Wanandoa hii hali imewahikukukuta?

Grand Canyon

JF-Expert Member
Jan 2, 2020
456
924
Ndoa zina mengi.

Mimi nimeoa huu mwaka wa 5 na tuna mtoto mmoja. Tatizo: Mke wangu akinitengea chakula anataka nimalize chote hata nikishiba. Nikibakisha tu nyumbani hapakaliki, ataanza kulia usiku kucha na maneno mara kwahiyo mimi sijui kupika, mara mbona mgahawani huwa hubakishi na maneno mengi

Tatizo mimi si mlaji sana, na nilisha mweleza awe ananitengea kidogo ili nikimaliza aniongezee lakini wapi, huwa anajaza sahani yangu mpaka nasema hiii bagosha huu mlima kilimanjaro nitauweza kweli? Siku zingine najikaza namaliza kwa mbinde ili kuzuia vita lakini sometimes nashindwa.

Sijajua tatizo ni nini, nikibakisha tu naye anazira kula, anaondoka dining namkuta chumbani analia.

Wakuu hili tatizo umewahi kukumbana nalo? ulisovuje?
 
Mkuu iyo ni kawaida sana...mimi nina mwaka na... Hakuna kitu wake wanapenda kama sifa. Mume akishiba anajisikia vizuri sana,usiposhiba anahisi umekula sehemu au hujapenda chakula chake. Pia mume akiwa na afya mke anasifiwa anajua kulisha na kutunza anaepuka maneno toka kwa mawifi au mama mkwe.

Tena mpende sana mkeo mana anakujali,kuna wake wengine akitenga chakula yuko chumbani anachat,kula usile utajua mwenyewe.
Itoshe tu kusema ANAKUJALI.
 
Mkuu iyo ni kawaida sana...mimi nina mwaka na... Hakuna kitu wake wanapenda kama sifa. Mume akishiba anajisikia vizuri sana,usiposhiba anahisi umekula sehemu au hujapenda chakula chake. Pia mume akiwa na afya mke anasifiwa anajua kulisha na kutunza anaepuka maneno toka kwa mawifi au mama mkwe.

Tena mpende sana mkeo mana anakujali,kuna wake wengine akitenga chakula yuko chumbani anachat,kula usile utajua mwenyewe.
Itoshe tu kusema ANAKUJALI.
Kweli kabisa mkuu
 
Back
Top Bottom