoka aondoke yeye ( jirani)
Baada ya kwenda kuutuliza msala na kutoa ushauri dogo akaendelea kukaza Yaani anataka baba ndie amuombe msamaha mtoto, nikamshauri jirani amuache amalize shule halafu akishaingia kitaa akajitegemee Kwa Sasa amuache kama alivyo ,
Hawa watoto wa kizazi hiki ni balaa tupu
 
Pole sana mwamba hapa Kuna jirani yangu watoto wake wawili wa kiume wametushia kumfanyia kitu kibaya baada ya huyo jirani kuwa mtata na kumchapa mmojawapo wa hao vijana wake wawili kisa ni kwamba dogo alipeleka grender kwenye ofisi ya kuchomea Ili fundi aitumie matokeo yake fundi akaenda kunywa chai akamuachia dogo ofisi dogo nae akasepa ofisi ikabaki bila mtu na Iko wazi , huyo jirani akazinguana na fundi Kwa Nini kaacha ofisi bila mtu , fundi akawaka na akasema amlaumu mwanae maanda ndio kamuachia ofisi na alitakiwa kupaka rangi baadhi ya magril Sasa huyo jirani akamwendea dogo na KUMPA kichapo , dogo kasusa na kumwambia dingi yake kwamba hatokaa akanyage kwenye ile ofisi , Mzee akafikiri utani asubuhi yake jirani kamuamsha mwanae huyo aende akafungue ofisi Kuna fundi anakuja kufanya KAZI dogo akagoma kabisa na kumuwekea ugumu babake, baba alivyotishia kumchapa dogo akadinda na kudai akidhubutu kurusha ngumi dogo nae atarudisha na atamfanyia kitu kibaya ikiwemo kumfikisha kwenye vyombo vya dola, dogo YUPO form four, jirani alipagawa akafikia hatua ya kufungashia virago vyake mwanae nje atafute pa kwenda, haya yote yanafanyika mke wa jirani alikuwa kanisani, basi jirani akanifuata nimpe ushauri juu ya huyo mtoto wake maana mtoto alifikia hatua ya kumwambia baba yake kwamba hapa ni Kwa mama yake kama kuondoka aondoke yeye ( jirani)
Baada ya kwenda kuutuliza msala na kutoa ushauri dogo akaendelea kukaza Yaani anataka baba ndie amuombe msamaha mtoto, nikamshauri jirani amuache amalize shule halafu akishaingia kitaa akajitegemee Kwa Sasa amuache kama alivyo ,
Hawa watoto wa kizazi hiki ni balaa tupu
Nakuelewa mkuu.
 
Nyie kwann sasa mlishusha mkungu wote wa ndizi si mngechukua hata kichana kimoja au viwili kupoza njaa tu halafu mnakwenda kuomba msosi kwa jurani.
 
Hahahahahhaaaa nimecheka kisa chenu na mdogo wako,hasa hapo mlipopata guts za kufunga mlango kwa nje.

Mdogo wako nae ana mtoto?

Jaribu kupata watoto wengine watapunguza makali ya utundu wa mtoto wa kwanza.

Out of Topic: sijui kwa nini nikikuona namkumbuka TIZED.

Kasie.
Utadhani Aki na Ukwa.
 
Kuna mtu alitupa kisa chake humu humu JF kuwa miaka wakiwa wadogo maza yao alikuwa anagombana sana na dingi yao ika sababu ya utoto na watoto huwa wanakuwa karibu sana na mama zao basi wao ilikuwa ni kulia na mama yao wakiamini baba mbaya.

Umri ulipokwenda madogo wakiwa sekondari form one na mdogo darasa la tano, kuna siku maza yao aliwasha moto kisa mzee kulala nje, ilikuwa usiku madogo wakamshikia baba yao kisu. Mzee alitokwa hadi na machozi akawaambia yaani mnanishikia kisu mimi, na ni baba yenu, mnajua mama yenu anataka nini kwangu?

Mzee akatoka usiku ule ule akaondoka nasikia hakurudi tena tokea lile tukio litokee.

Hawa madogo wakaendelea ishi na mama yao pekee bila dingi hadi kuwa watu wazima na kuanza kujitegemea.

Mwenyezi MUNGU sasa asivyo na masihara, huyu mkubwa akaja kuoa mwanamke ana mdomo kama mama yake.

Kijana akavumilia sana ila baadae yule mwanamke na tabia zake akaanza kumtesa kisaikolojia maana ikawa si kawaida. Kijana akajikuta anamtafuta baba yake popote alipo, akaja kukuta mzee wao alishafariki na alizikwa kitambo. Jamaa alilia sana kwenye kaburi la baba yake, akatamka maneno yote ya kuomba msamaha. Akasema amekua sasa anaelewa kwann baba hakuwa na amani na anajutia siku alimshikia kisu angejua angetulia tu siku ile.
 
Kuna mtu alitupa kisa chake humu humu JF kuwa miaka wakiwa wadogo maza yao alikuwa anagombana sana na dingi yao ika sababu ya utoto na watoto huwa wanakuwa karibu sana na mama zao basi wao ilikuwa ni kulia na mama yao wakiamini baba mbaya.

Umri ulipokwenda madogo wakiwa sekondari form one na mdogo darasa la tano, kuna siku maza yao aliwasha moto kisa mzee kulala nje, ilikuwa usiku madogo wakamshikia baba yao kisu. Mzee alitokwa hadi na machozi akawaambia yaani mnanishikia kisu mimi, na ni baba yenu, mnajua mama yenu anataka nini kwangu?

Mzee akatoka usiku ule ule akaondoka nasikia hakurudi tena tokea lile tukio litokee.

Hawa madogo wakaendelea ishi na mama yao pekee bila dingi hadi kuwa watu wazima na kuanza kujitegemea.

Mwenyezi MUNGU sasa asivyo na masihara, huyu mkubwa akaja kuoa mwanamke ana mdomo kama mama yake.

Kijana akavumilia sana ila baadae yule mwanamke na tabia zake akaanza kumtesa kisaikolojia maana ikawa si kawaida. Kijana akajikuta anamtafuta baba yake popote alipo, akaja kukuta mzee wao alishafariki na alizikwa kitambo. Jamaa alilia sana kwenye kaburi la baba yake, akatamka maneno yote ya kuomba msamaha. Akasema amekua sasa anaelewa kwann baba hakuwa na amani na anajutia siku alimshikia kisu angejua angetulia tu siku ile.
hadithi za abunuwasi
 
Back
Top Bottom